Saturday, August 25, 2012

CHEKA WEEEEE..>!!!!!!!!!!


Mlevi Mmoja Alibatizwa
akazamishwa majini
Mchungaji akasema
tangu sasa hautaitwa
RAHIMU utaitwa Yohana
Umekua kiumbe kipya.
Mlevi alipofika
Nyumbani akachukua
BIA akaitumbukiza
kwenye ndoo ya maji
akasema kuanzia sasa
hutaitwa TUSKER
utaitwa FANTA alafu
akainywa......!!!!!
...!!!!!.tafakari chukua
hatua...ULEVI
NOMAAAA..






MTALII mmoja kaja BONGO akakutana na interpreter mmoja mswahili anaitwa MKUBYA wakaenda hotelini mambo yakawa hivi:

TOURIST:"Do you have vegetables here?"
MKUBYA:"Mnavyo vijimeza hapa?"

WAITER:"Vijimeza vidogo hatuna."
MKUBYA:"No sir,they dont have."

TOURIST:"Ok,fine do you have hotdogs?"
MKUBYA:"Sawa,je mnao mbwa moto?"

WAITER:"Loh! Bwana we hatupiki mbwa hapa!"
MKUBYA"They dont cook here."

TOURIST:"What type of snacks do you have here?"
MKUBYA:"Aina gani ya nyoka munauza hapa?"

WAITER:"We bwana ee hapa hatupiki aina yeyote ya nyoka mwache akale nyumbani kwao."

MKUBYA:"They dont cook any type of snacks here,maybe you can go back and eat at home."

TOURIST:"Ok,atleast give us cocktail juice."
MKUBYA:"Ok,basi tupatie hata juisi ya mkia wa jogoo."

WAITER:"Pumbavu,hebu tokeni na bangi zenu hapa,tena sasa hivi kabla sijakasirika!!"

MKUBYA:"Lets get out of here i think this man is crazy!!"
~Ne~






Saa mbili asubuhi jamaa bado hajarudi nyumbani kwake toka jana.Mke akakerwa sana,mwishowe akaamua kumpigia simu:

WIFE:"Uko wapi we mwanamume ovyo,muhuni mkubwa usiku mzima humkumbuki mkeo kazi kuzurura tu,mi nimechoka mpuuzi wewe unipe talaka yangu! Tena leo.....uko wapi?"

JAMAA:"Unakumbuka lile duka la sonara? Pale ulipoona ule mkufu wa dhahabu ukaupenda sana?"

WIFE:{akaanza kuwa mpole} "Ndio
mume wangu mpenzi,napakumbuka.Kumbe darling uko nje unatafuta mazuri ili mkeo nipendeze,nisamehe kwa hayo maneno yangu makali.Kwa hivyo ndo uko hapo umeamua kuununua...we nawe unanipenda kweli,asante sana mume wangu,najua umechoka nunua haraka uje unywe chai kabla ya hujaenda ofisini.Mwaaaah♥"

JAMAA:"Hapana sio hivyo nilitaka nikwambie niko kwenye bar karibu na hilo duka....kuna beer za offer nakunywa tokea jana!!"





Shahidi wa tukio la ajali akitoa ushahidi wake mahakamani..na hivi ndivyo ilivyokua:

Mwanasheria: "Ni kweli kwamba uliishuhudia ajali iliyotokea?"

Shahidi: "Ndio niliishuhudia."

Mwanasheria: "Ulikua umbali gani kutoka kwenye tukio la ajali?"

Shahidi: "umbali wa futi 31 na nchi 6 na robo."
Mwanasheria (akidhani atamtia mtegoni shahidi): "Vizuri, Je unaweza kuiambia Mahakama ulijuaje kama umbali huo uliosema ndo wenyewe haswaa?"

Shahidi: "Kwa sababu ajali ilipotokea nilichukua futi ya kupimia nikapima na nilijua some stupid lawyer would ask me that question."





Kulikuwa na jamaa wawili kipofu na kiziwi waliongozana wakawa wanaenda porini walipofika sehemu moja wakaona matunda wakaamua na apande juu ya mti ikabidi apande yule kiziwi alipofika juu ya mti akakanyaga tawi lililooza akadondoka chini bahati mbaya nguo zikabaki kwenye matawi akamwambia yule mwenzie niangalie kama nimepona yule kipofu akaenda akampapasa akamshika kwenye makalio akasema yayayayaa! Yaani meno yote mdomoni hayamo asijue kuwa ameshika makalio.







Jamaa aktika mizunguko yake kafika mahali akajiskia ana kiu akaenda nyumba iliyokuwa jirani na hapo akaomba maji ya kunywa.. Akaja mtoto na kikombe cha maziwa akampa. Jamaa alipomaliza akaomba aongezwe dogo akamletea tena maziwa.. Jamaa ikabidi aulize, '' vipi mbona mnagawa maziwa kwa wingi namna hiyo?'' dogo akamwambia kuwa panya alindumbukia kwenye maziwa ndio maana wote hapa nyumbani wameyakataa.. duh jamaa kusikia vile kwa mshangao akaachia kikombe chini kikavunjika.. yule dogo akapiga kelele eti '' Yalaaaaaaaaa kile kikombe Bibi anachotemea mate kimevunjikaaaaaaa....






Mchaga alipata ajali alipozinduka pale hospitali akauliza "nipo wapi hapa?" Nesi akajibu,"umepata ajali, hapa upo hospitali. Bahati mbaya umekatika mkono." Mgonjwa: Na je saa yangu ipo wapi ya Rolex? Ipo mzee, nesi alijibu. Nesi: Mkeo na watoto wapo hapa kukufariji. Mgonjwa: Yeuwi... Wamefunga duka?






Jamaa walikuwa
wanacheza mpira. Kwa
bahati mbaya mchezaji
mmoja akaanguka na
kuzimia. Refari alikuwa
mzungu lakini wachezaji wote ni waswahili.
Mchezaji mmoja akataka
kumwambia refari
(Mzungu) kuwa huyu
jamaa kazimia. Akafikiria amwambie nini
refarii kwa sababu refari
hajui kiswahili. Akafikiria
kuwa neno "kazi" ni "Job" kwa kizungu, na neno "mia" ni "hundred" kwa kizungu, akasema sasa
nimejua nini nimwambie
refarii, akamwendea
refarii na kumwabia hivi
"Hello refari this man
kajob handred".







Jamaa1 alitulia beach mara
akapita mzungu
akamuuliza "R U RELAX"
jamaa hajui k2 akajibu
"NO" akapita mwingne
akamuuliza vilevile jamaa
akajibu "NO AM
ALEX"....Akaamua kusogea
mbele akamkuta mzungu
ame2lia akamuu "R U
RELAX"mzungu akajibu
"YEAH!" Jamaa akampiga
bonge la bao
akamwambia "ebo!!!
Wananiangaisha mie 2
kumbe we ndo relax
umejificha huku nenda
uko wenzio wanakutafuta.






KUNA DOGO MMOJA WAKIKE ANARUDI NYUMBANI KWAO NA MADAFU MAWILI MKONONI,MAMA YAKE AKAWA ANAMUULIZAWAKINA JUMA NDIO WAMEKUANGULIA MADAFU? MTOTO AKAJIBU HAPANA MAMA WAMEKATAA KABISA NIMEPANDA MWENYEWE KUANGUA .MAMA AKAANZA KUGOMBA WASHENZI SANA HAWA WAKINA JUMA WALITAKA UPANDE TU WAKUCHUNGULIE CHUPI,,,KISCHANA KIKAJIBU ,,NA MIMI NILIJUA TU NDOMAANA NILIIVUA KABLA YAKUPANDA WAMEZODOKA EEE MAMA,,,,,,,,,,MAMA KABAKI NA MSHANGAO WAAJABU.








Mlevi anarudi na rafiki yake mgeni nyumbani kwake na kuanza kumuelekeza hii ni nyumba yangu na lile ni gari langu, wakaingia ndani wanalikuta njemba limelala na mke wa mlevi bila wasiwasi mlevi akaendelea kuelekeza kile ni kitanda changu, yule ni mke wangu na yule aliyelala naye ni MIMI. .




Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home