Monday, September 3, 2012

Sifa 10 za kumtambua Mpenzi wa Kweli






Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatizwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha mtoto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto zinazowakabili.
Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo ni hizi zifuatazo.

1.Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.

2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri

4.Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuwa mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa kikwazo cha maisha yako, atakulinda daima.

6. Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7. Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine, hafichi hisia zake mbele za watu, atakutetea na kukufanya wa kwanza.

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9.Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.

Wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema kuna aina nyingi sana za mapenzi miongoni mwa binadamu. Hivyo ni muhimu kufahamu kuwa kupenda kwa mtu mmoja au watu kadhaa hakuwezi kulinganishwa na wengine kwa mazingira na mienendo.

Wakati fulani niliwahi kufanya uchunguzi miongoni mwa wapenzi ambapo nilikuwa nawauliza swali. “Vipi dada/ kaka, huyu ni mpenzi wako?” Wengi kati ya niliowauliza hawakupoteza hata nusu sekunde kujibu ‘NDIYO’.

Lakini watu hao hao nilipowauliza kwa mara nyingine “Unampenda kwa sababu gani?” Majibu ya wengi yalikuwa na sababu ambazo si za msingi na wengine walinyamaza au kuambulia kucheka.

Hebu wakati tunaendelea na mada hii, jiulize wewe mwenyewe ambaye una mke/mume swali kama hilo unampendea nini huyo mpenzi wako? Baada ya hapo sababu zinaweza kuwa ni kama zifuatazo “ Nampenda kwa sababu ni mzuri wa sura, tabia, umbo, na kusema kweli ananivutia” la kama hizo hazitakuwa sababu sina shaka nawe utanyamaza au utacheka.

Hii ina maana kuwa watu wengi ambao tuna wapenzi iwe wake au waume zetu, huenda tuliwapenda au tunawapenda hadi sasa bila kufahamu kwa nini tunawapenda na kitu gani kilitufanya tuwe wapenzi. Maana ikiwa ni uzuri, tabia, mvuto na sababu nyinginezo, basi lazima tufahamu kuwa uhai wa mapenzi yetu ni mdogo.

Inasemwa hivyo kwa sababu watu hubadilika tabia, sura, umbo, mvuto, ufahamu na hivyo kuweka ukomo wa mapenzi kuwa ni baada ya kutokea kwa mabadiliko hayo ambayo ni ya kawaida katika maisha ya mwanadamu, kwani ni wazi kwamba hakuna kinachodumu miongoni mwa hivyo vinavyotajwa na wengi kama sababu za kupendana.

Watalaam wa elimu nafsi na hasa Bw. Robert Stenberg walijitahidi sana kufanyia utafiti wa mapenzi na kuibuka na aina kuu kiasi cha nne ambazo wanazitaja kuwa ni PENZI LA UTIIFU, PENZI LA KUJALIANA, PENZI LA UIGIZAJI NA PENZI TIMILIFU.


Ufafanuzi unaotolewa na wataalamu hawa unaonyesha dhahiri makosa yanayoweza kufanywa na binadamu katika kuchagua au kupata wapenzi. Jambo ambalo limepelekea kuporomoka kwa uhusiano mwingi kati ya wanaume na wanawake. Wanasema penzi kamili linatakiwa kuwa na sifa tatu, ambazo ni tendo la ndoa, ukaribu na kujitolea.

PENZI LA UTIIFU

Penzi la utiifu au kama wengi wanavyolifahamu hujulikana kama ‘penzi la mahaba’. Katika aina hii ya penzi, wanaopendana hujali sana na kuendekeza zaidi miito ya kimwili. Mapenzi ya kiwango cha juu kabisa miongoni mwao hupatikana pale wanaposhiriki tendo la ndoa. Pia wanaopendana hupenda kuwa pamoja au karibu kwa muda mwingi.

Lakini kwa bahati mbaya penzi la aina hii linakosa sifa moja ambayo ni kujitolea. Wapenzi kwenye penzi hili huonekana na pengine hujiona kuwa wanapendana, lakini unapofika wakati ambapo kujitolea kunahitajika, penzi lililoonekana kushamiri hupukutika ghafla.

Kujitolea kunaweza kuwa na maana ya kuumia kwa ajili ya mwingine, kutoyumbishwa na watu wa pembeni na kuwa tayari kulinda penzi hilo kwa gharama yoyote. Kwa mfano ukiona mpenzi wako hayuko tayari kukusaidia unapoumwa, unapokuwa na matatizo, hakuhurumii unapokuwa taabuni ujue kuwa mapenzi yenu ni ya utiifu ambayo uhai wake ni mdogo.

Jambo la kufanya hapa ni kwa wapenzi wenyewe kujitambua na kuchukua hatua za kukamilisha pengo la kujaliana ili kutowapa nafasi wambea na shida za dunia kuyumbisha meli ya penzi ambayo wanasafiria, ikishindikana watu hawa wanashauriwa kutokuwa wepesi wa kuoana kwani uwezekano wa ndoa yao kutodumu ni mkubwa.

PENZI LA KUJALIANA

Penzi la kujaliana ni lile ambalo wanaopendana wanakuwa karibu mara zote na kushiriki mambo mengi pamoja. Wapenzi wa kundi hili huwa na hali ya kujitolea tofauti na penzi la utiifu ambalo tumeliangalia, lakini kasoro yao kubwa huwa kwenye miito ya mwili. Jambo la kufurahisha hapa ni kwamba wapenzi wa kundi hili wako makini kwa kila sehemu na mara nyingi huwa hawakubali kuingiliwa maamuzi ya mapenzi yao.

Lakini linapokuja suala la tando la ndoa hujitokeza kasoro nyingi za kutofikishana kileleni au kutofurahishana na hivyo anguko lao huletwa na muwasho wa mwili ambao huwasukuma wapendanao hao kutoka ndani ya uhusiano wao na kufanya usaliti.

Sasa ili kulifanya penzi la aina hii liwe imara lazima wapenzi waulizane kuhusu kutimiziana haja za mwili wanapokuwa faragha. Kama kuna kasoro kati yao si busara kufichana wanatakiwa kuwaona wataalamu wa mapenzi na kupata ushauri utakaosaidia kuondoa tatizo hilo. Hawa pia wanashauriwa kutooana haraka.

PENZI LA UIGIZAJI

Penzi la aina ya tatu linalotajwa na watafiti ni lile lijulikanalo kama penzi la Uigizaji. Hili ni lile penzi ambalo wanaopendana hukutana asubuhi na ikifika jioni tayari ni wapenzi kamili, ambapo hugandamana kama ruba, utadhani waigizaji wako kwenye matayarisho ya filamu. Ukiwatazama wanakuwa kama vichaa na msukumo wao wa kutimiza hisia za mwili huwa ni mkubwa kiasi cha kufikia kufanya mapenzi hata barabarani au kwenye sehemu za wazi.

Wapenzi wa aina hii huchukua muda mfupi sana kutangaziana mambo ya ndoa na pengine kuoana bila kufahamiana zaidi kitabia. Wanajuana asubuhi na jioni mwanamke/mwanaume keshahamia kwa mwenzake na maisha yanaanza, hapo hakuna ushauri wala muongozo wa watu wengine.

Tatizo kubwa ambalo hujitokeza katika penzi la aina hii ni wapenzi kuchokana mapema na hamu ya kufanya tendo la ndoa kupotea. “Yaani nikiwa na mume wangu sijisikii kabisa kufanya naye mapenzi, lakini kwa wengine nakuwa na hamu sana” hizi ni kauli za wapenzi wa penzi la kisinema sinema.

Mbali na hilo wapenzi wa aina hii ni rahisi kuporwa na kuanzisha uhusiano mpya, hivyo inashauriwa kuwa kwa wale ambao wanaona kuwa wako kwenye kundi hili, wajitahidi kujizuia na kupeana nafasi za kujuana zaidi kupitia ushauri wa watu wengine. Si vema kushiriki tendo la ndoa kila mara kwa staili na sehemu zile zile na pia haifai kukurupuka kuoana bila kuchunguzana tabia, ndoa za hivi hazidumu.


PENZI TIMILIFU

Aina ya mwisho ya penzi kama inavyoelezwa na mtaalamu Sternberq ni ile ya penzi timilifu. Aina hii ya mapenzi inakuwa na sifa zote tatu, yaani TENDO LA NDOA. Kwamba wapendanao huwa hawana kasoro katika eneo hili, unapofika muda wa kupeana raha hufikishana mahali pa juu. UKARIBU kwamba muda wote huwa karibu na kila mmoja hakai na kiu ya kutokumuona mwenzake kiasi cha kupoteza hisia na kushawishika kufanya usaliti.

Sifa ya mwisho ni KUJITOLEA. Ni mahodari kusaidiana, kufarijiana na hawako tayari kupokea mambo kutoka pembeni yanayohusu uhusiano wao, hivyo huwa si rahisi kwao kuyumba kwa sababu za umbea. Kumbuka katika penzi hili tendo la ndoa huwa si sehemu muhimu sana kwa wapenzi, yaani kwao penzi ni rohoni zaidi kuliko mwilini hata wakikaa muda wa miezi mitano bila kufanya tendo la ndoa upendo wao haupungui.

Hata hivyo, penzi la aina hii kwa mujibu wa wataalamu ni vigumu kupatikana na ni vigumu pia kulilinda, lakini linatajwa kuwa ni aina ya penzi bora ambalo ni muafaka kwa maisha ya baadaye ya ndoa kwa wanaopendana. Watu wengi kwa kutotambua aina hii ya mapenzi wamejikuta wakiliharibu kwa kufikiri tu kwamba wapenzi wao wamefika na hivyo kufanya makusudi ya kuharibu misingi ya penzi.

“Nimeshamshika atakwenda wapi, nikikohoa tu anaitika” Kauli kama hizi ni hatari sana katika penzi hili, hivyo inashauriwa ukiona unapendwa na mpenzi wako katika aina hii ya penzi ni vema ukawa macho ili kutolivunja kwa uzembe wako na kudhani unababaikiwa kumbe unapendwa kwa dhati.

Labels: ,

***Play gal – 61 (Revenge)







Ilipoishia..

“..Jerry haiwezekani mwanangu wa damu yangu kabisa eti amchukue Tina anajua tulivyompata..?, embu subiri nakuja sasa hivi..?”
Aisha alionekana kuwa na hasira zaidi kwani aliinuka kwa hasira na kwa shari. Nilichomoka kwa haraka huku nikielekea chumbani kwangu kumuwahi mwanangu Adrian lakini kabla sijafika chumbani Aisha akawa tayari ameshaniona kwa mbali kidogo akaniita kwa sauti ya kupaza na ya ukali..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaa….??????????????”

Sasa endelea…

Nilionesha woga uliochanganyika na kusita sita huku nikibaki njia panda nisielewe nimsubiri Aisha afike karibu au niingie ndani kumchukuwa mwanangu Adrian.
”..aahh..??  liwalo na liwe bwana..?”
Nilijikuta najijaza moyo wa kijasiri huku  nikiingia mpaka chumbani kwa nguvu zote nikimchukuwa mwanangu Adrian ambaye bado alikuwa kapitiwa na usingizi mzito. Nilijitahidi kufanya haraka haraka nikakusanya vitu muhimu ikiwa ni pamoja na mkoba mkubwa uliokuwa na hela kidogo na nguo za mwanangu Adrian. Kadri nilivyokuwa naendelea kupaki kwa haraka haraka ndivyo na sauti ya viatu ilioashiria kuwa Aisha yupo njiani anakuja ilikuwa ikiendelea kunishtua ndani ya fikra zangu. Sasa nikawa Tina sugu haswaa tena yule ambaye hasikii la mkuu. Nilichukuwa khanga nakumfunga mwanangu Adrian mgongoni kisha ule mkoba nikauweka kwapani na baada ya hapo nikafanya ishara ya msalaba huku kichwa na mikono yangu nikikielekezea juu.
“..eeh Mwenyezi Mungu nisaidie nakunilinda..”
Nilijisalia kimoyo moyo nakuanza kutoka huku nikifuatisha mlango ule ule wakutokea. Ile nakata kona ya kutokea kwenye kikorido uso wangu moja kwa moja ukakutana na rafiki yangu Aisha.
“..unakwenda wapi na mwanangu unampkeleka wapi..?”
“..mwanako..? leo hii ndio amekuwa mwanako..? Aisha kipenzi nashukuru kwa wema wako ulionifanyia ila kumbuka huyo Jerry ni muongo kakudanganya kwanza sijawahi kuonana naye toka kipiindi kile tulivyomfanyia mchezo ule..??”
Nilijitahidi kumdanganya Aisha lakini ndio kwanza kama nilikuwa naamsha mishipa yake ya hasira kwani alivimba nakutuna mara mbili ya Aisha yule nimjuaye mimi. Hakutaka kabisa kuniamini hata chembe na alichofanya nikukimbilia moja kwa moja kunivua khanga ile niliyokuwa nimembebea mwanangu Adrian.
“..Aisha niache mbona huni..?”
Kabla sijamalizia kuongea chochote nilishangaa  Aisha kunitupia kibao katika shavu langu nakuanza kujihisi kizunguzungu. Sikutaka kabisa kumlegezea zaidi yakuendelea kuing’ang’ania ile khanga asiweze kuifungua kwani kama angeweza kuifungua ingekuwa rahisi kumchukuwa mwanangu Adrian.
“..Jerryyyy???????? Jerryyy  njoo nisaidie..?”
Maskini Tina mimi nikawa katika vita kubwa yakuteteta  mwanangu Adrian asiweze kuwa mikononi mwa Jerry na huyu Aisha kwani nilishajiwekea dhamira ya kutomwachia na kama nitafanya hivyo maisha yangu yatakuwa mabaya zaidi kwani sina tena kizazi wala uwezo wakuweza kuzaa Tina mimi.  Makelele aliokuwa ameyatoa Aisha yakumuita Jerry  tayari yalikuwa yameshapenyeza katika ngome ya masikio ya Jerry na kwa muda huu nilianza kuhisi sauti za viatu tena ikitembea kwa mwendo wa haraka haraka. Nilichokifanya niliinua mkono wangu nakuudumbukiza moja kwa moja mpaka kwenye mkoba nakuchomoa chupa ya maziwa ya mtoto ambayo ilikuwa bado na maziwa yamoto nakisha kumwagia Aisha usoni. Aisha aliinama chini nakuanza kutapatapa huku mikono yake yote miwili akijiziba usoni na kufikicha kwa yale maumivu niliyokuwa nimempatia. Aisha akiwa bado anagala gala pale chini, nikarudishia lile dumu la maziwa nakisha nikaongoza kuelekea sebuleni. Ilinichukuwa hatua tatu tu uso kwa uso na Jerry mwenyewe na tena safari hii aliweza kuchukuwa mikono yake nakuziba njia ili mnisieweze kutoka Tina mimi.
“..kwanza nahakikisha nakuua..?  na pili namchukuwa huyo mtoto  wangu pumbavu mkubwa wewe..?”
“..hapa tutauana na siyo kuniua na kuhusu mtoto  sahau laba nife naye hapa sasa hivi..? baradhuri wewe usiye na hata huruma kwa binadamu. Umeniharibia shule sawa nimekubali ila kuhusu kumpata huyu mtoto ilo sahau Jerry..?”

Hasira kali ziliendelea kunitawala ndani ya halmashauri ya ubongo wangu. Kwa safari hii mwanangu Adrian alikuwa ameshahamka na tayari alikuwa akilia kwa sauti ya juu. Nilitamani japo nimshike nakumbembeleza lakini sikuweza kwani tayari Jerry alikuwa karibu yangu na alikuwa kaniwekea mikono yake shingoni mwangu. Nilijihisi kutapika kwani Jerry alidhamiria kuninyonga kutokana na mikono yake kushikana vilivyo na shingo yangu.
“..nakufa jamani nioookooeenn..?”
Nilijitahidi labda kutoa sauti   huenda majirani watanisikia lakini wapi ? haikusaidia chochote zaidi ya Jerry kukaza zaidi mikono yake huku nikihishiwa pumzi nakuanza kutapatapa mithili ya wacheza mieleka wakiangushana. Kitendo cha mimi kuishiwa nguvu kilimpa faraja na nguvu ya ajabu Jerry yakuweza kunifungua ile khanga yangu niliokuwa nimembebea mwanangu Adrian na kisha akamchukuwa mwanangu Adrian.
“..twende mwanangu huyu shetani hafai angekuua..?”
Jerry alimwambia mwanangu Adrian huku akimbusu japokuwa alikuwa mdogo sana kwani hakuweza kuelewa chochote zaidi ya kutoa macho.  Jerry alifanikiwa kumchukuwa mawanangu mikononi mwangu na kwa safari hii hakutaka hata kumuaga Aisha kwani bado Aisha alikuwa anatapatapa huku akiendelea kufikicha macho yake yaliokuwa nimeyamwagia maziwa ya moto ya mtoto.
Nilijiona sijielewi elewi kwani kila nikitaka kuinuka bado nguvu ziliniishia kabisa na pia shingoni kwangu kulikuwa kunauma sana. Taryari nilianza kuvuta taswira siku niliomchukuwa Adrian pale Ubungo nakutokomea zangu nakufananisha lile tukio kama tukio hili alilonifanyia Jerry leo hii. Mawazo mengi yalikuwa yanaendelea kutawala akili yangu huku nikiwa kama mtu aliyepigwa na bumbuwazi kwani nilijihisi mwanangu Adrian yupo tu kuwa hii ni ndoto lakini jibu lilibaki pale pale kila nilipomwangalia Aisha akiendelea kutapatapa.
“..dada twende nimeshamaliza kazi..?”
Nilikuwa kama sijiamini amini kwani ndani ya muda mfupi nilimshuhudia mfanyakazi wa ndani wa Aisha akiwa kambebelea mwanagu Adrian huku kamzungushia khanga zile zile alizonipora nazo Jerry pamoja na mtoto.
“..unasemaje..? na Jerry yuko wapi..?”
Bado nilikuwa sijiamini amini kama mwanangu Adrian amerudi mikononi mwangu tena. Nilitoka haraka mpaka eneo alipokuwa amesimama yule mfanyakazi. Nilipata furaha ya ajabu kwani kiukweli sikuweza kuamini kama kweli mwanangu Adrian amenusurika kuwa mikononi mwa Jerry.
“..embu niambie umemfanyaje Jerry mpaka umempata huyu mtoto..?”
“..wewe mwenyewe si unamuona huyo Jerry hapo chini alivyo..?”
Niligeuka tena kwa mara ya pili nakumuangalia Jerry vizuri lakini bado alionekana akitapatapata huku pembeni kukiwa na sufuria kubwa.
“yaan bado sijaelewa chochote..?”
“..ujue nini dada..?”
“eeh niambie..?”
“..wakati mnagombana kuhusu mtoto hapo kwenye korido nilikuwa nikiwasikia tu kwa muda mrefu huku nikiendelea kumtayarishia dada Aisha maji ya kuoga. Kadri mlivyokuwa mnaendelea kugombana na maji ndivyo yalikuwa yanazidi kuchemka. Nilipomaliza ile natoka tu nije kumwambia kuwa maji tayari nashangaa nakuona wewe ukiwa chini unatapatapa vivyo hivyo na kwa dada Aisha. Kwa hiyo nilichoamua nikuchukuwa sufuria hivyo hivyo likiwa na maji ya moto nakumwagia jerry ambaye alikuwa kamchukuwa mtoto na kumwagia mgongoni mwake kisha nikamuhai kumchukuwa mtoto. Na nilipoimchukuwa mtoto nilimmalizia kumwagia Jerry yale maji ya moto sana mpaka eneo lote la usoni mwake kwani niliona yeye ndiye chanzo cha matatizo ya kumgombea huyu mtoto hapa..”
“..ohh ahsante sana kwa kunisaidia nakumsaidia huyu mtoto..?”
“..usijari Anti.. ila hapa mie kama nitakamatwa nitafungwa tu..?? hivyo nakuomba tutoroke wote samahani Anti twende kabla majirani wala mlinzi hajatokea hapa..??”
Kwakuwa huyu Dada alikuwa ameshanisaidia kumpata mwanangu  Adrian na pia alinisaidia kmteketeza Jerry hivyo haikuwa na budi kumchukuwa. Nilimpa mwanangu Adrian na kisha nikamfuata Jerry pale chini nakuanza kumsachi mifukoni mwake ili nitafute funguo za gari lake niweze kutoroka. Nillifanikiwa kuzipata ndani ya muda mfupi.
“..chumbani kwa Aisha wapi..?”
Nilimuuliza yule mfanyakazi akanionesha.
“..nipe huyo mtoto na nakupa dakika mbili tu uingie usachi anapoweka hela zake kisha kwa haraka urudi tutoroke kabla mambo hayajawa makubwa hapa.”
Yule mfanyakazi alifanya kama nilivyomuelekeza na ndani ya muda mchache tayari alikuwa amerudi kashikilia bahasha ndogo ilioonesha ndani yake patakuwa na kile nilichomuagiza.
“..haya twende haraka haraka na tukifika hapo nje usioneshe kuwa na haraka haraka mlinzi atatugundua sawa..?”
“..sawa nimekuelewa Anti..?”
Nilimchukuwa mwanangu Adrian na kisha nikatoka na yule mfanyakazi huku nikimsihi mlinzi afungue geti nimuwaishe mwanangu hospitali anaumwa ghafla. Aliniuliza kuhusu Jerry na Aisha wako wapi hivyo nikamjibu kuwa wako chumbani kwao wametuachia ufunguo wa gari hivyo tunaenda hospitali hapo jirani nakurudi na huyu mfanyakazi wameniambia niende naye anisaidie.
Ndani ya dakika chache tayari tulikuwa nje ya geti huku nikiendesha gari la Jerry. Pembeni yangu alikuwa yule mfanyakazi huku mwanangu Adrian akiwa anatoa tu macho pembeni yetu. Giza lilikuwa limeanza kuwa tororo kwani saa ya kwenye gari ilionesha tayari imeshatimu saa sita kasoro. Hata magari tuliopishana nayo hayakuwa mengi sana kwa usiku huu. Tulikuwa hatujielewi tunaelekea wapi lakini wazo likanijia la kuwa tuna pesa tulizozichukuwa chumbani kwa Aisha.
“..ile bahasha uliochukuwa si unayo hapo..?”
Nilimuuliza yule mfanyakazi niliokuwa nimetoroka naye.
“..ninayo tena wala haiko mbali hapa..?”
“..ni kiasi gani cha pesa ulichochukuwa..?”
“..sijui ila ngoja niangalie vizuri..”
Yule mfanyakazi aliichukuwa ile bahasha ambayo ilikuwa imetuna vilivyo kuashilia kuwa amechukuwa hela nyingi sana. Kadri alivyokuwa anaingiza mkono kwenye ile bahasha ndivyo nayeye alikuwa akibadilika sura nakutetemeka nakuwa kama mtu mwenye hasira sana. Ilinibidi kulipaki gari pembeni nakumuuliza.
“..vipi embu toa ni shilingi ngapi zipo hapo..?”
Maskini tina mimi nilikuwa nimeshaingia tena matatizoni kwani alivyochomoa ile bahasha haikuwa na pesa yeyote zaidi yakutoa bastola na kisha kunielekezea kwenye paji langu la uso.
“..samahani najua huna hatia ila inanibidi kufanya hivi..?”
“..jamani kwani imekuwaje..??  nimekufanyaje wee binti..?”
“..Anti..? wala hujanifanya chiochote ila ninachotaka kusema namtaka mwanangu na wewe shuka chini sasa hivi kabla sijakufyatua..?”
“mwanako..? yupi..?  huyu hapa Adrian…?”
“..ndio ni mwanangu kabisa  wa damu na mimi ndio niliokuwa nimemzaa. Siri kubwa ilioko ni ya mimi na dada Aisha kuhusu huyu mtoto. Dada Aisha pale unapomuona hawezi kupata ujauzito kwani ameharibika kizazi kwa kutoa sana mimba ovyo kipindi cha nyuma. Na Jerry alikuwa akihitaji mtoto kwa udi na uvumba lakini kwa Aisha ikawa haiwezekani na ndipo wakaamua kunishirikisha mimi nilale na mlinzi wa pale ili nishike mimba niwazailie mtoto ambaye ndiye huyu uliokuwa umempora kutoka kwao.
Inaniuma sana huyu mtoto kumuona akihangaika kwani nilijifungua kwa operesheni na hapa unaponiona bado nyuzi hazijakaza vizuri katika maumbile yangu ya sehemu za siri. Sasa sina jinsi zaidi ya kumrudisha mwanangu mikononi mwanangu na wewe sihitaji kukuua ila shuka mwenyewe niache na mwanangu nitajua nitakapoelekea..?”





*** Najua play gal haiwezi kuisha utamu hata siku moja na mwisho wa hii ni **Play gal – 80


***Ki blog nawaombeni sana tuishie hapa na punde kitabu kikiwa tayari muda wowote kuanzia hivi sasa nitawajulisha..


**Kama unakihitaji ni inbox ili nikuweke katika orodha ya watakaokipata au andika jina lako unalotumia facebook then kikiwa tayari nitakushtua..
By admin..
Andrew Carlos Andrew (Andy Ryn)
Executive director,
Rusago  entertainment company ltd.
+255 713 133633,
 Facebook; Andy Ryn

Labels:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU 03. 09. 2012

Magazeti YETU









Labels:

Friday, August 31, 2012

Mambo 10 yanayozuia mafaniko ya kimasomo



UMASIKINI

Umasikini ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya wanafunzi kimasomo, lakini tunashauri kwamba kila mwanafunzi anayetoka katika familia masikini ajitambue na awe tayari kuishi sawa na kipato cha familia yake wakati akitafuta elimu.

Ni muhimu kwake kubana matumizi na asiwe mtu wa kujihukumu kwa kukosa hili na lile, awe mvumilivu na mwenye kuomba msaada kila sehemu anayoona hawezi kuivuka kwa nguvu zake. Uaminifu, bidii na utii unaweza kumsaidia kuvuka kikwazo hiki.

Kuhusu suala ya kufukuzwa shule kwa kukosa ada ni vema kwa mwanafunzi mwenye kipato kidogo akawasiliana na mwalimu wake au viongozi wa serikali ili wamsaidie kutatua tatizo. Haifai kujifungia chumbani na kuanza kulia au kuamua kuacha shule kwa kukosa mahitaji. Mambo yote yanawezekana kinachotakiwa ni nia, mipango na uvumilivu.


MAPENZI

Kama kuna mtu hafahamu nini maana ya mapenzi basi kuanzia leo ajue kuwa mapenzi ni ulevi kama vilevi vingine. Mtu anayependa hulewa na kujikuta anaharibu ufahamu wake kama mtu aliyelewa pombe.

Walevi wa mapenzi huweza kufanya mapenzi hata barabarani sehemu ya wazi, huku akili zao zikiwapa taarifa kwamba watu hawawaoni, mambo ya aina hii hufanywa pia na walevi wa pombe.

Lakini ulevi wa mapenzi una nguvu kubwa ya kuiteka akili na kumtia mtu mshawasho kiasi cha kuacha kazi muhimu na kukimbilia kufanya ngono.

Hivyo, mwanafunzi ambaye anataka mafanikio ya kimasomo lazima aweke kando masuala ya mapenzi kwa lengo la kutoitwika akili mzigo ambao kwa umri wa wanafunzi wengi hasa wa kike ambao ni waitikiaji wa kauli za wavulana ni vigumu kwao kuhimili.

Licha ya baadhi ya watalaamu wa masuala ya afya kubainisha faida za kufanya mapenzi kwa afya ya mwili, bado uchunguzi unaonyesha kuwa wanafunzi wengi ambao wengi wao huwa katika umri mdogo hushindwa kuzuia hisia za mapenzi na kujikuta wanakuwa watumwa wa ngono.

Mapenzi kwa mwanafunzi yana hasara za aina mbili. Kwanza, mapenzi yanapokuwa moto huteka hisia na kumfanya msomi atumie muda mwingi kuwaza juu ya mahaba na hivyo kuufanya ubongo uone kuwa mapenzi ni kitu muhimu na hivyo kujituma kuhifadhi mambo ya mapenzi kuliko masomo.

Jambo la pili ni machungu ya mapenzi hasa yanapokuwepo mafarakano, mfano kuachwa, kusalitiwa, kuudhiwa, kugombana na migogoro yote ya kimapenzi huleta msongo wa mawazo na kumfanya mwanafunzi asiweze kusoma kwa kiwango stahili. Hivyo, inashauriwa kuwa mwanafunzi asijihusishe kabisa na mapenzi.

MIGOGORO YA KIFAMILIA

Kizuizi kingine cha kufanikiwa kimasomo kwa mwanafunzi ni kuwepo katika familia zenye migogoro. Baba na mama hawaelewani, ndugu wanagombania mali na kadhalika. Lakini inashauriwa kuwa mwanafunzi anayetoka katika familia za aina hii hatakiwi kujiingiza katika misuguano ya kifamilia.

Anachotakiwa yeye ni kuwaza juu ya masomo na kutupilia mbali mawazo yote yanayochipuka kuisumbua akili kuhusu mambo makubwa ya kiukoo. Kimsingi ufahamu wa mtoto hasa wa madarasa ya chini ni mdogo, hivyo hawezi kutatua mambo ya wazazi na akijaribu atakuwa anajisumbua na kujiweka katika matatizo makubwa zaidi.

Jambo muhimu kwake katika ngazi ya maisha yake ya shule ni kusoma na kama atakuwa na kitu cha kulilia ni mahitaji ya shule tu, na akiona migogoro hiyo inaathiri masomo yake, labda ada hazilipwi anachotakiwa kufanya ni kuwaeleza wazazi na ndugu wamsaidie kuhusu haki yake ya kupewa elimu na akishindwa katika ngazi hiyo awasiliane na viongozi wa serikali kwa ngazi yake ili wamsaidie.

KUFIWA NA WAZAZI/WALEZI

Uchunguzi unaonesha kuwa watoto wengi hushuka kimasomo baada ya wazazi au walezi wao kufariki. Hapa kuna mambo mawili, kwanza ni huzuni na pili kukosa upendo toka kwa walezi wao wapya.

Kuhusu huzuni mwanafunzi aliyefiwa na wazazi anashauriwa kuacha kabisa kuishi na wazazi wake waliokufa kwenye akili, haitakiwi muda wote kuwaza jinsi wazazi walivyokuwa wakimfanyia mema katika maisha. Wanasaikolojia wanasema hakuna jambo baya la asili isipokuwa mawazo ya mtu mwenyewe.

Ieleweke kuwa jinsi mtu anavyowaza ndivyo anavyojiumiza, huku ukweli ukibaki kuwa hawezi kuwarudisha wazazi wake duniani. Hivyo basi kila wakati mwanafunzi ambaye ni yatima anapoingiwa na mawazo ya kuwakumbuka wazazi anatakiwa kuyaacha kwa kuzungumza na wenzake, kucheza au kutazama sinema za kufurahisha. Si busara kutazama picha za wazazi enzi za uhai wao na kupendelea kuwazungumzia kila mara.

MALEZI YA BUGHUDHA

Baadhi ya watoto ambao wanalelewa na ndugu au walezi ambao si wazazi hukumbwa na kadhia ya kubughudhiwa kwa matusi na maneno ya masimango, kupangiwa kazi ngumu na kunyimwa muda wa kujisomea. Usumbufu huu wa kimalenzi upo hata kwa baadhi ya wazazi ambao wanakasumba za kubagua watoto.

Lakini ushauri unaotolewa hapa ni kwamba maisha siku zote hayana njia ya mkato na watafiti wa masuala ya maisha wanasema misukosuko ya kimaisha ina faida kwa watu wenye uelewa. Wakomonisti wanasema huwezi kutambua uwezo wa nahodha kwenye bahari iliyotulia bali kwenye dhoruba kali.

Ni wazi kuwa mwanafunzi anayesumbuliwa kwa bughudha ana nafasi kubwa ya kushinda masomo kama atazichukua kadhia hizo kama changamoto za kumfanya asilale na kujitambua kuwa yuko kwenye bahari chafu isiyo salama.

Ukiwa kwenye familia za aina hii, soma kwa bidii, usijihukumu sana, jishushe na uwe tayari kutumia unachopewa bila kunung’unika, usijibu mapigo kwa ugomvi au kufokeana na wakubwa wanao kulea. Uwe tayari kutumika kama mtumwa ili baadaye uishi kama mfalme. Ila kama mambo yatazidi pendelea kushauriana na wazee wa ukoo au majirani ili wakutanue mawazo.

STAREHE

Maisha ya shule yanakata nidhamu ya matumizi ya pesa, muda na sheria za shule. Mwanafunzi hawezi kufanikiwa kimasomo kama ataendekeza mambo ta starehe, mfano kwenda disko, kukesha baa na kushiriki mapenzi na wanawake/wanaume kwenye majumba ya anasa.

Haishauriwi mwanafunzi kuwa mtu wa starehe kwani ni rahisi sana kwake kupata matatizo ambayo yanaweza kumharibia masomo yake, mfano kupigwa na kuumizwa, kukamatwa na polisi na kuhusishwa na matukio ya uhalifu na hata kukosa muda wa kuupumzisha mwili na akili.

UFUNDISHAJI DUNI

Walimu wasiokuwa na sifa za kufundisha ni tatizo kwa mafanikio ya mwanafunzi kimasomo, lakini wakati huo huo uhaba wa walimu nao huchangia kushusha kiwango cha kufaulu. Inashauriwa kuwa wanafunzi ambao hawafundishwi vizuri wamuone mwalimu wao wa taaluma na kumueleza tatizo lao ili ufumbuzi upatikane.

Lakini wakati huo huo ni sahihi kuwasiliana na wazazi/walezi na kuwataarifu uhaba wa walimu kwenye shule yako na kuwataka wakusaidie. Inaposhindikana kwa ngazi ya familia ni vema viongozi wa kitaifa wakajulishwa na hatua za kuhama shule zinaweza kufikiwa endapo kikwazo hiki kitakosa ufumbuzi.

UKOSEFU WA VIFAA

Shule nyingi zimekuwa hazina vifaa vya kutosha, hili nalo ni tatizo kubwa na dawa yake ni kwa wazazi wanaojiweza kuhakikisha kuwa wanawanunulia watoto wao vifaa binafsi vya kujisomea. Wakati huo huo ni wajibu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali kuwa na utamaduni wa kubadilisha vitendea kazi ili kupata unafuu wa tatizo hili.


KUHAMISHWA SHULE

Mwanafunzi anapohamishwa shule anaweza kuathirika kisaikolojia, lakini kama imebidi ni vema akatumia vidokezo nilivyoeleza huko nyuma katika kupata uenyeji na kuzoea mazingira mapya.

Haipaswi kuhuzunikia marafiki na walimu alioachana nao na kusahau kuwa yeye anajukumu la kusoma kwa bidii na kupata matokeo mazuri.

UDHALILI

Kuna wanafunzi ambao wanashindwa kufanikiwa kimasomo kwa sababu wanajiona wao ni duni mbele ya wenzao katika mavazi, uwezo wa kifedha na kadhalika. Kwao linakuwa ni jambo ngumu kujieleza mbele ya wenzao na muda wote hujawa na aibu na hali ya kutojiamini.

Kasoro hii ni kubwa na huwakwamisha wengi katika kupata uelewa wa mambo. Ni wajibu wa mwanafunzi kujiamini na kutupilia mbali aibu na kueleza hisia na kile anachofahamu mbele ya mwalimu na wanafunzi wenzake bila kujali kama atakosea au atachekwa. Mwanafunzi anatakiwa kuwa na mazoea ya kubadilishana mawazo na wengine na kuacha kujitenga.

Tabia hii si nzuri, mwanafunzi ambaye anataka kuwa na kumbukumbu juu ya yale aliyojifunza lazima awe tayari kushirikiana na wenzake katika kusoma, kujadiliana na kusaidia.

Labels: ,