Monday, August 27, 2012

***Play gal - 60 (Revenge)



Ilipoishia…

Chumba kilikuwa nikikubwa sana ambapo ndani yake kulikuwa na kila kitu. Kuanzia choo na bafu. Kitanda kikubwa. Nilimvua mwanangu Adrian nguo zake nakumpeleka bafuni ambapo nilimuogesha nakisha nikambadilisha pampasi, baada ya hapo nikaoga na nilipotoka kuoga tu Aisha tayari alikuwa chumbani kwangu kitandani na Adrian ananisubiri nitoke kuoga.
“..Tina nimekuletea nguo hizi hapa, mie huwa zinanibana sana si unajua kunenepa kwangu ovyo tena..!!”
“..Ooh..!!, ahsante Aisha..”
“..ila kuna kitu nahitaji ujue…

Endelea….

Mwili wote ukanisisimka kwa haraka na ghafla kuanzia kichwani mpaka miguuni. Kutokana na kule kutetemeka nilijikuta kuishiwa nguvu mwilini nakuhisi kama kojo linaanza kunidondoka mtu mzima huku akilini nikiwa na shauku kubwa ya kujua ni kitu gani hicho anachotaka kuniambia Aisha.
“…Eennhee shosti..!!  kitu gani tena hicho mbona waniacha roho juu na njia panda mwenzako....??”
“..njoo kwanza mpaka hapa kitandani.., halafu ukiwa katika kujifuta vizuri na kubadilisha nguo mimi nitakuwa nikikusimulia, sawa shosti wangu Tina..?”
“..ni sawa tu hamna neno, au mtoko nini jamani..?”
“..mbona una haraka kiasi hicho jamani hata sijakwambia ni kitu gani..?, siyo mtoko wala nini..??”
“..Sasa ni kitu gani hicho cha kunitia roho juu mwenzangu, wangwi wangwi hadi umeninyima raha na kunipa karaha kwa muda..?”
Muda wote Aisha ailionekana kama mtu wa masihara masihara kwani ni kweli alionesha kuna kitu anataka kuniambia, lakini hakuwa siriazi kwani alikuwa akicheka cheka huku akinipa mkono kwa kugonga.
“..hivi yule mchumba wako wa zamani ‘Jerry’ ushawahi kumuona..?”
Mapigo yangu ya moyo yalibadilisha uelekeo pale aliponitajia jina la ‘jerry’. Sikutaka kabisa kumsikikia Jerry  masikioni mwangu Tina mimi na hata sura yake kwani yeye ndio chanzo cha mimi kuishi maisha haya ya shida nakutangatanga mpaka hivi sasa.
“..kiukweli shosti wangu Aisha. Huyo ‘Jerry’ ndio kwanza nakusikia unamtaja wewe leo hii, kwani toka enzi hizo sikumtia machoni na si unakumbuka alichonifanyiaga kipindi cha nyuma mpaka tukamfanyizia nakumkata kata nanihii yake kwa kutumia viwembe si unakumbuka..?”
“”..hehe heee..!!, halooo!!! Nakumbuka shosti..!!, lakini nadhani yale yalishapita siku nyingi sana, ila kuna jipya nataka nikujuze shosti wangu Tina ambalo hulijui..?”
Sasa nikatuliza pumzi zangu huku nikimtolea macho Aisha aniambie ni kitu gani hicho..
“..haya niambie shosti kwani amekuwaje huyo Jerry..?”
“ni stori ndefu sana Tina lakini maadam upo nitakusimulia kila kitu na utajua nakuelewa tu huyo Jerry. Kwanza kabisa unajua kipindi kile tumemfanyizia  kwanza hakututambua kama ni sisi ndio tulimfanyia ule unyama wa kumkatakata nanii yake kwa viwembe hadi kumpelekea kuharibika njia ya kutolea mbegu za uzazi. Tina..?”
“nakusikia endelea tu..?”
“..najua hutaweza kuamini lakini inakubidi tu uanzae kuamini kwani Jerry kwa sasa amekuwa ni mtu wa karibu sana na mimi..?”
“..bado sijakuelewa elewa Aisha , unamaanisha nini haswa..?”
“..nimekuwa msaada mkubwa sana kwa Jerry katika maisha yake.. Kuna siku moja nilikuwa naelekea kufanya ‘shopping’ zangu pale Mlimani city na kwa bahati nikakutana nae uso kwa uso. Kwa kuwa nilikuwa katika kipindi kigumu sana cha chuo si unajua tena bumu likiisha tunavyotaabika sisi..?”
“..ni kweli..?”
“..basi nikajikomba Aisha mimi kwa Jerry nakujifanya namjua kuliko. Kwa kuwa siku hiyo alikuwa peke yake ikawa ni rahisi sana kumshawishi. Jerry alionesha yuko tofauti sana kwani alikuwa ni mtu mwenye msimamo haswaa. Lakini akaniambia yuko tayari kunigharamia kiasi chochote cha pesa endapo tu nitamtekelezea mambo mawili makubwa kwake..?”
“..hee makubwa..!!, mambo gani tena..??”
Akili yangu sasa ikawa kama imenivurugika huku nikibaki njia panda na nisielewe ni kitu gani hicho ambacho aisha ameambiwa na Jerry. Mawazo yangu yote yakanirudisha mpaka siku niliyoota kuwa nachukuliwa mwanangu na Aisha wakisaidiana na Jerry na kisha nikabakwa na vijana nisioweza kuwatambua..
“..inawezekana ile ndoto ikawa kweli na leo hii ikanitokea ‘live’..?”
Nilijisemea kimoyo moyo huku sura ikinibadilika nakumuangalia mwanangu Adrian pembeni. Hasira kali iliyoamsha misuli pembezoni mwa uso wangu huku ikihamasisha dukuduku kali moyoni. Japo alikuwa hajamalizia kuongea lakini akili yangu ikawa imeshabadilika kwa kiasi kikubwa nakuona huenda nitatekwa tu. kuwa hapa hapanifai hata kidogo tena.
“..ennhee Aisha ikawaje sasa ni mambo gani hayo mawili aliokuwa amekuomba huyo Jerry”..
“..aliniweka wazi kuwa yeye hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba, amesumbuka sana kwa madaktari na mpaka kwa waganga wa kienyeji  lakini imeshindikana. Hivyo akaamua aoe na kuishi na mwanamke ambaye yuko sawa nayeye ambaye hana uwezo wa kuzaa ‘mgumba’. Basi akaoa lakini mtafaruku umekuja kwa wazazi wa pande zote mbili wanataka wajukuu.. kilichofanyika Jerry akaniomba kwanza nimtunzie siri na aibu hii kubwa ambayo amehangaika nayo kwa muda mrefu sana bila ya kuwa na mtoto. Pili akaniomba apandikize mbegu zake kwangu kutokea hospitalini ili nishike mimba nakumzalia.
“..hee.., halafu..?”
“..kama nitashika mimba atakuwa bega kwa bega na mimi mpaka nitakapojifungua. Atahakikisha amenijengea jumba kubwa nakuniwekewa kila kitu ndani nitakachokihitaji. Pia mkewe atamsafirisha nje ya nchi kwa siri siri bila ya ndugu kujua chochote na atakaporudi atakuta nimeshajifungua hivyo atamchukuwa mtoto nakumlea. Tulijaribu mbegu zake karibu mara tano lakini ikashindikana mimi kushika mimba kwa kutumia mbegu za Jerry. Kwa kuwa tayari nilishaingia tamaa ya hela na makazi kama alivyoniahidi Jerry. Nikapanga dili na dokta kisha nikasafiri mpaka Morogoro kwa mpenzi wangu Almeida akanipa ujauzito hivyo nikamsakizia Jerry kuwa tumeshafanikiwa kushika mimba. Jerry alifurahi sana kwa kuwa nilikuwa katika kipindi kigumu. Ilinibidi nisimamishe kwanza mambo yangu ya chuo kwa muda wa miezi tisa huku na ujauzito. Nikatafutiwa mfanyakazi wa ndani ambapo hata hivyo haikuwa ikipita siku bila Jerry kunipigia simu au kuniletea vitu mbalimbali vya kuniliwaza..”
“..kwa hiyo sasa huyo mtoto ukajifungua au ikawaje sasa..?”
“tina..? yani mtoto nilijifungua salama bonge la toto  mzuri kama huyo wa kwako. Hii nyumba na gari unavyoviona ameninunulia Jerry. Na mkewe ni rafiki yangu wa karibu sana na haipiti siku bila kunitembelea ama kunipigia simu na hivi nimeshamaliza chuo kabisa utamuona hapa kila siku..”
Mapigo yangu ya moyo yakaishiwa nguvu na kwa sasa yakawa kama yamepigwa ganzi ama kumwagiwa maji tena yale ya barafu ambayo hutoa kama moshi. Kichwa kilianza kunigonga huku nisielewe nianzie wapi. Sikuwa na hamu tena ya kukaa hapa japo ndio kwanza ilikuwa siku ya kwanza. Tukiwa bado kwenye maongezi na Aisha mara tukasikia sauti ya gari ikipiga honi huko nje. Hatujakaa sawa mara tena Simu ya Aisha ikaita, akapokea..
“..yeahh honey mambooo..!!! Ni wewe karibu namimi ndio kwanza nimemaliza chuo leo vipi upo peke yako ama..?”
“..sikuweza kutambua vizuri kuwa Aisha anaongea na nani zaidi yakuniaga kwa ishara huku akiniacha chumbani nakuelekea sebuleni..”
Mawazo mengi bado yaliendelea kunitawala ndani ya halmashauri ya ubongo wangu. Sikuweza kujitambua Tina mimi. Nilihisi kama ndoto. Nilivaa nguo kwa kutetemeka mithili ya mtu mwenye ukoma au yule anayeumwa malaria kali sana. Midomo yangu ilikuwa ikitetemeka kwa haraka haraka mithili ya maji yanapochemka katika sufuria. Nilibaki nimeduwaa peke yangu huku nikiwa sipati jibu wala ufafanuzi wa hili jambo. Nilichokifanya niliiinuka taaratibu kisha nikamweka mwanangu Adriani vizuri kitandani nakuanza kunyatanyata kuelekea sebuleni huku mwanangu Adrian nikimuacha akiwa amelala fofofo.  Niliendelea kunyata kimya kimya. Sauti za taratibu na za kimahaba kuashiria sebuleni kuna mtu na mume wake ndizo zilikuwa zikinivuta zaidi. Nilipokaribia nilifunua pazia la kuingilia sebuleni kwa utaratibu huku nikifumba jicho langu la upande wa kulia nakuliachia jicho la upande wa kushoto likifanya kazi yake ya kuangaza nakushuhudia tukio zima huku masikio yangu yakiwa sambamba na hilo tukio.
“..Jerry..?? Jerry..? oohh…!! Nooo…!!! Aisha noo..??”
Maskini Tina mie alikuwa ni Jerry katika himaya hii. Na kwasasa alionesha sura ya ukali huku akimuhadithia Aisha tukio zima nililomfanyia pale stendi miezi michache iliyopita. Alikuwa akimuomba sana Aisha msaada wa kunitafuta popote pale nilipo ili ampate mtoto wake. Jerry alikuwa akitoa machozi kama mtoto mdogo vile huku akimbembeleza Aisha wawe kitu kimoja kuhakikisha huyo mtoto anapatikana. Nikiwa bado nashuhudia Jerry akimbembeleza Aisha mara Aisha akainuka pale nakutoka huku akielekea sehemu ambapo nipo..
“..Jerry haiwezekani mwanagu wa damu yangu kabisa eti amchukue Tina anajua tulivyompata..?, embu subiri nakuja sasa hivi..?”
Aisha alionekana kuwa na hasira zaidi kwani aliinuka kwa hasira na kwa shari. Nilichomoka kwa haraka huku nikielekea chumbani kwangu kumuwahi mwanangu Adrian lakini kabla sijafika chumbani Aisha akawa tayari ameshaniona kwa mbali kidogo akaniita kwa sauti ya kupaza na ya ukali..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaa….??????????????”






*** Najua bado unatamani sana kujua kitakachompata Tina, hii sio ndoto ni ukweli kabisa, je unavyodhani ndio utakuwa mwisho wa **Play gal..? nini hatma ya Tina..?


*** kwanini mikosi haimuishi Tina kila kukicha..?


*** utamu ndio kwanza unazidi kunoga, chonde chonde usikubali kusimuliwa **Play gal ittakayofuata kwani ni nzuri zaidi ya hapa.  Jiandae kwa kumshuhudia tena Tina kilichompata ndani ya   ***Play gal – 61



***itaendelea>>>>>>>>>

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home