Monday, September 3, 2012

Sifa 10 za kumtambua Mpenzi wa Kweli






Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatizwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha mtoto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto zinazowakabili.
Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo ni hizi zifuatazo.

1.Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.

2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri

4.Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuwa mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa kikwazo cha maisha yako, atakulinda daima.

6. Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7. Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine, hafichi hisia zake mbele za watu, atakutetea na kukufanya wa kwanza.

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9.Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.

Wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema kuna aina nyingi sana za mapenzi miongoni mwa binadamu. Hivyo ni muhimu kufahamu kuwa kupenda kwa mtu mmoja au watu kadhaa hakuwezi kulinganishwa na wengine kwa mazingira na mienendo.

Wakati fulani niliwahi kufanya uchunguzi miongoni mwa wapenzi ambapo nilikuwa nawauliza swali. “Vipi dada/ kaka, huyu ni mpenzi wako?” Wengi kati ya niliowauliza hawakupoteza hata nusu sekunde kujibu ‘NDIYO’.

Lakini watu hao hao nilipowauliza kwa mara nyingine “Unampenda kwa sababu gani?” Majibu ya wengi yalikuwa na sababu ambazo si za msingi na wengine walinyamaza au kuambulia kucheka.

Hebu wakati tunaendelea na mada hii, jiulize wewe mwenyewe ambaye una mke/mume swali kama hilo unampendea nini huyo mpenzi wako? Baada ya hapo sababu zinaweza kuwa ni kama zifuatazo “ Nampenda kwa sababu ni mzuri wa sura, tabia, umbo, na kusema kweli ananivutia” la kama hizo hazitakuwa sababu sina shaka nawe utanyamaza au utacheka.

Hii ina maana kuwa watu wengi ambao tuna wapenzi iwe wake au waume zetu, huenda tuliwapenda au tunawapenda hadi sasa bila kufahamu kwa nini tunawapenda na kitu gani kilitufanya tuwe wapenzi. Maana ikiwa ni uzuri, tabia, mvuto na sababu nyinginezo, basi lazima tufahamu kuwa uhai wa mapenzi yetu ni mdogo.

Inasemwa hivyo kwa sababu watu hubadilika tabia, sura, umbo, mvuto, ufahamu na hivyo kuweka ukomo wa mapenzi kuwa ni baada ya kutokea kwa mabadiliko hayo ambayo ni ya kawaida katika maisha ya mwanadamu, kwani ni wazi kwamba hakuna kinachodumu miongoni mwa hivyo vinavyotajwa na wengi kama sababu za kupendana.

Watalaam wa elimu nafsi na hasa Bw. Robert Stenberg walijitahidi sana kufanyia utafiti wa mapenzi na kuibuka na aina kuu kiasi cha nne ambazo wanazitaja kuwa ni PENZI LA UTIIFU, PENZI LA KUJALIANA, PENZI LA UIGIZAJI NA PENZI TIMILIFU.


Ufafanuzi unaotolewa na wataalamu hawa unaonyesha dhahiri makosa yanayoweza kufanywa na binadamu katika kuchagua au kupata wapenzi. Jambo ambalo limepelekea kuporomoka kwa uhusiano mwingi kati ya wanaume na wanawake. Wanasema penzi kamili linatakiwa kuwa na sifa tatu, ambazo ni tendo la ndoa, ukaribu na kujitolea.

PENZI LA UTIIFU

Penzi la utiifu au kama wengi wanavyolifahamu hujulikana kama ‘penzi la mahaba’. Katika aina hii ya penzi, wanaopendana hujali sana na kuendekeza zaidi miito ya kimwili. Mapenzi ya kiwango cha juu kabisa miongoni mwao hupatikana pale wanaposhiriki tendo la ndoa. Pia wanaopendana hupenda kuwa pamoja au karibu kwa muda mwingi.

Lakini kwa bahati mbaya penzi la aina hii linakosa sifa moja ambayo ni kujitolea. Wapenzi kwenye penzi hili huonekana na pengine hujiona kuwa wanapendana, lakini unapofika wakati ambapo kujitolea kunahitajika, penzi lililoonekana kushamiri hupukutika ghafla.

Kujitolea kunaweza kuwa na maana ya kuumia kwa ajili ya mwingine, kutoyumbishwa na watu wa pembeni na kuwa tayari kulinda penzi hilo kwa gharama yoyote. Kwa mfano ukiona mpenzi wako hayuko tayari kukusaidia unapoumwa, unapokuwa na matatizo, hakuhurumii unapokuwa taabuni ujue kuwa mapenzi yenu ni ya utiifu ambayo uhai wake ni mdogo.

Jambo la kufanya hapa ni kwa wapenzi wenyewe kujitambua na kuchukua hatua za kukamilisha pengo la kujaliana ili kutowapa nafasi wambea na shida za dunia kuyumbisha meli ya penzi ambayo wanasafiria, ikishindikana watu hawa wanashauriwa kutokuwa wepesi wa kuoana kwani uwezekano wa ndoa yao kutodumu ni mkubwa.

PENZI LA KUJALIANA

Penzi la kujaliana ni lile ambalo wanaopendana wanakuwa karibu mara zote na kushiriki mambo mengi pamoja. Wapenzi wa kundi hili huwa na hali ya kujitolea tofauti na penzi la utiifu ambalo tumeliangalia, lakini kasoro yao kubwa huwa kwenye miito ya mwili. Jambo la kufurahisha hapa ni kwamba wapenzi wa kundi hili wako makini kwa kila sehemu na mara nyingi huwa hawakubali kuingiliwa maamuzi ya mapenzi yao.

Lakini linapokuja suala la tando la ndoa hujitokeza kasoro nyingi za kutofikishana kileleni au kutofurahishana na hivyo anguko lao huletwa na muwasho wa mwili ambao huwasukuma wapendanao hao kutoka ndani ya uhusiano wao na kufanya usaliti.

Sasa ili kulifanya penzi la aina hii liwe imara lazima wapenzi waulizane kuhusu kutimiziana haja za mwili wanapokuwa faragha. Kama kuna kasoro kati yao si busara kufichana wanatakiwa kuwaona wataalamu wa mapenzi na kupata ushauri utakaosaidia kuondoa tatizo hilo. Hawa pia wanashauriwa kutooana haraka.

PENZI LA UIGIZAJI

Penzi la aina ya tatu linalotajwa na watafiti ni lile lijulikanalo kama penzi la Uigizaji. Hili ni lile penzi ambalo wanaopendana hukutana asubuhi na ikifika jioni tayari ni wapenzi kamili, ambapo hugandamana kama ruba, utadhani waigizaji wako kwenye matayarisho ya filamu. Ukiwatazama wanakuwa kama vichaa na msukumo wao wa kutimiza hisia za mwili huwa ni mkubwa kiasi cha kufikia kufanya mapenzi hata barabarani au kwenye sehemu za wazi.

Wapenzi wa aina hii huchukua muda mfupi sana kutangaziana mambo ya ndoa na pengine kuoana bila kufahamiana zaidi kitabia. Wanajuana asubuhi na jioni mwanamke/mwanaume keshahamia kwa mwenzake na maisha yanaanza, hapo hakuna ushauri wala muongozo wa watu wengine.

Tatizo kubwa ambalo hujitokeza katika penzi la aina hii ni wapenzi kuchokana mapema na hamu ya kufanya tendo la ndoa kupotea. “Yaani nikiwa na mume wangu sijisikii kabisa kufanya naye mapenzi, lakini kwa wengine nakuwa na hamu sana” hizi ni kauli za wapenzi wa penzi la kisinema sinema.

Mbali na hilo wapenzi wa aina hii ni rahisi kuporwa na kuanzisha uhusiano mpya, hivyo inashauriwa kuwa kwa wale ambao wanaona kuwa wako kwenye kundi hili, wajitahidi kujizuia na kupeana nafasi za kujuana zaidi kupitia ushauri wa watu wengine. Si vema kushiriki tendo la ndoa kila mara kwa staili na sehemu zile zile na pia haifai kukurupuka kuoana bila kuchunguzana tabia, ndoa za hivi hazidumu.


PENZI TIMILIFU

Aina ya mwisho ya penzi kama inavyoelezwa na mtaalamu Sternberq ni ile ya penzi timilifu. Aina hii ya mapenzi inakuwa na sifa zote tatu, yaani TENDO LA NDOA. Kwamba wapendanao huwa hawana kasoro katika eneo hili, unapofika muda wa kupeana raha hufikishana mahali pa juu. UKARIBU kwamba muda wote huwa karibu na kila mmoja hakai na kiu ya kutokumuona mwenzake kiasi cha kupoteza hisia na kushawishika kufanya usaliti.

Sifa ya mwisho ni KUJITOLEA. Ni mahodari kusaidiana, kufarijiana na hawako tayari kupokea mambo kutoka pembeni yanayohusu uhusiano wao, hivyo huwa si rahisi kwao kuyumba kwa sababu za umbea. Kumbuka katika penzi hili tendo la ndoa huwa si sehemu muhimu sana kwa wapenzi, yaani kwao penzi ni rohoni zaidi kuliko mwilini hata wakikaa muda wa miezi mitano bila kufanya tendo la ndoa upendo wao haupungui.

Hata hivyo, penzi la aina hii kwa mujibu wa wataalamu ni vigumu kupatikana na ni vigumu pia kulilinda, lakini linatajwa kuwa ni aina ya penzi bora ambalo ni muafaka kwa maisha ya baadaye ya ndoa kwa wanaopendana. Watu wengi kwa kutotambua aina hii ya mapenzi wamejikuta wakiliharibu kwa kufikiri tu kwamba wapenzi wao wamefika na hivyo kufanya makusudi ya kuharibu misingi ya penzi.

“Nimeshamshika atakwenda wapi, nikikohoa tu anaitika” Kauli kama hizi ni hatari sana katika penzi hili, hivyo inashauriwa ukiona unapendwa na mpenzi wako katika aina hii ya penzi ni vema ukawa macho ili kutolivunja kwa uzembe wako na kudhani unababaikiwa kumbe unapendwa kwa dhati.

Labels: ,

Friday, August 31, 2012

Mambo 10 yanayozuia mafaniko ya kimasomo



UMASIKINI

Umasikini ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya wanafunzi kimasomo, lakini tunashauri kwamba kila mwanafunzi anayetoka katika familia masikini ajitambue na awe tayari kuishi sawa na kipato cha familia yake wakati akitafuta elimu.

Ni muhimu kwake kubana matumizi na asiwe mtu wa kujihukumu kwa kukosa hili na lile, awe mvumilivu na mwenye kuomba msaada kila sehemu anayoona hawezi kuivuka kwa nguvu zake. Uaminifu, bidii na utii unaweza kumsaidia kuvuka kikwazo hiki.

Kuhusu suala ya kufukuzwa shule kwa kukosa ada ni vema kwa mwanafunzi mwenye kipato kidogo akawasiliana na mwalimu wake au viongozi wa serikali ili wamsaidie kutatua tatizo. Haifai kujifungia chumbani na kuanza kulia au kuamua kuacha shule kwa kukosa mahitaji. Mambo yote yanawezekana kinachotakiwa ni nia, mipango na uvumilivu.


MAPENZI

Kama kuna mtu hafahamu nini maana ya mapenzi basi kuanzia leo ajue kuwa mapenzi ni ulevi kama vilevi vingine. Mtu anayependa hulewa na kujikuta anaharibu ufahamu wake kama mtu aliyelewa pombe.

Walevi wa mapenzi huweza kufanya mapenzi hata barabarani sehemu ya wazi, huku akili zao zikiwapa taarifa kwamba watu hawawaoni, mambo ya aina hii hufanywa pia na walevi wa pombe.

Lakini ulevi wa mapenzi una nguvu kubwa ya kuiteka akili na kumtia mtu mshawasho kiasi cha kuacha kazi muhimu na kukimbilia kufanya ngono.

Hivyo, mwanafunzi ambaye anataka mafanikio ya kimasomo lazima aweke kando masuala ya mapenzi kwa lengo la kutoitwika akili mzigo ambao kwa umri wa wanafunzi wengi hasa wa kike ambao ni waitikiaji wa kauli za wavulana ni vigumu kwao kuhimili.

Licha ya baadhi ya watalaamu wa masuala ya afya kubainisha faida za kufanya mapenzi kwa afya ya mwili, bado uchunguzi unaonyesha kuwa wanafunzi wengi ambao wengi wao huwa katika umri mdogo hushindwa kuzuia hisia za mapenzi na kujikuta wanakuwa watumwa wa ngono.

Mapenzi kwa mwanafunzi yana hasara za aina mbili. Kwanza, mapenzi yanapokuwa moto huteka hisia na kumfanya msomi atumie muda mwingi kuwaza juu ya mahaba na hivyo kuufanya ubongo uone kuwa mapenzi ni kitu muhimu na hivyo kujituma kuhifadhi mambo ya mapenzi kuliko masomo.

Jambo la pili ni machungu ya mapenzi hasa yanapokuwepo mafarakano, mfano kuachwa, kusalitiwa, kuudhiwa, kugombana na migogoro yote ya kimapenzi huleta msongo wa mawazo na kumfanya mwanafunzi asiweze kusoma kwa kiwango stahili. Hivyo, inashauriwa kuwa mwanafunzi asijihusishe kabisa na mapenzi.

MIGOGORO YA KIFAMILIA

Kizuizi kingine cha kufanikiwa kimasomo kwa mwanafunzi ni kuwepo katika familia zenye migogoro. Baba na mama hawaelewani, ndugu wanagombania mali na kadhalika. Lakini inashauriwa kuwa mwanafunzi anayetoka katika familia za aina hii hatakiwi kujiingiza katika misuguano ya kifamilia.

Anachotakiwa yeye ni kuwaza juu ya masomo na kutupilia mbali mawazo yote yanayochipuka kuisumbua akili kuhusu mambo makubwa ya kiukoo. Kimsingi ufahamu wa mtoto hasa wa madarasa ya chini ni mdogo, hivyo hawezi kutatua mambo ya wazazi na akijaribu atakuwa anajisumbua na kujiweka katika matatizo makubwa zaidi.

Jambo muhimu kwake katika ngazi ya maisha yake ya shule ni kusoma na kama atakuwa na kitu cha kulilia ni mahitaji ya shule tu, na akiona migogoro hiyo inaathiri masomo yake, labda ada hazilipwi anachotakiwa kufanya ni kuwaeleza wazazi na ndugu wamsaidie kuhusu haki yake ya kupewa elimu na akishindwa katika ngazi hiyo awasiliane na viongozi wa serikali kwa ngazi yake ili wamsaidie.

KUFIWA NA WAZAZI/WALEZI

Uchunguzi unaonesha kuwa watoto wengi hushuka kimasomo baada ya wazazi au walezi wao kufariki. Hapa kuna mambo mawili, kwanza ni huzuni na pili kukosa upendo toka kwa walezi wao wapya.

Kuhusu huzuni mwanafunzi aliyefiwa na wazazi anashauriwa kuacha kabisa kuishi na wazazi wake waliokufa kwenye akili, haitakiwi muda wote kuwaza jinsi wazazi walivyokuwa wakimfanyia mema katika maisha. Wanasaikolojia wanasema hakuna jambo baya la asili isipokuwa mawazo ya mtu mwenyewe.

Ieleweke kuwa jinsi mtu anavyowaza ndivyo anavyojiumiza, huku ukweli ukibaki kuwa hawezi kuwarudisha wazazi wake duniani. Hivyo basi kila wakati mwanafunzi ambaye ni yatima anapoingiwa na mawazo ya kuwakumbuka wazazi anatakiwa kuyaacha kwa kuzungumza na wenzake, kucheza au kutazama sinema za kufurahisha. Si busara kutazama picha za wazazi enzi za uhai wao na kupendelea kuwazungumzia kila mara.

MALEZI YA BUGHUDHA

Baadhi ya watoto ambao wanalelewa na ndugu au walezi ambao si wazazi hukumbwa na kadhia ya kubughudhiwa kwa matusi na maneno ya masimango, kupangiwa kazi ngumu na kunyimwa muda wa kujisomea. Usumbufu huu wa kimalenzi upo hata kwa baadhi ya wazazi ambao wanakasumba za kubagua watoto.

Lakini ushauri unaotolewa hapa ni kwamba maisha siku zote hayana njia ya mkato na watafiti wa masuala ya maisha wanasema misukosuko ya kimaisha ina faida kwa watu wenye uelewa. Wakomonisti wanasema huwezi kutambua uwezo wa nahodha kwenye bahari iliyotulia bali kwenye dhoruba kali.

Ni wazi kuwa mwanafunzi anayesumbuliwa kwa bughudha ana nafasi kubwa ya kushinda masomo kama atazichukua kadhia hizo kama changamoto za kumfanya asilale na kujitambua kuwa yuko kwenye bahari chafu isiyo salama.

Ukiwa kwenye familia za aina hii, soma kwa bidii, usijihukumu sana, jishushe na uwe tayari kutumia unachopewa bila kunung’unika, usijibu mapigo kwa ugomvi au kufokeana na wakubwa wanao kulea. Uwe tayari kutumika kama mtumwa ili baadaye uishi kama mfalme. Ila kama mambo yatazidi pendelea kushauriana na wazee wa ukoo au majirani ili wakutanue mawazo.

STAREHE

Maisha ya shule yanakata nidhamu ya matumizi ya pesa, muda na sheria za shule. Mwanafunzi hawezi kufanikiwa kimasomo kama ataendekeza mambo ta starehe, mfano kwenda disko, kukesha baa na kushiriki mapenzi na wanawake/wanaume kwenye majumba ya anasa.

Haishauriwi mwanafunzi kuwa mtu wa starehe kwani ni rahisi sana kwake kupata matatizo ambayo yanaweza kumharibia masomo yake, mfano kupigwa na kuumizwa, kukamatwa na polisi na kuhusishwa na matukio ya uhalifu na hata kukosa muda wa kuupumzisha mwili na akili.

UFUNDISHAJI DUNI

Walimu wasiokuwa na sifa za kufundisha ni tatizo kwa mafanikio ya mwanafunzi kimasomo, lakini wakati huo huo uhaba wa walimu nao huchangia kushusha kiwango cha kufaulu. Inashauriwa kuwa wanafunzi ambao hawafundishwi vizuri wamuone mwalimu wao wa taaluma na kumueleza tatizo lao ili ufumbuzi upatikane.

Lakini wakati huo huo ni sahihi kuwasiliana na wazazi/walezi na kuwataarifu uhaba wa walimu kwenye shule yako na kuwataka wakusaidie. Inaposhindikana kwa ngazi ya familia ni vema viongozi wa kitaifa wakajulishwa na hatua za kuhama shule zinaweza kufikiwa endapo kikwazo hiki kitakosa ufumbuzi.

UKOSEFU WA VIFAA

Shule nyingi zimekuwa hazina vifaa vya kutosha, hili nalo ni tatizo kubwa na dawa yake ni kwa wazazi wanaojiweza kuhakikisha kuwa wanawanunulia watoto wao vifaa binafsi vya kujisomea. Wakati huo huo ni wajibu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali kuwa na utamaduni wa kubadilisha vitendea kazi ili kupata unafuu wa tatizo hili.


KUHAMISHWA SHULE

Mwanafunzi anapohamishwa shule anaweza kuathirika kisaikolojia, lakini kama imebidi ni vema akatumia vidokezo nilivyoeleza huko nyuma katika kupata uenyeji na kuzoea mazingira mapya.

Haipaswi kuhuzunikia marafiki na walimu alioachana nao na kusahau kuwa yeye anajukumu la kusoma kwa bidii na kupata matokeo mazuri.

UDHALILI

Kuna wanafunzi ambao wanashindwa kufanikiwa kimasomo kwa sababu wanajiona wao ni duni mbele ya wenzao katika mavazi, uwezo wa kifedha na kadhalika. Kwao linakuwa ni jambo ngumu kujieleza mbele ya wenzao na muda wote hujawa na aibu na hali ya kutojiamini.

Kasoro hii ni kubwa na huwakwamisha wengi katika kupata uelewa wa mambo. Ni wajibu wa mwanafunzi kujiamini na kutupilia mbali aibu na kueleza hisia na kile anachofahamu mbele ya mwalimu na wanafunzi wenzake bila kujali kama atakosea au atachekwa. Mwanafunzi anatakiwa kuwa na mazoea ya kubadilishana mawazo na wengine na kuacha kujitenga.

Tabia hii si nzuri, mwanafunzi ambaye anataka kuwa na kumbukumbu juu ya yale aliyojifunza lazima awe tayari kushirikiana na wenzake katika kusoma, kujadiliana na kusaidia.

Labels: ,

Monday, August 27, 2012

VITU VINAVYOWAHARIBIA WANAWAKE KIMAPENZI


vKUNA msemo kuwa: “Wanawake, mwalimu wao ni kipofu.” Mimi siuamini kwa maana umekaa kiukandamizaji zaidi. Haujengi heshima kwa mtu wa jinsi ya kike tangu analizaliwa mpaka anapoingia kaburini. Binafsi naamini wapo wenye uelewa mkubwa lakini wanashambuliwa na mapokeo ya samaki mmoja akioza.

Ni msemo ambao ukiingia kwenye vichwa vya watu unaweza kuwafanya wanaume wawadharau hata mama zao. Mama anatoa mafundisho lakini kijana anasikiliza, linaingilia sikio la kwanza na kutokea la pili. Kichwani anajiongeza: “Aah, hawa si mwalimu wao kipofu?”

Msemo huo unamaanisha kuwa wanawake huwa hawajui waendako. Kwamba njia ya kupita walifundishwa na mwalimu mwenye ulemavu wa macho. Siupendi kwa sababu siyo tu hauna ladha nzuri kwa mwanamke bali pia kwa mtu mwenye ulemavu husika. Unadhalilisha kupita kiasi.

Tangu nikiwa na umri mdogo, nilipenda sana kusikiliza busara za watu walionizidi umri. Niliamini wananijenga na kweli walifanya hivyo. Mtazamo huo, ulinifanya nijue mengi nikiwa na umri mdogo. Hata haya ninayoandika na kushauri, yanatokana na elimu niliyopata kwenye kada tofauti.

Wakati huo sijui ndani ya mwanamke kuna nini, mtu mmoja aliniambia: “Mdogo wangu Luqman, napenda unavyopenda kukaa na sisi wakubwa. Unaweza kuwa na busara katika maisha yako lakini usipokuwa mwangalifu, mwanamke anaweza kukufanya uonekane mwendawazimu mtaani.

“Siku ukiwa na mwanamke, jaribu sana kuwa mwangalifu. Unaweza kumpa kila atakacho lakini mwisho akakuuguza uendawazimu. Ukatembea barabarani unazungumza peke yako kama kichaa au ukiwa nyumbani ukashinda unabwabwaja maneno yasiyoeleweka mpaka majirani wakakuona mwendawazimu.

“Mkeo anaweza kutoka nyumbani anakwenda kumtembelea shangazi yake, kwa kumthamini na kwa sababu huna gari, ukampa fedha ya kukodi teksi. Akitoka njiani, anakutana na dereva teksi anampa lifti. Huwezi kuamini, huyo aliyempa lifti ndiye atamuona bora, mwenye roho nzuri kuliko wewe uliyempa fedha ya kuchukua teksi.

“Matokeo yake ni kwamba akishamuona ni mkarimu sana, anakuwa mnyenyekevu hata kwenye maeneo mengine. Mwisho wanakuwa wapenzi. Hiyo ndiyo tabia ya mwanamke, atasahau mema yako, hatajali watoto mnaolea.” Huyo mtu aliyeniambia maneno hayo anaitwa Jaffari, ni mtu mzima hivi sasa. Enzi hizo nilikuwa nasoma sekondari Mwanza.

Ukweli upo wapi? Ninachoweza kueleza ni kwamba wapo wanawake waungwana mno hapa duniani. Wanadumisha mapenzi ya dhati bila kusaliti licha ya kukumbana na vishawishi kemkem. Wanajua thamani ya wapenzi wao pamoja na changamoto zinazoweza kuwakabili katika maisha.

Hata hivyo, kuna aina ya wanawake ambao Jaffari alikutana nao ndiyo maana akasema hivyo. Isingekuwa rahisi kutoa maneno hayo pasipo kuona kitu. Inawezekana alitendwa na mkewe au alishuhudia kitu kwa rafiki yake, hivyo kumpa tafsiri aliyojijengea kuhusu wanawake.

Tukishika moja kuwa kuna kitu alijionea, basi ni vema kuwazungumzia wanawake ambao walimfanya akawa na mtazamo huo. Hao ndiyo wanaowaharibia wengine mpaka wanakosa thamani. Mtu anatendwa na mkewe lakini lawama anazielekeza kwa wanawake wote kwamba eti ndivyo walivyo!
Jambo ambalo mtu hapendi afanyiwe, basi asianze kumfanyia mwenzake.
Heshima, woga na ‘breki’ katika kauli, vinapaswa kuzingatiwa. Kusaliti maana yake umekosa woga, heshima na busara ya kimapenzi na maisha kwa jumla.
Hekima ni ipi? Kuendelea kuwa na mwenzi ambaye hana heshima juu yako, hakuhofii kwa chochote, wala busara ya maisha haimuongozi kutenda yaliyo mema kwa ajili ya ustawi wa familia yenu. Bila shaka, hekima inafaa kukuongoza kuchukua uamuzi kwa ajili ya furaha na amani ya kudumu baadaye.
Nitoe hoja kuwa hata wanaume wapo wenye matatizo mtindo mmoja, kwa hiyo na wanawake wapo wenye hulka tofauti.
Kama huyo wako ni pasua kichwa, basi wapo waliojaliwa utulivu, heshima, hekima na maarifa ya kudumisha uhusiano. Ikiwa huyo anakunyima furaha, angalia kama unaweza kujivua gamba, kwani wapo wanawake wema.
Mungu hajaumba mtu akamfanya kuwa mbaya kwa asilimia 100, Shetani ndiye anayeharibu vichwa vya watu na kuwafanya wawe na akili zisizofaa. Hata katika jamii ya Wasamaria, alipatikana mmoja aliye mwema ndiyo maana akaitwa Msamaria mwema.
Hivyo basi, wasisemwe vibaya wanawake wote kwa ajili ya makosa ya wachache.
Hata hivyo, hao wachache wanapaswa kubadilika ili wawape heshima wenzao.
Tamaa haifai kwa namna yoyote.
Binafsi nawaheshimu wanawake kwa maana ndiyo waliotufanya tustarehe kwenye matumbo yao kwa miezi tisa, wanawezesha tuitwe akina baba na kadhalika.
Mambo hayo makuu, hayapingiki ndani ya kila mwanaume isipokuwa Adam.
Pamoja na hivyo, zipo dhana nyingine nyingi ambazo zinafanya wanawake wasemwe vibaya. Twende kwa mifano.
Hivi karibuni, niliitwa nimshauri kijana mmoja ambaye kwa hakika alikuwa amechanganyikiwa kabisa.
Alichanganywa na mapenzi.
Mwanamke ambaye aliamini ndiye wa maisha yake, alimuacha katika mazingira ambayo hakuyategemea.
Alikuwa anamhudumia kwa kila kitu lakini akapigwa kibuti kwa SMS.
Kijana huyo anaitwa Mully, akiwa kazini kwake, akaona SMS iliyotoka kwa mtu ‘aliyemsevu’ kwa jina la My Dream.
Kama ujuavyo tena mapenzi, kijana akafungua haraka, akitegemea atapata maneno matamu kutoka kwa mwenzi wake lakini alichokutana nacho ni hiki: “Kuanzia leo, mimi na wewe basi.
Nimepata mchumba nataka kuolewa.”
Mully aliposoma maneno hayo akapagawa, akaamua kupiga simu ya mpenzi wake lakini hakupokea.
Akaamua kumuuliza kwa SMS: “Baby upo serious au unatania?” Haikupita hata dakika moja, majibu yakarudi: “Nipo serious kabisa, tena kuanzia leo usiniite baby na usinijue kwa lolote.”
Meseji hiyo ikamchanganya akili kijana, akaondoka kazini kwake bila hata kuwaaga wenzake.
Yule mpenzi wake anaitwa Janette, ni mtumishi wa ndani kwenye nyumba ya ofisa wa benki Masaki, Dar. Kijana akaondoka kazini kwake Mwenge hadi kazini kwa mkewe. Akili siyo zake.
Itaendelea wiki ijayo

Tunaendelea kuchambua kuhusu dhana ambazo zinawaharibia wanawake kimapenzi. Katika kuhakikisha somo linaeleweka sawia, mwishoni mwa makala ya wiki iliyopita, nilieleza mfano huu:
Hivi karibuni, niliitwa nimshauri kijana mmoja ambaye kwa hakika alikuwa amechanganyikiwa kabisa.
Alichanganywa na mapenzi. Mwanamke ambaye aliamini ndiye wa maisha yake, alimuacha katika mazingira ambayo hakuyategemea. Alikuwa anamhudumia kwa kila kitu lakini akapigwa kibuti kwa SMS.
Kijana huyo anaitwa Mully, akiwa kazini kwake, akaona SMS iliyotoka kwa mtu ‘aliyemsevu’ kwa jina la My Dream. Kama ujuavyo tena mapenzi, kijana akafungua haraka, akitegemea atapata maneno matamu kutoka kwa mwenzi wake lakini alichokutana nacho ni hiki: “Kuanzia leo, mimi na wewe basi. Nimepata mchumba nataka kuolewa.”
Mully aliposoma maneno hayo akapagawa, akaamua kupiga simu ya mpenzi wake lakini hakupokea. Akaamua kumuuliza kwa SMS: “Baby upo serious au unatania?” Haikupita hata dakika moja, majibu yakarudi: “Nipo serious kabisa, tena kuanzia leo usiniite baby na usinijue kwa lolote.”
Meseji hiyo ikamchanganya akili kijana, akaondoka kazini kwake bila hata kuwaaga wenzake. Yule mpenzi wake anaitwa Janette, ni mtumishi wa ndani kwenye nyumba ya ofisa wa benki Masaki, Dar. Kijana akaondoka kazini kwake Mwenge hadi kazini kwa mkewe. Akili siyo zake.
Alipofika, akagonga geti halikufunguliwa, kwa hiyo akapanga matofali getini akakaa. Baadaye Janette akatoka, alikuwa anakwenda dukani, akakutana uso kwa uso na Mully. Yakaanza maneno, baby nimekukosea nini? … sikutaki… baby niambie kosa langu… nimesema sikutaki...
Mtoto wa kike akaona ubishi unampotezea muda, akaingia ndani, akatoka nje na beseni la maji machafu, akamwagia Mully. Kijana wa watu akaloa chapachapa. Janette akarudi ndani, akapiga simu kwa bosi wake, punde polisi wakafika na kumzoa, eti ni mwizi.
Kaka yake Mully akaenda kumuwekea dhamana Oysterbay Polisi. Kuanzia hapo kijana akawa chini, akawa anazungumza hovyo, kazi akawa hafanyi. Kijana akasema: “Mbona mimi ningemuoa tu, sina shida.” Kijana akawa hali, haogi, kazi hafanyi. Akili zikamruka.
Nilijitahidi kumpa ushauri unaofaa kwa vipindi vitatu ndani ya siku tatu mfululizo, baada ya kuona anapata nafuu, nilishauri apelekwe eneo ambalo atabadili mazingira. Alipelekwa nyumbani kwao Singida. Wiki iliyopita, alirudi Dar akiwa mpya kabisa. Anatazama mbele na hamfikirii tena yule mwanamke.
Hata kazi anaendelea vizuri. Machungu ya kuachwa na Janette yamebaki historia. Vema amekaa sawa lakini kitu ambacho kipo wazi ni kuwa Mully alimpenda sana mpenzi wake na aliamini ndiye mwanamke wa maisha. Hali hiyo ndiyo ilimfanya ashindwe kupokea matokeo ya kuachwa.
Alishawekeza mambo mengi kwa Janette hususan rasilimali. Mully aliniambia kuwa kwa siku alikuwa anampa Janette kuanzia shilingi 15,000 mpaka 20,000. Alikuwa anamnunulia mavazi ya kisasa, kiasi kwamba ukimuona, usingeweza kudhani ni mfanyakazi wa ndani.
Baadaye ikaja kubainika kuwa kumbe Janette alipata kiburi cha kuachana na Mully kwa sababu ya bosi wake. Kwamba yule ofisa wa benki baada ya kumuona mfanyakazi wake anameremeta, akaamua kujiweka, binti naye badala ya kufikiria kuwa ni mume wa mtu akakubali.
Wameendelea kuwa na uhusiano lakini za mwizi ni 40, mke akashtukia kuwa anaibiwa mumewe ndani ya nyumba yake. Akamtimua kazi Janette na kipigo juu. Yule jamaa wala hakumtetea ndiyo kwanza akashiriki kusaidia kumtimua. Binti aende wapi? Kazini ameshaharibu, kwa Mully nako alishalikoroga.

Labels: ,

AINA 4 ZA MAPENZI



Wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema kuna aina nyingi sana za mapenzi miongoni mwa binadamu. Hivyo ni muhimu kufahamu kuwa kupenda kwa mtu mmoja au watu kadhaa hakuwezi kulinganishwa na wengine kwa mazingira na mienendo.

Wakati fulani niliwahi kufanya uchunguzi miongoni mwa wapenzi ambapo nilikuwa nawauliza swali. “Vipi dada/ kaka, huyu ni mpenzi wako?” Wengi kati ya niliowauliza hawakupoteza hata nusu sekunde kujibu ‘NDIYO’.

Lakini watu hao hao nilipowauliza kwa mara nyingine “Unampenda kwa sababu gani?” Majibu ya wengi yalikuwa na sababu ambazo si za msingi na wengine walinyamaza au kuambulia kucheka.

Hebu wakati tunaendelea na mada hii, jiulize wewe mwenyewe ambaye una mke/mume swali kama hilo unampendea nini huyo mpenzi wako? Baada ya hapo sababu zinaweza kuwa ni kama zifuatazo “ Nampenda kwa sababu ni mzuri wa sura, tabia, umbo, na kusema kweli ananivutia” la kama hizo hazitakuwa sababu sina shaka nawe utanyamaza au utacheka.

Hii ina maana kuwa watu wengi ambao tuna wapenzi iwe wake au waume zetu, huenda tuliwapenda au tunawapenda hadi sasa bila kufahamu kwa nini tunawapenda na kitu gani kilitufanya tuwe wapenzi. Maana ikiwa ni uzuri, tabia, mvuto na sababu nyinginezo, basi lazima tufahamu kuwa uhai wa mapenzi yetu ni mdogo.

Inasemwa hivyo kwa sababu watu hubadilika tabia, sura, umbo, mvuto, ufahamu na hivyo kuweka ukomo wa mapenzi kuwa ni baada ya kutokea kwa mabadiliko hayo ambayo ni ya kawaida katika maisha ya mwanadamu, kwani ni wazi kwamba hakuna kinachodumu miongoni mwa hivyo vinavyotajwa na wengi kama sababu za kupendana.

Watalaam wa elimu nafsi na hasa Bw. Robert Stenberg walijitahidi sana kufanyia utafiti wa mapenzi na kuibuka na aina kuu kiasi cha nne ambazo wanazitaja kuwa ni PENZI LA UTIIFU, PENZI LA KUJALIANA, PENZI LA UIGIZAJI NA PENZI TIMILIFU.


Ufafanuzi unaotolewa na wataalamu hawa unaonyesha dhahiri makosa yanayoweza kufanywa na binadamu katika kuchagua au kupata wapenzi. Jambo ambalo limepelekea kuporomoka kwa uhusiano mwingi kati ya wanaume na wanawake. Wanasema penzi kamili linatakiwa kuwa na sifa tatu, ambazo ni tendo la ndoa, ukaribu na kujitolea.

PENZI LA UTIIFU

Penzi la utiifu au kama wengi wanavyolifahamu hujulikana kama ‘penzi la mahaba’. Katika aina hii ya penzi, wanaopendana hujali sana na kuendekeza zaidi miito ya kimwili. Mapenzi ya kiwango cha juu kabisa miongoni mwao hupatikana pale wanaposhiriki tendo la ndoa. Pia wanaopendana hupenda kuwa pamoja au karibu kwa muda mwingi.

Lakini kwa bahati mbaya penzi la aina hii linakosa sifa moja ambayo ni kujitolea. Wapenzi kwenye penzi hili huonekana na pengine hujiona kuwa wanapendana, lakini unapofika wakati ambapo kujitolea kunahitajika, penzi lililoonekana kushamiri hupukutika ghafla.

Kujitolea kunaweza kuwa na maana ya kuumia kwa ajili ya mwingine, kutoyumbishwa na watu wa pembeni na kuwa tayari kulinda penzi hilo kwa gharama yoyote. Kwa mfano ukiona mpenzi wako hayuko tayari kukusaidia unapoumwa, unapokuwa na matatizo, hakuhurumii unapokuwa taabuni ujue kuwa mapenzi yenu ni ya utiifu ambayo uhai wake ni mdogo.

Jambo la kufanya hapa ni kwa wapenzi wenyewe kujitambua na kuchukua hatua za kukamilisha pengo la kujaliana ili kutowapa nafasi wambea na shida za dunia kuyumbisha meli ya penzi ambayo wanasafiria, ikishindikana watu hawa wanashauriwa kutokuwa wepesi wa kuoana kwani uwezekano wa ndoa yao kutodumu ni mkubwa.

PENZI LA KUJALIANA

Penzi la kujaliana ni lile ambalo wanaopendana wanakuwa karibu mara zote na kushiriki mambo mengi pamoja. Wapenzi wa kundi hili huwa na hali ya kujitolea tofauti na penzi la utiifu ambalo tumeliangalia, lakini kasoro yao kubwa huwa kwenye miito ya mwili. Jambo la kufurahisha hapa ni kwamba wapenzi wa kundi hili wako makini kwa kila sehemu na mara nyingi huwa hawakubali kuingiliwa maamuzi ya mapenzi yao.

Lakini linapokuja suala la tando la ndoa hujitokeza kasoro nyingi za kutofikishana kileleni au kutofurahishana na hivyo anguko lao huletwa na muwasho wa mwili ambao huwasukuma wapendanao hao kutoka ndani ya uhusiano wao na kufanya usaliti.

Sasa ili kulifanya penzi la aina hii liwe imara lazima wapenzi waulizane kuhusu kutimiziana haja za mwili wanapokuwa faragha. Kama kuna kasoro kati yao si busara kufichana wanatakiwa kuwaona wataalamu wa mapenzi na kupata ushauri utakaosaidia kuondoa tatizo hilo. Hawa pia wanashauriwa kutooana haraka.

PENZI LA UIGIZAJI

Penzi la aina ya tatu linalotajwa na watafiti ni lile lijulikanalo kama penzi la Uigizaji. Hili ni lile penzi ambalo wanaopendana hukutana asubuhi na ikifika jioni tayari ni wapenzi kamili, ambapo hugandamana kama ruba, utadhani waigizaji wako kwenye matayarisho ya filamu. Ukiwatazama wanakuwa kama vichaa na msukumo wao wa kutimiza hisia za mwili huwa ni mkubwa kiasi cha kufikia kufanya mapenzi hata barabarani au kwenye sehemu za wazi.

Wapenzi wa aina hii huchukua muda mfupi sana kutangaziana mambo ya ndoa na pengine kuoana bila kufahamiana zaidi kitabia. Wanajuana asubuhi na jioni mwanamke/mwanaume keshahamia kwa mwenzake na maisha yanaanza, hapo hakuna ushauri wala muongozo wa watu wengine.

Tatizo kubwa ambalo hujitokeza katika penzi la aina hii ni wapenzi kuchokana mapema na hamu ya kufanya tendo la ndoa kupotea. “Yaani nikiwa na mume wangu sijisikii kabisa kufanya naye mapenzi, lakini kwa wengine nakuwa na hamu sana” hizi ni kauli za wapenzi wa penzi la kisinema sinema.

Mbali na hilo wapenzi wa aina hii ni rahisi kuporwa na kuanzisha uhusiano mpya, hivyo inashauriwa kuwa kwa wale ambao wanaona kuwa wako kwenye kundi hili, wajitahidi kujizuia na kupeana nafasi za kujuana zaidi kupitia ushauri wa watu wengine. Si vema kushiriki tendo la ndoa kila mara kwa staili na sehemu zile zile na pia haifai kukurupuka kuoana bila kuchunguzana tabia, ndoa za hivi hazidumu.


PENZI TIMILIFU

Aina ya mwisho ya penzi kama inavyoelezwa na mtaalamu Sternberq ni ile ya penzi timilifu. Aina hii ya mapenzi inakuwa na sifa zote tatu, yaani TENDO LA NDOA. Kwamba wapendanao huwa hawana kasoro katika eneo hili, unapofika muda wa kupeana raha hufikishana mahali pa juu. UKARIBU kwamba muda wote huwa karibu na kila mmoja hakai na kiu ya kutokumuona mwenzake kiasi cha kupoteza hisia na kushawishika kufanya usaliti.

Sifa ya mwisho ni KUJITOLEA. Ni mahodari kusaidiana, kufarijiana na hawako tayari kupokea mambo kutoka pembeni yanayohusu uhusiano wao, hivyo huwa si rahisi kwao kuyumba kwa sababu za umbea. Kumbuka katika penzi hili tendo la ndoa huwa si sehemu muhimu sana kwa wapenzi, yaani kwao penzi ni rohoni zaidi kuliko mwilini hata wakikaa muda wa miezi mitano bila kufanya tendo la ndoa upendo wao haupungui.

Hata hivyo, penzi la aina hii kwa mujibu wa wataalamu ni vigumu kupatikana na ni vigumu pia kulilinda, lakini linatajwa kuwa ni aina ya penzi bora ambalo ni muafaka kwa maisha ya baadaye ya ndoa kwa wanaopendana. Watu wengi kwa kutotambua aina hii ya mapenzi wamejikuta wakiliharibu kwa kufikiri tu kwamba wapenzi wao wamefika na hivyo kufanya makusudi ya kuharibu misingi ya penzi.

“Nimeshamshika atakwenda wapi, nikikohoa tu anaitika” Kauli kama hizi ni hatari sana katika penzi hili, hivyo inashauriwa ukiona unapendwa na mpenzi wako katika aina hii ya penzi ni vema ukawa macho ili kutolivunja kwa uzembe wako na kudhani unababaikiwa kumbe unapendwa kwa dhati.

Labels: ,