Tuesday, August 7, 2012

***Play gal – 57 (Revenge)


Ilipoishia….

Nilichokifanya nilimfanyia yule mzee ishara ya kumnyamazisha kwa kutumia kidole changu kukiweka mdomoni, kisha nikamchukua mwanangu Adriani hivyo hivyo akiwa analia nakumtupia uvunguni mwa kitanda na baada ya hapo nikaelekea moja kwa moja mpaka mlangoni tena kwa kujiamini huku nimejifunika khanga nakuufungua mlangu nusu.
“eenhe unasemaje..?”
Uso wangu kwa sasa ukawa umekutana moja kwa moja na Mmama ambaye sura yake si ngeni kabisa machoni mwangu huku akibubujikwa na machozi yalioambatana na kwikwi na nilipomuuliza tu kuwa anasemaje. Pale pale alinisukuma nakuingia mpaka chumbani kwangu kwa nguvu…

Sasa endelea….

“...Hivi jamani nikupe nini ili uridhike mwanaume wewe..? eti Baba Jose..? Kwanini unanifanyia mimi hivi..? kitu gani hujaridhika kutoka kwangu..? kitu gani sikupi mie..?”
Nilishusha pumzi chini huku macho yangu nikiyatoa kwa tahamaki nikiendelea kumshuhudia yule Mama akilalama. Kumbe yule mzee niliokuwa nafanya nae mapenzi alikuwa ni mume wake wa ndoa. Na kwa sasa alikuwa kama kishamfumania akiwa na mimi. Aliendelea kumlalamikia sana mume wake huku akimshika shingoni vilivyo.
“..Lakini mama Jose..?”
“..lakini nini..? hivi kweli baba Jose ndio mchezo wako huo unaofanyaga..? lini utakuwa mume wangu..? kama ni watoto tunao wanne, badala tupange ni jinsi gani tutawatunza na kuwasomesha we ndio kwanza unahangaika nakutangatanga na visichana vidogo.. embu inuka twende nyumbani huko..?”
Bado yule Mama alionekana kuwa na hasira iliyoambatana na kwikwi kali kwani kila muda alikuwa akihema kwa shida huku akiishiwa pumzi kwa hasira ambayo alikuwa nayo ya kumfumania mume wake. Akiwa bado anagombana na mume wake mara mwanangu Adrian akaanza kulia pale chini yao.
“..tobaa..!!!, na tena kumbe binti mwenyewe ana mtoto mchanga..? wewe baba Jose nini unafanya jamani..? twende..!!, twende..!!, twende nyumbani nimesema..?
Nilisogea mpaka karibu yao kiuwoga woga huku nanyata mithili ya simba anaponyemelea kitoweo nakumchukuwa mwananagu Adrian nakuanza kumbembeleza huku  nikiwaacha yule Mama na mumewe wakiendelea kuvutana. Waliendelea kuzozana tena kwa sauti ya juu nakusababisha watu waanze kuchungulia madirishanai huku wakipiga kelele za uchochezi. Baada ya muda kama wa dakika tano nzima za ugomvi na kuvutana huku na kule ndipo wakaondoka zao wakiniacha nikiendelea kumbembeleza mwanangu Adrian ambaye kwa muda huu ni kama alikuwa akizidisha kulia.
Baada ya muda kama wa dakika kumi ndipo mwanangu Adrian akaanza kunyamaza nakunifanya nijisikie faraja tele moyoni. Tabasamu aliokuwa akiendelea kulitoa ni wazi kuwa alikuwa mtoto msikivu anapobembelezwa. Niliinua mkono wangu wa kulia nakuanza kumpapasa maeneo ya shingoni, mpaka usoni mwake. Alinishtua sana kwani mwili wake ulionekana wamoto sana. Kamasi za majimaji zilizokuwa zinamtiririka kupitia puani mwake ni wazi zilionesha kuwa anaumwa. Nilimvua nguo zake haraka haraka nakuanza kumuogesha. Nikiwa bado namuogesha mara tena nikasikia kama mtu anabisha hodi. Mwanzo nilionesha kusita lakini kadri nilivyokuwa naendelea kumuogesha mwanangu Adrian ndivyo na yule mtu alizidi kupiga hodi. Nilimtoa kwenye beseni lake la kuogea nakumuweka kitandani nakuelekea mlangoni kujua ni nani alikuwa anapiga hodi.
“Mama  Adrian..? Mambo..? Samahani unahitajika na meneja yupo mapokezi..?”
“..sawa Salma.., mwambie nakuja sasa hivi..?”
Alikuwa ni rafiki yangu wa humu ndani ambaye nayeye ni mfanyakazi na yupo mapokezi na kwa muda huu alikuwa amekuja kuniiita kuwa nahitajika na meneja. Ile hali yangu ya uwoga ilianza kunitawala tena, mwili wangu wote uliishiwa nguvu nakujihisi kama ile hali ya kutetemeka imenianza tena kwani safari hii nilikuwa natetemeka sana maeneo ya mdomoni na nywele kunisisimka. Nilichokifanya nilivaa nguo zangu haraka haraka na kisha kumchukuwa mwanangu Adrian nakuelekea mpaka mapokezi ambapo ndipo alipokuwa meneja akiniita.
“..naam bosi wangu nasikia unaniita..?”
“..ndio nakuita, hivi mama Adrian kwanini unataka kutuchafulia jina hapa mtaani..?”
“..kwani vipi meneja..?”
“ina maana hujui kitu ulichofanya muda si mrefu..?”
“..anhh..!!, unajua meneja ni kwamba..”
Kabla sijaanza kumsimulia meneja. Alinikatiza kuendelea kuongea neno lolote. Sura yake ilikuwa imembadilika na hakuwa kama meneja yule wa awali niliomzoea kwani alionekana dhahiri kuchukizwa na kile kitendo cha mimi kufumaniwa na yule Mzee.
“..sitaweza kuvumilia ujinga unaoendelea kufanya kila siku humu ndani. Katafute gesti nyingine za kufanya huo ujinga hapa kuanzia sasa hatukuitaji na mambo yako ibilisi we..?”
“..Jaribu kunisikiliza na mimi basi meneja..?”
“..hapana..?, hapana nimesema siwezi kukusikiliza tena wala kukuelewa kwa namna yeyote zaidi ya kukuona umeenda huko chumbani nakutoa kila kilicho chako na ufunguo wangu nauhitaji ndani ya dakika kumi, umenisikia na kunielewa..??”
Nilikuwa sina tena ujanja Tina mimi kwani pamoja nakumpigia magoti meneja huku nikitoa machozi ya hapa na pale lakini haikusaidia chochote wala kunielewa. Inaonekana kile kitendo cha mimi kufumaniwa kilimuuma sana nakuona kuwa amechafuliwa jina na atakosa wateja. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuelekea tena chumbani nakukusanya kila kilichokuwa changu. Sikuwa na begi lakuwekea nguo hivyo nilichukuwa nguo zangu na za mwanangu Adrian kisha nikaziweka kwenye fuko kubwa la lambo, na vitu vidogo vidogo kama chupa ya maziwa na vijipodozi niliviweka kwenye ule mkoba wa kipindi kile nilioondoka nao kutoka kwa mama yake na huyu mtoto. Nilirudi mpaka pale eneo la mapokezi nilipomuacha Meneja.
“..funguo wenu huu hapa..?”
“…Nenda huko hatukuhitaji tena hapa Malaya uliokubuhu wee..?”
Niliumia sana moyoni kwa maneno aliokuwa akinitolea yule meneja nakujiona kuwa sifai na sina hata haja ya kuishi hapa duniani.
“..Adrian..? najua wewe huna hatia lakini sina jinsi inabidi nikuhifadhi nakukulea mpaka utakapokuwa kwa hali yeyote ile. Kubali vitu vyote utakavyokutana navyo ukiwa na mimi mpaka utakapokuwa mkubwa..?”
“Nilijikuta naongea na mwanangu Adrian japo alikuwa haelewi ninachokiongea kwakuwa bado mchanga sana lakini alitoa tabasamu nakunifanya nimbusu paji la usoni mwake nakuelekea kituo cha dala dala huku nisielewe ninapoelekea.


*********


*** unavyodhani Tina ataelekea wapi kuishi na tawezaje kuishi na motto Adrian angali mchanga..?

*** Nini hatma ya Tina na nini mwisho wa story hii umeshaujua..?

*** Usikubali usimuliwe endelea kuwa na mimi katika Play gal – 58 kwani ndio kama story inaanza upya….

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home