Monday, September 3, 2012

***Play gal – 61 (Revenge)







Ilipoishia..

“..Jerry haiwezekani mwanangu wa damu yangu kabisa eti amchukue Tina anajua tulivyompata..?, embu subiri nakuja sasa hivi..?”
Aisha alionekana kuwa na hasira zaidi kwani aliinuka kwa hasira na kwa shari. Nilichomoka kwa haraka huku nikielekea chumbani kwangu kumuwahi mwanangu Adrian lakini kabla sijafika chumbani Aisha akawa tayari ameshaniona kwa mbali kidogo akaniita kwa sauti ya kupaza na ya ukali..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaa….??????????????”

Sasa endelea…

Nilionesha woga uliochanganyika na kusita sita huku nikibaki njia panda nisielewe nimsubiri Aisha afike karibu au niingie ndani kumchukuwa mwanangu Adrian.
”..aahh..??  liwalo na liwe bwana..?”
Nilijikuta najijaza moyo wa kijasiri huku  nikiingia mpaka chumbani kwa nguvu zote nikimchukuwa mwanangu Adrian ambaye bado alikuwa kapitiwa na usingizi mzito. Nilijitahidi kufanya haraka haraka nikakusanya vitu muhimu ikiwa ni pamoja na mkoba mkubwa uliokuwa na hela kidogo na nguo za mwanangu Adrian. Kadri nilivyokuwa naendelea kupaki kwa haraka haraka ndivyo na sauti ya viatu ilioashiria kuwa Aisha yupo njiani anakuja ilikuwa ikiendelea kunishtua ndani ya fikra zangu. Sasa nikawa Tina sugu haswaa tena yule ambaye hasikii la mkuu. Nilichukuwa khanga nakumfunga mwanangu Adrian mgongoni kisha ule mkoba nikauweka kwapani na baada ya hapo nikafanya ishara ya msalaba huku kichwa na mikono yangu nikikielekezea juu.
“..eeh Mwenyezi Mungu nisaidie nakunilinda..”
Nilijisalia kimoyo moyo nakuanza kutoka huku nikifuatisha mlango ule ule wakutokea. Ile nakata kona ya kutokea kwenye kikorido uso wangu moja kwa moja ukakutana na rafiki yangu Aisha.
“..unakwenda wapi na mwanangu unampkeleka wapi..?”
“..mwanako..? leo hii ndio amekuwa mwanako..? Aisha kipenzi nashukuru kwa wema wako ulionifanyia ila kumbuka huyo Jerry ni muongo kakudanganya kwanza sijawahi kuonana naye toka kipiindi kile tulivyomfanyia mchezo ule..??”
Nilijitahidi kumdanganya Aisha lakini ndio kwanza kama nilikuwa naamsha mishipa yake ya hasira kwani alivimba nakutuna mara mbili ya Aisha yule nimjuaye mimi. Hakutaka kabisa kuniamini hata chembe na alichofanya nikukimbilia moja kwa moja kunivua khanga ile niliyokuwa nimembebea mwanangu Adrian.
“..Aisha niache mbona huni..?”
Kabla sijamalizia kuongea chochote nilishangaa  Aisha kunitupia kibao katika shavu langu nakuanza kujihisi kizunguzungu. Sikutaka kabisa kumlegezea zaidi yakuendelea kuing’ang’ania ile khanga asiweze kuifungua kwani kama angeweza kuifungua ingekuwa rahisi kumchukuwa mwanangu Adrian.
“..Jerryyyy???????? Jerryyy  njoo nisaidie..?”
Maskini Tina mimi nikawa katika vita kubwa yakuteteta  mwanangu Adrian asiweze kuwa mikononi mwa Jerry na huyu Aisha kwani nilishajiwekea dhamira ya kutomwachia na kama nitafanya hivyo maisha yangu yatakuwa mabaya zaidi kwani sina tena kizazi wala uwezo wakuweza kuzaa Tina mimi.  Makelele aliokuwa ameyatoa Aisha yakumuita Jerry  tayari yalikuwa yameshapenyeza katika ngome ya masikio ya Jerry na kwa muda huu nilianza kuhisi sauti za viatu tena ikitembea kwa mwendo wa haraka haraka. Nilichokifanya niliinua mkono wangu nakuudumbukiza moja kwa moja mpaka kwenye mkoba nakuchomoa chupa ya maziwa ya mtoto ambayo ilikuwa bado na maziwa yamoto nakisha kumwagia Aisha usoni. Aisha aliinama chini nakuanza kutapatapa huku mikono yake yote miwili akijiziba usoni na kufikicha kwa yale maumivu niliyokuwa nimempatia. Aisha akiwa bado anagala gala pale chini, nikarudishia lile dumu la maziwa nakisha nikaongoza kuelekea sebuleni. Ilinichukuwa hatua tatu tu uso kwa uso na Jerry mwenyewe na tena safari hii aliweza kuchukuwa mikono yake nakuziba njia ili mnisieweze kutoka Tina mimi.
“..kwanza nahakikisha nakuua..?  na pili namchukuwa huyo mtoto  wangu pumbavu mkubwa wewe..?”
“..hapa tutauana na siyo kuniua na kuhusu mtoto  sahau laba nife naye hapa sasa hivi..? baradhuri wewe usiye na hata huruma kwa binadamu. Umeniharibia shule sawa nimekubali ila kuhusu kumpata huyu mtoto ilo sahau Jerry..?”

Hasira kali ziliendelea kunitawala ndani ya halmashauri ya ubongo wangu. Kwa safari hii mwanangu Adrian alikuwa ameshahamka na tayari alikuwa akilia kwa sauti ya juu. Nilitamani japo nimshike nakumbembeleza lakini sikuweza kwani tayari Jerry alikuwa karibu yangu na alikuwa kaniwekea mikono yake shingoni mwangu. Nilijihisi kutapika kwani Jerry alidhamiria kuninyonga kutokana na mikono yake kushikana vilivyo na shingo yangu.
“..nakufa jamani nioookooeenn..?”
Nilijitahidi labda kutoa sauti   huenda majirani watanisikia lakini wapi ? haikusaidia chochote zaidi ya Jerry kukaza zaidi mikono yake huku nikihishiwa pumzi nakuanza kutapatapa mithili ya wacheza mieleka wakiangushana. Kitendo cha mimi kuishiwa nguvu kilimpa faraja na nguvu ya ajabu Jerry yakuweza kunifungua ile khanga yangu niliokuwa nimembebea mwanangu Adrian na kisha akamchukuwa mwanangu Adrian.
“..twende mwanangu huyu shetani hafai angekuua..?”
Jerry alimwambia mwanangu Adrian huku akimbusu japokuwa alikuwa mdogo sana kwani hakuweza kuelewa chochote zaidi ya kutoa macho.  Jerry alifanikiwa kumchukuwa mawanangu mikononi mwangu na kwa safari hii hakutaka hata kumuaga Aisha kwani bado Aisha alikuwa anatapatapa huku akiendelea kufikicha macho yake yaliokuwa nimeyamwagia maziwa ya moto ya mtoto.
Nilijiona sijielewi elewi kwani kila nikitaka kuinuka bado nguvu ziliniishia kabisa na pia shingoni kwangu kulikuwa kunauma sana. Taryari nilianza kuvuta taswira siku niliomchukuwa Adrian pale Ubungo nakutokomea zangu nakufananisha lile tukio kama tukio hili alilonifanyia Jerry leo hii. Mawazo mengi yalikuwa yanaendelea kutawala akili yangu huku nikiwa kama mtu aliyepigwa na bumbuwazi kwani nilijihisi mwanangu Adrian yupo tu kuwa hii ni ndoto lakini jibu lilibaki pale pale kila nilipomwangalia Aisha akiendelea kutapatapa.
“..dada twende nimeshamaliza kazi..?”
Nilikuwa kama sijiamini amini kwani ndani ya muda mfupi nilimshuhudia mfanyakazi wa ndani wa Aisha akiwa kambebelea mwanagu Adrian huku kamzungushia khanga zile zile alizonipora nazo Jerry pamoja na mtoto.
“..unasemaje..? na Jerry yuko wapi..?”
Bado nilikuwa sijiamini amini kama mwanangu Adrian amerudi mikononi mwangu tena. Nilitoka haraka mpaka eneo alipokuwa amesimama yule mfanyakazi. Nilipata furaha ya ajabu kwani kiukweli sikuweza kuamini kama kweli mwanangu Adrian amenusurika kuwa mikononi mwa Jerry.
“..embu niambie umemfanyaje Jerry mpaka umempata huyu mtoto..?”
“..wewe mwenyewe si unamuona huyo Jerry hapo chini alivyo..?”
Niligeuka tena kwa mara ya pili nakumuangalia Jerry vizuri lakini bado alionekana akitapatapata huku pembeni kukiwa na sufuria kubwa.
“yaan bado sijaelewa chochote..?”
“..ujue nini dada..?”
“eeh niambie..?”
“..wakati mnagombana kuhusu mtoto hapo kwenye korido nilikuwa nikiwasikia tu kwa muda mrefu huku nikiendelea kumtayarishia dada Aisha maji ya kuoga. Kadri mlivyokuwa mnaendelea kugombana na maji ndivyo yalikuwa yanazidi kuchemka. Nilipomaliza ile natoka tu nije kumwambia kuwa maji tayari nashangaa nakuona wewe ukiwa chini unatapatapa vivyo hivyo na kwa dada Aisha. Kwa hiyo nilichoamua nikuchukuwa sufuria hivyo hivyo likiwa na maji ya moto nakumwagia jerry ambaye alikuwa kamchukuwa mtoto na kumwagia mgongoni mwake kisha nikamuhai kumchukuwa mtoto. Na nilipoimchukuwa mtoto nilimmalizia kumwagia Jerry yale maji ya moto sana mpaka eneo lote la usoni mwake kwani niliona yeye ndiye chanzo cha matatizo ya kumgombea huyu mtoto hapa..”
“..ohh ahsante sana kwa kunisaidia nakumsaidia huyu mtoto..?”
“..usijari Anti.. ila hapa mie kama nitakamatwa nitafungwa tu..?? hivyo nakuomba tutoroke wote samahani Anti twende kabla majirani wala mlinzi hajatokea hapa..??”
Kwakuwa huyu Dada alikuwa ameshanisaidia kumpata mwanangu  Adrian na pia alinisaidia kmteketeza Jerry hivyo haikuwa na budi kumchukuwa. Nilimpa mwanangu Adrian na kisha nikamfuata Jerry pale chini nakuanza kumsachi mifukoni mwake ili nitafute funguo za gari lake niweze kutoroka. Nillifanikiwa kuzipata ndani ya muda mfupi.
“..chumbani kwa Aisha wapi..?”
Nilimuuliza yule mfanyakazi akanionesha.
“..nipe huyo mtoto na nakupa dakika mbili tu uingie usachi anapoweka hela zake kisha kwa haraka urudi tutoroke kabla mambo hayajawa makubwa hapa.”
Yule mfanyakazi alifanya kama nilivyomuelekeza na ndani ya muda mchache tayari alikuwa amerudi kashikilia bahasha ndogo ilioonesha ndani yake patakuwa na kile nilichomuagiza.
“..haya twende haraka haraka na tukifika hapo nje usioneshe kuwa na haraka haraka mlinzi atatugundua sawa..?”
“..sawa nimekuelewa Anti..?”
Nilimchukuwa mwanangu Adrian na kisha nikatoka na yule mfanyakazi huku nikimsihi mlinzi afungue geti nimuwaishe mwanangu hospitali anaumwa ghafla. Aliniuliza kuhusu Jerry na Aisha wako wapi hivyo nikamjibu kuwa wako chumbani kwao wametuachia ufunguo wa gari hivyo tunaenda hospitali hapo jirani nakurudi na huyu mfanyakazi wameniambia niende naye anisaidie.
Ndani ya dakika chache tayari tulikuwa nje ya geti huku nikiendesha gari la Jerry. Pembeni yangu alikuwa yule mfanyakazi huku mwanangu Adrian akiwa anatoa tu macho pembeni yetu. Giza lilikuwa limeanza kuwa tororo kwani saa ya kwenye gari ilionesha tayari imeshatimu saa sita kasoro. Hata magari tuliopishana nayo hayakuwa mengi sana kwa usiku huu. Tulikuwa hatujielewi tunaelekea wapi lakini wazo likanijia la kuwa tuna pesa tulizozichukuwa chumbani kwa Aisha.
“..ile bahasha uliochukuwa si unayo hapo..?”
Nilimuuliza yule mfanyakazi niliokuwa nimetoroka naye.
“..ninayo tena wala haiko mbali hapa..?”
“..ni kiasi gani cha pesa ulichochukuwa..?”
“..sijui ila ngoja niangalie vizuri..”
Yule mfanyakazi aliichukuwa ile bahasha ambayo ilikuwa imetuna vilivyo kuashilia kuwa amechukuwa hela nyingi sana. Kadri alivyokuwa anaingiza mkono kwenye ile bahasha ndivyo nayeye alikuwa akibadilika sura nakutetemeka nakuwa kama mtu mwenye hasira sana. Ilinibidi kulipaki gari pembeni nakumuuliza.
“..vipi embu toa ni shilingi ngapi zipo hapo..?”
Maskini tina mimi nilikuwa nimeshaingia tena matatizoni kwani alivyochomoa ile bahasha haikuwa na pesa yeyote zaidi yakutoa bastola na kisha kunielekezea kwenye paji langu la uso.
“..samahani najua huna hatia ila inanibidi kufanya hivi..?”
“..jamani kwani imekuwaje..??  nimekufanyaje wee binti..?”
“..Anti..? wala hujanifanya chiochote ila ninachotaka kusema namtaka mwanangu na wewe shuka chini sasa hivi kabla sijakufyatua..?”
“mwanako..? yupi..?  huyu hapa Adrian…?”
“..ndio ni mwanangu kabisa  wa damu na mimi ndio niliokuwa nimemzaa. Siri kubwa ilioko ni ya mimi na dada Aisha kuhusu huyu mtoto. Dada Aisha pale unapomuona hawezi kupata ujauzito kwani ameharibika kizazi kwa kutoa sana mimba ovyo kipindi cha nyuma. Na Jerry alikuwa akihitaji mtoto kwa udi na uvumba lakini kwa Aisha ikawa haiwezekani na ndipo wakaamua kunishirikisha mimi nilale na mlinzi wa pale ili nishike mimba niwazailie mtoto ambaye ndiye huyu uliokuwa umempora kutoka kwao.
Inaniuma sana huyu mtoto kumuona akihangaika kwani nilijifungua kwa operesheni na hapa unaponiona bado nyuzi hazijakaza vizuri katika maumbile yangu ya sehemu za siri. Sasa sina jinsi zaidi ya kumrudisha mwanangu mikononi mwanangu na wewe sihitaji kukuua ila shuka mwenyewe niache na mwanangu nitajua nitakapoelekea..?”





*** Najua play gal haiwezi kuisha utamu hata siku moja na mwisho wa hii ni **Play gal – 80


***Ki blog nawaombeni sana tuishie hapa na punde kitabu kikiwa tayari muda wowote kuanzia hivi sasa nitawajulisha..


**Kama unakihitaji ni inbox ili nikuweke katika orodha ya watakaokipata au andika jina lako unalotumia facebook then kikiwa tayari nitakushtua..
By admin..
Andrew Carlos Andrew (Andy Ryn)
Executive director,
Rusago  entertainment company ltd.
+255 713 133633,
 Facebook; Andy Ryn

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home