Monday, August 13, 2012

***Play gal - 58 (Revenge)


                                                 






http://bossip.files.wordpress.com/2012/05/black-woman-crying.jpg?w=366
*** Play gal – 58 (Revenge)

Ilipoishia…
Niliumia sana moyoni kwa maneno aliokuwa akinitolea yule meneja nakujiona kuwa sifai na sina hata haja ya kuishi hapa duniani.
“..Adrian..? najua wewe huna hatia lakini sina jinsi inabidi nikuhifadhi nakukulea mpaka utakapokuwa kwa hali yeyote ile. Kubali vitu vyote utakavyokutana navyo ukiwa na mimi mpaka utakapokuwa mkubwa..?”
“Nilijikuta naongea na mwanangu Adrian japo alikuwa haelewi ninachokiongea kwakuwa bado mchanga sana lakini alitoa tabasamu nakunifanya nimbusu paji la usoni mwake nakuelekea kituo cha dala dala huku nisielewe ninapoelekea.
Sasa endelea…

“..nitaishi tu, Mungu ndio ajuaye..!”
Nilijikuta naongea peke yangu huku mwanangu Adrian nikimuweka vizuri kwani alikuwa ameshalala. Ilinichukuwa zaidi ya dakika karibu kumi nzima nikiwa nimezubaa peke yangu kituo cha daladala huku nikifikiria nitaelekea wapi na huyu mtoto. Akili yangu ikawa si ya Tina yule wa zamani bali ni ya Tina mlezi tena yule wa mlezi wa katoto kachanga ‘Adrian. Hatimaye nikaingia kwenye daladala iendayo mwananyamala na bado nilikuwa sijielewielewi.
“…Sitakuacha na wala sintokuwa msaliti kwako mwanangu Adrian..!!”
Bado niliongea peke yangu nilipoingia kwenye daladala. Baadhi ya abiria karibu wote ndani ya daladala walikuwa wakinishangaa sana na nadhani nikutokana na kuonesha sura ya huzuni na kuchanganyikiwa kwa mawazo juu ya mwanangu Adrian. Safari ya kutokea Temeke na kuelekea Mwananyamala ilianza. Njia nzima nilikuwa mtu wa mawazo tu haswa ni jinsi gani nitaishi huko niendako. Kuna wakati nilifikiria hata kwenda pale chuo kwa rafiki yangu Aisha japo anipe ushauri wa huyu mtoto na maisha yangu kwa ujumla lakini nikaogopa kwanza kuchekwa na pili mara ya mwisho nilipata uchizi nikiwa pale chuo hivyo kama wataniona na mtoto mdogo watanishangaaa sana na kunicheka kwa dharau.
“ahh..!! liwalo na liwe bwana…!!, konda nishushe hapo magomeni hospitali..?”
Nilijikuta naghairi kufika Mwananyamala ambapo ndio mwisho wa daladala hii na ndio malengo yangu kwa ujumla japo sikujua naenda kwa nani. Hivyo akili na mwawazo yangu ya ghafla yakabadilisha mwelekeo mzima wa safari yangu. Na kwa sasa nikashuka pale magomeni hospitali na mizigo yangu kisha nikaelekea upande wa pili nakupanda daladala ziendazo Posta kwa lengo la kushukia pale chuo cha biashara CBE ambapo ndipo nilipokuwa nasoma chuo na rafiki yangu kipenzi Aisha. Saa ya kwenye daladala ilikuwa jibu tosha kuwa inaelekea saa kumi na moja ya jioni. Haikunichukuwa muda sana kwani mwendo wa kutoka Magomeni hospitali mpaka chuo cha biashara CBE ni kama dakika saba hivyo nilishuka huku nambembeleza mwanangu Adrian mgongoni.
“..twende mwanangu.., hapa ndipo nilipokuwa nasoma..??”
Tayari akili yangu ilikuwa ni sawa na ya mwanangu Adrian kwani kuna kipindi nilikuwa nikiongea naye utadhani kuwa ananielewa nakunisikia kwa ninachokiongea. Mshipa wangu wa aibu niliuweka pembeni kwa muda nakuvaa sura ya mbuzi tena yule beberu kabisa. Nilijitwisha fuko langu la lambo kichwani huku kwenye kwapa nikiuweka mkoba wangu vilivyo na mgongoni nikimbeba mwanangu Adrian tena akiwa amepitiwa na usingizi.
“..embuuu…!! embuu…!!, hivi tulikuwa tunakaa nae bweni lipi tena..?? ok..!!  ok, nimeshakumbuka ghorofa  G namba 13..”
Chuo chote cha biashara CBE kilikuwa kimya sana na najua tu ikiwa hali kama hii ni dhahiri kuwa wanafunzi wote wanakuwa katika mitihani tena ile ya kumaliza chuo. Pale getini hakukuwa na mlinzi yeyote hivyo niliingia bila ya kuulizwa na mtu yeyote. Nilipishana na baadhi ya wanafunzi wachache sana tena wale masista duu na wengine mabrazameni bila ya kujali wala kujiogopa nilipishana nao huku akili yangu yote nikulifikia jengo G namba 13.
“..samahani Anti.. eti namba 13 kuna watu…”
Nilimuuliza mdada mmoja alioonesha sura yake ni ngeni kabisa machoni mwangu kwanza hata alikuwa hanifahamu kwani hakuonesha mshtuko wowote..
“..kwani wewe unamtaka nani..? Maana wanafunzi karibu wote wanafanya mitihani kasoro wale wa mwaka wa kwanza walioingia juzi juzi ndio wapo wapo humu mabwenini..”
“..sawa..!!, unamfahamu Aisha.., anakaa chumba hicho hapo juu namba 13..?”
“..Aisha..? Aisha..??, mhhh..!! Namfahamu wewe ni nani yake labda..?”
“..rafiki yake wakaribu na nimesoma naye hapa hapa chuoni..”
“””haloooo…!!! Eti rafiki yake wa karibu nimesoma naye..??, unahadhi wewe yakutembea na Aisha..? mwenye hipsi.., shepu shepu sio la mchina.. wakutembea na  ‘Verosa’ sio daladala, bajaji wala teksi..?  
Alinitolea maneno ya umbea na yakuumiza sana roho tena kwa pozi huku mdomo akiyumbisha kana kwamba sina hadhi yakuongea naye yeye wala huyo Aisha.
“..subiri hapo hapo nikakuangalizie maana nahisi utakuwa umekosea njia kwani Aisha nimjuaye mimi hawezi kuwa na mtu kama wewe ambaye hujui hata kujipodoa wala kuoga, mwenye kunuka makwapa na hilo toto sijui ndio kojo au lijimavi limeshajinyea..?”
Aliondoka huku akiendelea kuongea maneno yake machafu na kwenda kumuita Aisha. Niliumia sana moyoni nakutamani hata kumrukia na kumpiga lakini niiliogopa kufanya vurugu yeyote katika maeneo ya hapa chuoni. Kwani niliamini nitakamatwa na tena ikijulikana nilikuwa nasoma hapa ndio nitaharibu kila kitu.hivyo nikawa mpole tena mjinga haswaa huku nimejibanza nakumsubiri huyo alieenda kumuita Aisha. Ilinichukuwa dakika kama nne nzima peke yangu. Harufu kali ya marashi ya ‘adorable’ ilioambatana na sauti ya viatu ndio ilinifanya nianze kutoa mchozi kwani ndio marashi niliokuwa nayapenda kutumia na rafiki yangu kipenzi Aisha tulipokuwa wote chuo kipindi kile.
“..Aishaaaaa..?? Aisha rafiki yangu..?”
Nilishusha fuko langu chini nakumkimbilia aisha huku nikitaka kumkumbatia lakini nilipofika karibu yake tu akanikwepa nakunifyonza huku macho akiyatoa vilivyo.
“..wee chizi vipi..?”
“..jamani Aisha embu niangalie vizuri..? umeshanikumbuka rafiki yangu kipenzi..?”
“..sauti siyo ngeni.., embu nikumbushe unatokea wapi wewe..?”
Maskini Aisha alikuwa ameshanisahau kabisa japo mimi nilishamtambua. Kuharibika kwangu sura na nyele zangu za kipindi kile vilitosha kunibadilisha nakuwa Tina feki. Hata nilipomwambia Aisha kuwa naitwa Christina ama Tina bado alikataa nakusema kuwa Tina yule wazamani alishakuwaga chizi wa mitaani na siwezi kuwa mimi. Nilitumia dakika kama kumi nzima za kumulelewesha hadi akanitambua.
“..niwewe Tina..? hata bado siamini kipenzi changu kwanini umekuwa hivyo jamani..??, shetani gani aliokutembelea Tina ukabadilika kiasi kile..?? Ona sasa mwenzako nimetoka kumalizia mtihani wa mwisho.., si tungekuwa tumemaliza wote sasa hivi Tina..?”
Aisha aliongea na mimi kwa uchungu wa hali ya juu huku akitaoa machozi kama vile mtoto mdogo. Alinitoa mule chuoni ndani nakunipeleka mpaka nje. Tukatafuta sehemu nzuri ya baa nakukaa kisha nikaanza kumsimulia yote yalionikuta kipindi sipo naye. Aliona na kufananisha maisha yangu kama vile sinema tena ile ya tamthiliya ambayo ya muda mrefu sana. Nilimuelezea kuanzia tulipoanza naye mpaka nilipomucha chuo nakuanza kufanya umalaya wangu tena kwa kumficha mambo mengi. Kuhusu kuathirika kwangu nilimficha lakini kuhusu huyu mtoto nilimdanganya kuwa ni mtoto wangu ambaye nilizaa na mchungaji yupo Mwanza kaniacha na kunitelekeza na mtoto.
“..pole sana rafiki yangu Tina, ndio maisha jinsi yalivyo. Enhee kwa hiyo unaishi wapi kwa sasa..?”
“Aisha..? hapa unaponiona sina mbele wala nyuma na naishi peke yangu na huyu mtoto wangu tena kwa kutangatanga..”
Tukiwa bado tunaongea mara mwanangu Adrian akashtuka kutoka usingizini nakuanza kulia kwa sauti ya juu. Nilimfunua vizuri nakuanza kumbembeleza huku nikimtolea maziwa kwenye chupa..
“..mtoto wako mzuri sana Tina.., anaitwa nani..?”
“..anaitwa Adrian. Kwa hiyo sasa hivi Aisha umeolewa au maana nakuona na pete ya uchumba shosti..?”
Nilimbadilishia mada asiendelee kuniuliza juu ya huyu mtoto. Alikuwa amevalishwa pete lakini hakuniweka wazi kuhusu bwana anayeishi naye ila aliniambia tu ni mfanyabiashara tena wakimataifa hivyo si mtu wakukaa sana nayeye hivyo ni kama anaishi yeye na mfanyakazi tu. Alinichukuwa pale nakuelekea mpaka eneo aliokuwa amepaki gari lake na safari ya kuelekea kwake ikaanza kwani aliniahidi kuishi na mie mpaka mtoto atakapokuwa mkubwa ama mimi nitakapopata kazi yakueleweka nakujitegemea mwenyewe.
“..Aisha..?, wewe ni rafiki wangu wa milele.., na sina rafiki kama wewe..?”
Niliongea kwa kusisimka huku uso wangu ukitawaliwa kwa machozi ya furaha. Gari lake lilikuwa zuri sana na lenye vioo vyeusi vya kumfanya mtu wanje asiweze kuwaona. Mwanangu Adrian nilikuwa nimeshamshusha mgongoni nakumlaza siti ya pembeni yangu. Muda wote Aisha alikuwa akitabasamu nakucheka na mimi karibu njia nzima na hata tulipofika kwenye foleni alikuwa akinipigisha stori za chuo nilivyoacha gumzo kwa kila anayenijua na hata kitendo cha wazazi wangu kuja kunitafuta chuoni. Kifupi nilifarijika sana nakujiona mtu mwenye bahati ya mara nyingine tena bahati ya mtende.
“..kumbe Aisha unaishi mbali hiivi…??, enhee..!! ni wapi hivi shosti maana hiyo safari hatufiki tu..”
“..weee unafikiri mbali basi..?? ni hapo bunju tu.., tukivuka aka kapori tu tumeshafika..”
Gari ilitembea kama alivyoniahidi kuwa tukivuka tu kapori tumeshafika. Giza nalo lilikuwa limeshatanda. Nilihakikisha mwanagu Adriani nimemfunika vizuri kwa ajili ya baridi ya mule ndani ya gari. Tukiwa bado tupo eneo la kale kapori mara Aisha akasimamisha gari kisha akaanza kufungua droo za mbele ya gari yake kana kwamba kuna kitu amekisahau au anakitafuta amekikumbuka. Ghafla akatoa bastola ndogo nakunielekezea kichwani mwangu..
“..hapo hapo ulipo Tina..??, usitingishike wala kuongea chochote na nitakufyatua usipotii amri hii..??”
Mapigo yangu ya moyo yakabadilika nakuanza kutemeka huku kojo likichukuwa nafasi yake kunitiririka. Nikawa siamini kwa kilichonitokea. Nilibaki kimya kama alivyoniambia Aisha huku ile bastola iking’ang’ana katika paji langu la uso vilivyo tayari kwa kufyatuka. Sikuweza kujipindua zaidi ya kusikia tu Aisha akiongea na mtu kwenye simu.
“..kazi yenu tayari haya sasa mko wapi mnipe changu..?”
Aisha aliongea kwenye simu kwa sauti ya ukali na yakikatili kisha ndani ya dakika chache mlango wa gari kwa upande wangu ukafunguliwa. Tochi zilinimulika kisha nikashikwa na watu nisiowafahamu halafu kwenye gari nikamshuhudia Jerry kiingia kisha akambeba yule mtoto na kuondoka zao na Aisha huku wakiniacha nimekumbatiwa na watu nisiowafahamu.
“..mnampeleka wapi mwanangu..??, mrudisheni..??”
Nilitoa makelele ya nguvu lakini haikusaidia chochote zaidi ya ile gari kutokomea huku wale wavulana waliokuwa wamenishika kwa kunikumbatia wakianza kunivua nguo zangu na zao tayari kwa kunibaka kwa zamu…






*** kila siku stori inazidi kunoga je Tina atalipizaje kisasi kwa Aisha..?


*** Inamaana Jerry alishampanga Aisha kuwa kama Tina atatokea chuoni basi wamchukue mtoto halafu watalipana pesa..?? nini hatma ya Tina..?


******* hii ndio play gal (Revenge).., usithubutu kuhadithiwa hata inayofuata kwani ni kali sana zaidi ya hapa.


*** endelea kuwa nami kwa msisimko zaidi wa hadithi hii yenye ukweli ndani yake ya play gal 59

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home