Saturday, August 4, 2012

*** Play gal – 56 (Revenge)



Ilipoishia…

“..ama nife mimi Tina..!, au Jerry..! sitamrudisha huyu mtoto kamwe..!!”
Nilijisemea kwa sauti ya chini chini huku nikitokomea mpaka kwenye geti la nje kabisa na nilipofika nje kabisa ndipo kwa mbaali nikasikia tangazo kuwa kuna dada ametoroka na mtoto na amevaa suruali ya jinsi akiwa na mkoba mweupe. Eti akamatwe popote alipo humu ndani ya stendi..
“..It’s too late Jerry..!! (Jerry umeshachelewa..!!)”
Niliongea kwa kujidai huku nikipanda dalaladala yakuelekea Mbagala na nisijue naenda kwa nani na wala itakuwaje huko nieandapo na huyu mtoto..

Sasa endelea…

Ile hali ya woga na kutetemeka ilishaanza kutoweka  ndani ya akili na mwili wangu kwa ujumla.  Na sasa akili yote nilikuwa nimeielekeza ni jinsi gani nitaishi na huyu mtoto huko niendako. Nilijiona mtu tofauti sana kutokana na kuwa na mtoto japo si wakwangu lakini kwa jinsi nilivyokuwa nambembeleza akilia hata akicheka. Nilikuwa nacheka naye kila abiria allikuwa akinishangaa nakuona ni jinsi gani nilivyokuwa na kipenzi na mtoto wangu japo ukweli si mtoto wa kumzaa mimi. Ilinichukuwa kama lisaa mpaka kufika Temeke. Japo daladala ilikuwa inaelekea mbagala lakini kwa upande wangu kutokana na  kuchoka sana mwili na pia mtoto alikuwa kashajisaidia hivyo nilitakiwa nimbadilishe nguo nikaamua kushukia Temeke nakutafuta gesti ya bei nafuu uswahilini.




*******



‘Mji mwema guest house’ ndio gesti niliokuwa nimefikia Tina mimi na huyu mtoto wa Jerry niliomuiba. Kwa sasa alikuwa amelala hivyo nilipoingia tu chumbani nilimvua nguo zote kisha nikaifungasha vizuri ile pampasi yake iliyokuwa imejaa kinyesi pamoja na mkojo nakuiweka katika mfuko wa rambo nakuvitupia kwa pembeni. Nilipomaliza kumsafisha nilichukuwa pampasi ya akiba ambayo ilikuwa katika huu mkoba mkubwa niliouchukuwa kwa mama yake na huyu mtoto.
Usingizi ulikuwa wa shida sana kwangu nadhani hii yote ni kutokana na kuchoka sana mwili na hata akili yangu. Mawazo mengi niliokuwa nayo na mipangilio yangu ya baadaye kuhusu huyu mtoto ni kati ya vitu ambavyo bado vilisumbua sana katika halmashauri ya kichwa changu. Nilifanikiwa kuupata usingizi kwa tabu sana na nilipokuja kushtuka usiku wa manane napo sikuwa na saa wala simu hivyo sikuweza kugundua imetimia muda gani lakini giza bado lilikuwa ni tororo. Mtoto alikuwa anakoroma kuashiria kuwa alikuwa na usingizi sana. Nilitamani japo kupata tena usingizi kwa mara ya pili lakini bado kichwa changu kikaendelea kuwa na mawazo mgando ya kumuwaza Jerry kwa vitendo alivyowahi kunifanyia kipindi cha nyuma.
“..Piga ua.! Lazima nije kumtafuta Jerry na nimuue kabisa kwani adhabu ya kumchukulia huyu mtoto wake haitoshi.. yeye ndio aliofanya mpaka nimepoteza ramani ya maisha yangu kwa ujumla..”
Nilijikuta naropoka mwenyewe kitandani nakufanya mpaka mtoto ashtuke nakuanza kulia. Nilimtoa pale kitandani nakuanza kumbembekleza lakini haikusaidia kitu zaidi ya kuzidisha kulia zaidi. Nilimchukulia japo ile nyonyo yake ya kunyonyea maziwa ambapo ilibakiwa na vimaziwa kidogo alivyokuwa amevihifadhi mama yake kwenye mkoba lakini bado haikusaidia kitu chochote. Machozi yalikuwa mengi sana nakunisisimua mwili mzima kila nilipokuwa nikimwangalia huyu mtoto. Alibadilika mwili nakuwa mwekundu kutokana na kulia kwa muda mrefu. Nilijitahidi kumbembeleza hata kwa kutoa maziwa yangu nakumdanganyishia kama namnyonyesha  ndipo akanyamaza nakuanza kunyonya maziwa yangu ambayo kiukweli hayakuwa yakitoa chochote.
“..Sasa huuuuyu mtoto nimuite jina gani..?”
Nilibaki nimeduwaa mwenyewe huku nikijisikia raha kwa kunyonywa maziwa yasiotoka na kale katoto mpaka akapitiwa tena na usingizi. Nilijiuliza maswali mengi sana juu ya jina la huyu mtoto kwani Jerry mara ya mwisho alimuita Mama yake na huyu mtoto ‘Mama Brayan’ hivyo moja kwa moja huyu mtoto ndio atakuwa ‘Brayan’. Lakini kwa upande wangu inanibidi nimbadilishe jina huyu motto haraka iwezekanavyo.
“..Adrian..!!, Adrian..!! yeees..! nitamwita Adrian tu haina hata ulazima wa kumuita jina la nyumbani kwetu kwani mtoto si damu yangu..?”
Niliongea kimoyomoyo huku nikijitandikia vizuri shuka nakujilaza tena kitandani tayari kwa kuutafuta usingizi kwa mara ya pili.


~ BAADA YA WIKI TATU ~


Mtoto Adrian nilishamzoea na nilishamchukulia kama moja ya mtoto wangu wa kumzaa. Pale gesti wahudumu wote wakajua ni mtoto wangu na hata wakanipa jina la Mama Adrian. Uchangamfu wangu wa kuongea na kila mtu ni kati ya vitu ambavyo viliwavutia wengi. Zile hela ambazo nilizichukuwa kwa Mchungaji James nilipomuua kwa sasa zikawa zimeniishia, si kwa kula tu bali hata kwa matumizi ya huyu Adrian. Ilifika kipindi natumia hadi elfu kumi na tano kwa ajili ya matumizi ya mtoto tu. Ilinibidi kila siku niwe na pampasi tatu hadi nne na kopo zima la maziwa ya ng’ombe kwa ajili ya kumnywesha. Sikutaka kujihusisha na marafiki wa mbali nahii gesti kwani niliamini ndipo kujulikana kwangu mpaka kwa Jerry. Habari za nyumbani kwa Baba na Mama yangu sasa nikawa nimezisahau kabisa. Nilianza maisha ya kujitegemea mimi kama mimi tena bila ya kuwa na msaada wowote huku asililimia mia nikiamini endapo baba au mama yangu akagundua kuwa sipo chuoni muda mrefu ataumia sana. Sasa akili yangu yote nikaielekeza katika kufanya mapenzi na watu tofauti tofauti ili tu nipate chochote cha kuniwezesha kujikimu mimi na huyu Adrian. Kuna kipindi nilikubali hata kuingiliwa kinyume na maumbile ili mradi tu nipate chochote na hata wanaume wengine walikuwa wananiingia hivi hivi bila hata ya kutumia kondomu na hata kunilipa.
Siri kubwa tatu ndizo zilikuwa zimekaa kichwani mwangu kama sheria na kiapo cha  kutokumwambia mtu yeyote mpaka mwisho wa uhai wangu. Siri ya kwanza ni juu ya huyu mtoto si wangu ila wote wanatambua kuwa ni wangu. Siri ya pili ni kuwa hapa nilipo nimejificha na nilishawahi kufanya mauaji hivyo ni wazi natafutwa huko Mwanza na pia natafutwa na Jerry na mkewe juu ya huyu mtoto wao niliotoroka naye. Na siri ya mwisho inayoniumiza sana akili yangu ni juu ya ugonjwa huu wa ukimwi. Ni kweli nimeathirika japokuwa dalili zake sijazipata bado lakini mara ya mwisho niliambiwa hospitali kuwa nimeathirika. Na ndio siri iliyonifanya hata nishindwe kuendelea na masomo kwa kuchanganyikiwa na pia hata niwafiche ndugu, wazazi hata na marafiki zangu wote wanaonifahamu.
“..Binti leo nina buku tano tu..”
“..Twende tu haina shida ila tunatumia kondomu..”
“..aanhaa..!!, kondomu ya nini..?”
“..hheee..!!, we vipi..? basi niongezee ziwe elfu kumi twende bila kondomu..”
Alikuwa ni mzee mzima kabisa ambaye ana uwezo hata wa kunizaa, na kwa muda huu alikuwa meshazoea kuja kufanya mapenzi na mimi kwa kutumia kondomu sasa leo naona kaja kivingine kabisa na anataka twende naye bila kutumia kinga. Tulikubaliana naye nakuelekea mpaka chumbani kwangu nilipopanga ambapo nilimchukuwa Brayani nakumlaza chini kisha nikapanda kitandani nakuvua nguo zangu zote nakubakiwa na shanga tu kiuononi kwa ajili ya kuwadanganyishia wanaume wapenda ngono.
“.. haya nipe changu kabla..?, huna navaa nguo hakuna kufanya chochote..?”
“..hilo tu..! ondoa shaka..!!”
Yule mzee hakuwa mbishi, alichomoa noti ya shilingi elfu kumi nakunipatia. Niliichukuwa nakuiweka kwenye nguo za Adriani pale chini kisha nikamfuata huyu mzee mpaka kitandani. Nilianza kwa kumchezea kifuani kwake. Hakutaka kuchezewa sana kwani haja yake nikufanya tu mapenzi  na mimi hivyo akajiandaa tayari kwa kufanya mapenzi. Akiwa kishavua nguo zote mara tukasikia mlio wa simu yake ikiita..
“.embu naomba simu yangu hapo kwenye suruali..”
Alinituma nimtolee simu yake. Haraka haraka nikainuka na kwenda kumtolea na kisha kumkabidhi.. ile nampa tu simu ikakatika. Akaiangalia namba nakuizima kabisa kisha akanigeukia kwa tabasamu nakuanza kufanya mapenzi na mimi. Nilimuonea huruma sana kwakuwa nimeshaathirika hivyo nilimuona kuwa naye anapoelekea ni huko huko. Kutokana na tamaa zangu za pesa hata sikutaka kumzuia alifanya atakavyo na alipomaliza tu cha kwanza.
“..unataka kuongeza..?”
Nilimwambia kwa sauti ya taratibu na ya kimahaba huku nikimrembulia macho. Yule mzee alitaka tena hivyo akachukuwa suruali yake akaniongeza elfu kumi nyingine napo tukaanza tena kufanya mapenzi kwa mara ya pili. Tukiwa katikati ya mapenzi mara mwanangu Adrian akaanza kulia kwa sauti yake ya juu. Sikutaka kumbembeleza mpaka nimalizane kwanza na huyu mzee. Hivyo tukaendelea tena lakini kwa safari hii mwanangu Adriani ni kama alikuwa amezidisha kulia kwa sauti ya juu. Bado sikutaka kwenda kumbembeleza. Tukiwa tupo katikati ya mahaba mara  tukasikia hodi inapigwa Mlangoni kwangu. Ilipiga kwa nguvu kuashiria kuwa mtu anahasira au anataka kitu cha haraka. Hakukuwa na sauti nyingine yeyote zaidi ya kulia sana kwa mwanangu Adrian na yule mtu kuendelea kupiga hodi kwa nguvu. Nilichokifanya nilimfanyia yule mzee ishara ya kumnyamazisha kwa kutumia kidole changu kukiweka mdomoni, kisha nikamchukua mwanangu Adriani hivyo hivyo akiwa analia nakumtupia uvunguni mwa kitanda na baada ya hapo nikaelekea moja kwa moja mpaka mlangoni tena kwa kujiamini huku nimejifunika khanga nakuufungua mlangu nusu.
“eenhe unasemaje..?”
Uso wangu kwa sasa ukawa umekutana moja kwa moja na Mmama ambaye sura yake si ngeni kabisa machoni mwangu huku akibubujikwa na machozi yalioambatana na kwikwi na nilipomuuliza tu kuwa anasemaje. Pale pale alinisukuma nakuingia mpaka chumbani kwangu kwa nguvu…




*** Unavyodhani huyo Mama nii yupi..? Na Tina atafanyaje..?


*** Nini hatma ya Tina kimaisha..?

*** Usithubutu kusimuliwa story hii ndio kwanza imeanza kunoga kwani mwisho wa hii ya 56 ni mwanzo wa  57..
**Jiandae kujua kilichompata Tina ndani ya Play gal – 57

~~~ Itaendelea~~~

Labels:

1 Comments:

At August 4, 2012 at 3:17 AM , Blogger andrew said...

embu tupia comments zako hapa, unaonaje kitackachotokea hapo? ni mama yupi huyoo??

 

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home