Thursday, August 16, 2012

**** Play gal - 59 (Revenge)



Ilipoishia…

Aisha aliongea kwenye simu kwa sauti ya ukali na yakikatili kisha ndani ya dakika chache mlango wa gari kwa upande wangu ukafunguliwa. Tochi zilinimulika kisha nikashikwa na watu nisiowafahamu halafu kwenye gari nikamshuhudia Jerry kiingia kisha akambeba yule mtoto na kuondoka zao na Aisha huku wakiniacha nimekumbatiwa na watu nisiowafahamu.
“..mnampeleka wapi mwanangu..??, mrudisheni..??”
Nilitoa makelele ya nguvu lakini haikusaidia chochote zaidi ya ile gari kutokomea huku wale wavulana waliokuwa wamenishika kwa kunikumbatia wakianza kunivua nguo zangu na zao tayari kwa kunibaka kwa zamu…

 Sasa endelea..


Walinigombania huku kila mmoja akinivuta huku na kule. Nilijitahidi japo kutoa sauti za makelele lakini haikusaidia kitu zaidi ya wale vijana kunipiga vibao na kisha kuniburuta mpaka eneo la kichakani kwenye giza totoro. Mwili wangu wote ukawa hauna thamani tena. Hawakuwa watu wazuri hata kidogo kwani walinifanya kwa nguvu na baada ya hapo wakachukuwa majiti nakunisokomeza ambapo walinisababishia maumivu makubwa na makali sana mwilini mwangu na haswa upande wa matiti yangu kwani walikuwa wakiyavuta na kuyafinya kwa kucha zao ndefu  na hata wengine kuyauma kwa kutumia meno. Ndani ya kama nusu saa walikuwa wameshaniharibu sana na pia walikuwa wameshatawanyika kila mmoja. Uwezo wa kusimama sikuwa nao zaidi ya kujiburuta chini chini huku nikitafuta japo barabara kuu ya kuweza kutokea. Tumbo nalo lilianza kuniuma sana tena kule kuuma kwa kuvuta maeneo ya chini ya kitovu.
“..nimekukosea nini eeh Mungu wangu..? Niangalie ninavyoteseka..? Weka japo mikono yako uniangaze na kunipa nguvu eeh  Baba..?”
Nilianza kumlaumu mwenyezi Mungu aliyeniumba nakujiona nimetengwa kabisa katika ulimwengu huu uliojaa mateso. Mikono yangu miwili ndio ilikuwa kama miguu kwa kujisukumia taratibu. Hatimaye baada ya mwendo kidogo nikaona gari kwa mbali linapita. Nilijaribu japo kutoa sauti ya ukali kwa makelele lakini ilishindikana kwani sikuwa na sauti kubwa tena na hata hivyo lile gari lilikuwa katika mwendo kasi hivyo halikuweza hata kuniona wala kusimama. Akili yangu sasa ikawa inamfikiria mwanangu Adrian niliyeporwa na rafiki yangu kipenzi Aisha akishirikiana na Jerry.
“..na lazima niwatafute na kuwaua kabisa..?”
Hasira yangu kwa sasa ikawa imefika kikomo kwani nilijihisi kutokwa na mishipa pembezoni mwa paji la uso wangu.  Nilijikuta nimepata nguvu za ajabu tena zile za ghafla. Niliweza kuinuka na kwa sasa nikawa natembea haraka  haraka mithili ya wanajeshi wakiwa katika mazoezi yao ya kwenda vitani. Haikunichukuwa  mwendo sana mara kwa mbele yangu kidogo nikakutana na dalaldala pamoja na teksi teksi zikiwa zimepaki huku eneo lile kukiwa na watu wakifanya shughuli zao mbali mbali. Hapo hapo halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi haraka nakutambua kuwa pale patakuwa ni kituo cha daladala na pia ni maeneo ya makazi ya watu. Mwili wangu sasa ukaondoka na hofu ya kuwa bado porini. Furaha yote nikaihamishia ndani ya lile eneo huku nikilisogelea kwa tabasamu ya hapa na pale. Nilipofika tu pale kwenye mwanga kila mmoja akaanza kunishangaa. Nilijiangalia mwili wote kisha.
“..Mamaaaaa..!!!!!, Mamaaaaaa…!!!”
Maskini Tina mimi kumbe nilikuwa sijavaa hata nguo. Nilikuwa uchi wa mnyama na mwili wangu kwa sasa ulikuwa umegandia damu damu ambazo zilikuwepo maeneo yote ya kuzunguka mapajani, tumboni mpaka kwenye maziwa yangu. Aibu kubwa niliipata lakini sikuwa na jinsi zaidi ya akili yangu kunituma nirudi kule machakani nilipobakwa nikazichukuwe nguo zangu. Kwa mwendo wa haraka niligeuka nyuma nakuanza kuondoka zangu. Hatua mbili tatu mara uso kwa uso nikakutana na gari.
“..Mamaa nakufaaa..!!”
Mwili wangu wote ulikuwa uvunguni mwa gari lilikokuwa linapita njia na kwasasa lilikaribia kunigonga. Ni breki tu ndizo zilisaidia. Yule aliyekuwa akiendesha gari alishuka huku anaongea maneno kwa ukali. Kadri alivyonisogelea na ile sauti ilivyokuwa ikitikisa ngome ya masikio yangu ndivyo nilivyokuwa nikisisimka nakupata na wasiwasi kama namfahamu. Aliponifikia karibu tu.
“..haa Aisha niwewe…? Kwanini unanifanyia hivi jamani..??, umenitumia vijana wanibake sawa…? Ukaona haitoshi ukanipora na mwanagu Adrian ukampa Jerry kisa pesa Aisha….??. Haya sasa si unataka unigonge..??, nigonge kabisa ili ndoto zako ziwe zimetimia si ndio..?”
Niliongea kwa jazba sana baada yakugundua kuwa kumbe aliyetaka kunigonga alikuwa ni rafiki yangu kipenzi Aisha na kwa muda huu alishuka nakuniongelesha kwa hasira zake. Nikiwa bado nipo uvunguni mwa gari huku Aisha akiniongelesha mara nikasikia sauti ya mtoto wangu akilia ndani ya gari.
“..Aisha mwanagu Adrian yuko wapi nasikia analia..??, nasikia analia.., yuko wapi..?”
Hasira kali nilizoinuka nazo pale chini zilinifanya nimsukume Aisha nakuongoza moja kwa moja mpaka kwenye mlango wa gari lake bila kugeuka nyuma. Nilifungua mlango ule kwa hasira zote nakumshuhudia mwanangu Adrian akiwa anatapika ovyo huku kafungwa fungwa ovyo na makamba shingoni mwake. Nilianza kumfungua haraka haraka lakini kitendo cha kumalizia kumfungua tu zile kamba nikahisi kimya kwa mwanagu Adrian. Nikamtingisha bado kimya. Nikamgusa na kuegemeza kichwa changu kifuani mwake japo nisikie mapigo yake ya moyo napo kimya. Akili yangu moja kwa moja ikanituma kuwa mwanangu Adrian sinaye tena yaani ameshafariki..
“Adrriiiiiiiiiaaaaaaaaaaaaaaaaaaannnnnnn….???????, Adriiiiiiiiiiiiiiaaaaaaaaan…..??”
Bado nilimuinua nakumtingisha tingisha lakini ndio kama nilikuwa najifurahisha na mdori kwani alishafariki muda mrefu.
“..Aisha..?? Aisha…??, Aishaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa..??”
Nilishtuka kutoka usingizini huku jasho likinitiririka mithili ya maji ya chemu chemu yakifuata mkondo wake huku kwikwi kali sana ya hasira na maji kwa ujumla vikinishika vilivyo. Kizunguzungu cha ghafla kilichonishika nilijihisi naona kama ukungu mbeleni mwangu kwani macho yangu yalikuwa yameishiwa nguvu ya kuona vizuri. Nilishusha pumzi nakupikicha macho yangu huku nisiamini kama vile vyote vilivyonitokea kuwa ilikuwa ni ndoto. Eti mpaka rafiki yangu Aisha akanigeuka nakumchukua mwanangu Adrian. Haraka haraka nikageuka pembeni yangu nakumwangalia mwanagu Adrian ambaye alikuwa bado amelala. Nilimuinua nakumbusu kwenye paji lake la uso.
“..inaonekana unampenda sana mwanao Adrian…?”
Aliniongelesha rafiki yangu Aisha ambaye kwa muda huu tulikuwa bado tupo njiani kuelekea nyumbani kwake na alikuwa akiendesha gari. Nilijilaumu sana kuota ndoto ya ajabu kiasi kile lakini haina jinsi kwani ndoto haipangwi. Nilimgeukia rafiki yangu Aisha mara mbili mbili huku nikioneshwa kutetemeka kwa uwoga nakudhani huenda nilichokuwa nakiota kikanitokea muda wowote.
“..ahh..!! itakuwa mandoto tu..!!, kwanza hawezi kunifanyia hivyo rafiki yangu kipenzi Aisha….”
Nilijikuta najifariji kwa kuongea kimoyo moyo huku nikiachia tabasamu kwa kumwangalia Aisha.
“..daah..!!, kumbe hujaacha kulala lala enhh..??”
“..ennhh..!!  shosti wangu kwa jinsi ninavyopenda kulala Tina mimi..? Yani ni kama ugonjwa kwangu toka kipindi kile tupo wote chuoni.., si unakumbuka hata darasani nilikuwa siingii ama nachelewa kisa usingizi..?”
“.. ni kweli.., ila umelala sana, yani tokea tunatokea pale chuoni CBE umelala tu na mwanako wote. Tumepita kwenye mafoleni pale Morocco, Kijitonyama hadi Mwenge kote bado umelala tu Tina..?”
“ndio hivyo..!!, wanasema usingizi mwanaharamu ukikushika. Lakini bado tu hatujafika aisha..?”
“ujue ni vijifoleni tu vya hapa na pale ndivyo vinafanya hivi, lakini isingekuwa hivi..? tungekuwa nyumbani muda mrefu sana.. lakini hatuna muda mrefu tunafika..”
Niliendelea kupiga  stori mbili tatu na rafiki yangu kipenzi Aisha japo bado kale ka uwoga ka ndoto kalikuwa kakinitawala ndani ya halmashauri yangu ya ubongo. Ndani ya dakika kama kumi hivi tulikuwa tunatazamana na geti kubwa  jekundu lililopambwa na nakshi nakshi za silva. Aisha alipiga honi kama mara mbili na punde akatoka kijana aliyekuwa amevaa kofia kuashiria kuwa huenda alikuwa ni mlinzi wa Aisha. Alitufungulia nakuingia mpaka ndani.
“..Tina karibu na jisikie uko nyumbani. Hapa ndipo ninapoishi na mume wangu niliyekwambia kuwa kwa sasa ni mfanyabiashara na wala si mtu wa kukaaa sana hapa bongo kwani huwa anakuja na kuondoka siku hiyo hiyo au anakaa hata siku moja mbili anaondoka zake. Karibu ndani kipenzi changu..”
Aisha alinikaribisha kwa ukarimu sana. Tuliingia mpaka ndani na akanikabidhi chumba kimoja.
“..hiki kitakuwa chumba chako kuanzia sasa Tina. Jisikie uko nyumbani na jisikie upo kwako rafiki yangu kipenzi Tina..”
“..haa..!!, sijui hata nikushukuru vipi mpenzi..!! Ahsante sana na ubarikiwe uendelee kuwa na moyo huo huo Aisha..”
Chumba kilikuwa nikikubwa sana ambapo ndani yake kulikuwa na kila kitu. Kuanzia choo na bafu. Kitanda kikubwa. Nilimvua mwanangu Adrian nguo zake nakumpeleka bafuni ambapo nilimuogesha nakisha nikambadilisha pampasi, baada ya hapo nikaoga na nilipotoka kuoga tu Aisha tayari alikuwa chumbani kwangu kitandani na Adrian ananisubiri nitoke kuoga.
“..Tina nimekuletea nguo hizi hapa, mie huwa zinanibana sana si unajua kunenepa kwangu ovyo tena..!!”
“..Ooh..!!, ahsante Aisha..”
“..ila kuna kitu nahitaji ujue…





*** je unavyodhani ni kitu gani hicho Aisha anachotaka kusema..?

*** Aisha ataishi vizuri na Tina kweli..? na nini hatma ya Tina katika story hii..?

*** stori ndio kwanza kama inaanza upya.. usithubutu uikose wala kusimuliwa inayofuata, ***Play gal 60

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home