Saturday, July 28, 2012

Kim Kardashian affairs..


  Kim Kardashian was married to Damon Thomas

2000-2004

Kardashian was 20 years old when she married Damon Thomas, a producer. A heated divorce followed with Kardashian claiming Thomas physically and emotionally abused her.







Kim Kardashian dated Ray J
2005-2007
Kim Kardashian met Ray-J while he was working as a stylist for his sister, Brandy. The two are said to be on and off again for nearly three years before things ended for good. In 2007 their split got really messy when a sex tape they made was picked up for distribution by Vivid Entertainment. At first Kim denied rumours of the tape's existance but later settled with Vivid
for $ 5 million.


  

Kim Kardashian dated Nick Lachey

2006 - 2006
Nick Lachey briefly dated Kim Kardashian after his divorce from Jessica Simpson in 2006. They were photographed together a couple of times, holding hands.
Kim Kardashian dated Nick Cannon

September 2006 - January 2007
Kim Kardashian and Nick Cannon dated briefly in late 2006, but it's unclear just how serious things got before they called things off.

Kim Kardashian dated Reggie Bush

2007 - 2009
These two quickly became a power couple, with pictures of the very photogenic pair regularly filling the pages of gossip magazines everywhere.

Kim Kardashian dated Reggie Bush

October 2009 - March 2010
After reconciling, it seems they couldn't make it last. Rumors say that Bush's family had issues with Kardashian's somewhat checkered past.
 Kim Kardashian had a fling with Shengo Deane
2010 - 2010
Kim Kardashian had a fling with Australian bodyguard Shengo Deane, but it wasn't meant to last. The two crossed paths twice, with Kim seeming to put things to an end on an episode of 'Keeping Up with the Kardashians.'




Kim Kardashian had a fling with Cristiano Ronaldo

April 2010 - April 2010
The two had whirlwind romance, with paparazzi catching the two in a kiss outside a restaurant in Madrid.




 
Kim Kardashian dated Miles Austin
June 2010 - September 2010
Kim Kardashian seems to have a thing for football players, dating both running back Reggie Bush and, more recently, Miles Austin, a wide receiver for the Dallas Cowboys. They called it quits in September 2010, with sources say their crazy schedules made dating too difficult.





Kim Kardashian was rumored to be with Michael Copon
October 2010 - October 2010

Kim Kardashian and 'One Tree Hill' star Michael Copon were rumored to be dating in October 2010. They met back in 2006 while starring in 'Beyond the Break' and allegedly reconnected in NYC and began dating.






Kim Kardashian was rumored to be with John Mayer

October 2010 - October 2010

Kim Kardashian was spotted out with John Mayer on at least a couple of occasions in October, 2010, but it's unclear whether any romantic connection was made.


    

Kim Kardashian was rumored to be with Gabriel Aubry

November 2010 - December 2010
Kim Kardashian and Gabriel Aubry were seen at a Lakers game together in November 2010, and a source said they've been dating "a little bit." In early December, sources said the two split, mostly because Kim thought he was just using her for fame. Typical.

Kim Kardashian dated Kris Humphries

December 2010 - May 2011
Fresh off the heels of a breakup with alleged beau Gabriel Aubrey, Kim started dating yet another athlete: New Jersey Nets player Kris Humphries. Wouldn't it be weird to have a mom and boyfriend with the same name?



       
Kim Kardashian was engaged to Kris Humphries

May 2011 - August 2011
After six months of dating, NBA player Kris Humphries got on one knee and proposed to Kim with rose petals that spelled out "WILL YOU MARRY ME?" He presented her with a 20.5-carat, $2 million Lorraine Schwartz ring.


  
Kim Kardashian was married to Kris Humphries
August 2011 - October 2011
Kim Kardashian and Kris Humphries were married in a lavish wedding attended by some of the biggest names in Hollywood on August 20, 2011. 'People' magazine reportedly paid $1.5 million for exclusive rights to photos of the wedding. The two announced they were separating about 10 weeks later on October 31, 2011. 

Kim Kardashian is dating Kanye West
April 2012 - Present
After watching 'The Hunger Games' together, grabbing dinner at NYC eatery Serafina, and spending the day at FAO Schwarz in early April 2012, it became clear that Kim Kardashian and Kanye West were more than just friends. In May 2012, they spent a week in Cannes together for the city's annual film festival.

Labels: , ,

PENDA KULA MBOGA ZA MAJANI NA UONE FAIDA ZAKE..

Baada ya utambulisho wa umuhimu na faida ya kula matunda na mboga kwani kila mboga na kila tunda vina nafasi tofauti ya kujenga na kulinda mwili. Watoto wengi wanasumbua sana kwenye kula hasa mboga majani asilimia kubwa sio wapenzi angalu upande wa matunda watoto wengi hupenda matunda lakini kwa kuchagua sio matunda yote watapenda kula tabia hii hujitokeza kwa kila mtoto hakuna aliekamilika nakumbuka hata mimi nilipokua mtoto nilikua nasumbua sana kula kiasi ikapelekea kua na afya dhaifu wakati wa kukua kwangu mpaka nilipobadili tabia na kuanza kula bila ya kufatiliwa.

Unaweza badilisha tabia ya mtoto wako au mtu yeyote unaeishi nae nyumba moja asiyependa kula mboga majani au matunda kwa kubadilisha muonekano wa chakula hicho au tunda hilo kwa kulinakshi kwa mtindo wowote ule ilimradi kionekane kitu tofauti na kinachovutia hii itakua njia rahisi sana kumvutia mtoto au mkubwa chakula kizuri au upambaji wa chakula sio mpaka hotelini hata nyumbani unaweza fanya sanaa hii na wala haiitaji muda mrefu wa maandalizi muonekano bora wa chakula hutia hamasa kwa mlaji leo tutaangalia utengenezaji wa salad na kuipamba na uandaaji wa mboga ktk muonekano wa kuvutia upande wa kuchonga matunda tutaangalia wakati ujao fata maelezo jinsi ya kutengeneza salad yenye mchanganyiko wa mboga mboga hapo chini.





Hili ni jokofu la kutunzia mchanganyiko wa mboga katika nyuzi joto 4 hadi 5 tu kwa hali ya usalama sana kwa manufaa na afya ya mlaji tukianzia juu kushoto ni mahindi mabichi ya njano kabla huifadhiwa katika kopo tayari kwa matumizi, karoti iliyokwaruzwa, Lime stone lettuce, chicory, Radish iliyokwaruzwa, zucchin iliyokwaruzwa, rollo nyekundu, rollo ya kijani, matango yaliyokatwa, celeriac salad, curly endive, chicory nyekundu.



Katika sahani yako anza kupanga mboga ambazo zimekatwakatwa  ambazo ni karoti, matango, mahindi machanga ya njano, celeriac salad na  radish nyeupe

Chota kidogo kidogo kila moja panga kwa mtindo wa duara nusu sahani tu kama mduara wa nusu mwezi kati kati acha nafasi kiasi.

Baada ya hapo chukua jani la salad moja moja toka kila aina ya salad pagange sambamba majani hayo kisha zungusha yabane kama unataka kuyafunga kamba kisha kata kiasi upande wa chini utakua umepata kitako safi utakua umetengeneza kama uwa rozi.

Kisha liweke juu ya zile mboga mboga pembei yake kata kipande cha tikiti maji rangi yeyote ile kama ni la kijani, jekundu au rangi ya chungwa pamba kama invyoonekana katika picha.

Kisha kata slice nyembamba ya chungwa katikati yake weka tunda lolote dogo la mviringo kama zabibu au strawbery chomeka toothpick ili ishikilie chungwa juu ya tikiti maji.

Salad hii unaweza mwagia dresing yeyote ile mfano italian dressing, french dressing au siki na chumvi inatosha salad hii unaweza kula na kipande cha kuku, samaki wakuchemsha au wa kukaanga na unakua umekula mlo safi kabisa bila stach kwa watu wanaofanya dayati hapa ni mahala pake mvuto na muonekano wa sahani utamfanya mlaji avutie hata kama si mpenzi wa mboga na matunda.



Hili ni jokofu la kutunzia mchanganyiko wa mboga katika nyuzi joto 4 hadi 5 tu kwa hali ya usafi sana kwa manufaa na afya ya mlaji tukianzia juu kushoto ni nanasi iliyopikwa katika sukari, embe mafuta, cappers, vitunguu vidogo vya kopo,  chopped chives, chopped onion, olives nyeusi, asparagus, matango machanga yaliyosindikwa, olives zakijani, Nyanya



Katika sahani yako anza kupanga mboga ambazo zimekatwakatwa ambazo ni karoti, matango, mahindi machanga ya njano, celeriac salad na radish nyeupe.

Chota kidogo kidogo kila moja panga kwa mtindo wa duara kuzunguka sahani yote katikati acha nafasi.

Baada ya hapo chukua jani la salad moja moja toka kila aina ya salad pagange sambamba majani hayo kisha zungusha yabane kama unataka kuyafunga kamba kisha kata kiasi upande wa chi utakua umepata kitako safi utakua umetengeneza kama uwa rozi.

Kisha liweke pembeni ya zile mboga mboga katikati ya sahani unaweza weka mchanganyiko wowote ule wa nyama ya kuku, ngo'mbe, samaki au sausage iliyochemshwa ikapoa.

Kata saizi ya kuweza kuingia mdomoni kisha changanya na vitunguu vilivyochopiwa safi pamoja chives.

Mchanganyiko huo unaweza malizia na chaguo lako la dresing yeyote uipendayo kisha unamwagia kati kati ya sahani mwisho kata nyanya kipande weka pamoja na tango dogo la kopo na olive moja ya kijani na moja nyeusi kwa kupamba salad yako.




Kwa upande wa mlo kamili baada ya kupika chakula chako kikaiva kama ni ugali au wali

Chemsha njegere zisiive sana

Kisha kata vitunguu vidogo sana kaanga katika siagi dakika 1 tu

Kisha weka hizo njegere zilizoiva katika sufuria kwa dk 2 usiasahau chumvi kisha zitoe

Chukua nyanya nzuri ngumu iliyokwisha iva kata nusu pia kata kidogo katika kitako ili iweze kukaa katika sahaki

Kisha toa mbegu zote katikati ya nyanya tumia kijiko kuchota na jaza zile njegere kwanye nyanya

Kisha save nyanya hiyo yenye njegere kama mboga majani itakayo ambatana na chakula chako kama ni cha mchana au cha usiku.

Muonekano na mchanganyiko wa rangi inakua kivutio kizuri sana kwa mtu asiependa kula mboga majani.




Sasa hapa ndio utawakamata kweli kweli wasiopenda kula mboga za majani,

Chukua maharage mabichi yachemshe kiasi yasiive sana yabaki na rangi yake nzuri ya kijani

Kisha unachukua bacon slice zipo aina mbili zipo bacon za nguruwe na bacon za ng'ombe chaguo ni lako mlaji.

Kisha chukua maharage hesabu kumi na tano kisha zungushia bacon katika maharage hayo weka katika ubao wa kukatia kata ncha za mwisho ili kuweka usawa na muonekano mzuri zaidi.

Ukishamaliza weka kikaango kwenye jiko la moto wa wastani tu weka mafuta kiasi katika kikaango yakishapata moto weka maharage yaliyozungushiwa bacon kaanga kiasi tu ili ile bacona ikauke.

Kisha toa tayari kwa chakula pia sevu kama mboga majani itakayo ambatana na chakula chako kama ni cha mchana au cha usiku. Muonekano na mchanganyiko wa rangi inakua kivutio kizuri sana kwa mtu asiependa kula mboga majani.
 
KWA KUFATILIA MAELEZO HAYA YOTE UTAKUA UMEFANIKIWA KUMREKEBISHA KAMA NI MUME AU MTOTO ASIEPENDA KULA MBOGA ZA MAJANI AU MATUNDA IKIWA UMESHAFAHAMU PIA UMUHIMU WA VYAKULA HIVYO KWA BINADAMU





Nashukuru sana mdau aliezungumzia upatikanaji wa bacon ya ng'ombe, nikweli kwa ulaya kupata bacon ya ng'ombe ni adimu sana ila hapa kwetu Tanzania zinapatikana kwa wingi ukienda katika supermaket kubwa au maduka makubwa ya nyama utapata.

Endapo umekosa basi chukua mboga hiyo hapo juu inaitwa leeks kata jani lake lisafishe vizuri kisha zungushia vizuri maharage yako hatua za upishi ni zile zile unaikaanga kidogo tu itaiva na italeta harufu nzuri sana kwahiyo kwa asie kula kabisa nyama atakua nae kafaidika.
Jumapili njema..
endelea kupata uhondo hapa hapa bongomixx

Labels:

Friday, July 27, 2012

*** Play gal - 54 ( Revenge)


Ilipoishia…

Nikiwa bado katika hali ya kuongea na dereva teksi na hata sikuwa nimepanda ile gari wala kupatana naye bei rasmi. Mara kwa ghafla akatokea mwanamama mnene mrefu kidogo. Alikuwa mweusi huku sura yake ikikunjamana vilivyo mithili ya mtu anapopigwa jua la utosi. Macho yake yalionesha kuwa tata kwani mbali na machozi yaliokuwa yakimtoka pia yalikuwa ni mekundu kama mtu aliyefiwa ama kumpoteza mume au mtoto wa kumzaa.
“..unakwenda wapi Malaya mkubwa wewe..?”
Aliuliza kwa sauti ya jazba. Sikuwa namtambua zaidi yakumtolea macho mimi pamoja na dereva teksi. Mwili wangu ulikuwa tayari umeshakata tamaa ya kuishi huku nikihisi kama kojo likiteleza ndani ya suruali yangu iliyokuwa imenibana…

Sasa endelea….
Uoga uliochanganyikana na kutetemeka mwili mzima ni kati ya vitu ambavyo vilikuwa bado vinasumbua halmashauri ya kichwa changu huku nikibaki njia panda nikiendelea kumkodolea macho yule Mmama alioonesha kunikazia macho vilivyo huku akiendelea kutoa matusi makubwa na mazito.
“...na leo ndio utanitambua vizuri..? yaani siku ya nne leo huonekani cha nyumbani wala hujui hata watoto wanaishije huko..? Wewe kazi kuendesha hiki ki teksii chako tena bila hata haya unaongea tu na wanawake shenzii kabisa wewe mwanaume..!”
Nilishusha pumzi huku nikinyanyua mkono wangu wa kulia nakushika kifua changu huku nikijihisi mapigo yangu ya moyo yalivyokuwa yakiendelea kunitoka. Nikatoa kitambaa nakuanza kujifuta futa jasho lilikokuwa limeshaanza kupenyeza kwenye uso wangu nakupitilizia shingoni. Kumbe yule dererva teksi niliokuwa naye ndio alikuwa akiongeleshwa na mke wake sijui. Aibu kubwa ikanijaa ghafla Tina mimi nakufikiri kuwa kumbe ningeumbuka kama ndio angekuwa mke wa mchungaji James.
“..Naona hapa tena hamna safari..?, embu ngoja nitafute usafiri mwingine…”
Niliondoka zangu nakuwaacha pale yule dereva teksi na mke wake wakiendelea kugombana. Nikatafuta teksi nyingine ambapo ilinifikisha mpaka stendi kubwa ya mabasi. Umati wa watu ulikuwa umefurika ndani ya stendi hii ya mabasi huku kila mmoja akiwa yuko ‘bize’ si kwa kubeba mizigo yake bali kwa purukushani za hapa na pale za kugombea tiketi. Nilijisogeza mpaka eneo la karibu na basi la ‘Mohammedi trans’ ambayo ni mabasi maarufu sana kwa safari ziiendazo dar es salaam.
“.. Nauli ya hapa mpaka dar shilingi ngapi..?”
“..nauli yake shilingi elfu  thelathini na nane tu..”
Nilichomoa hela kwenye suruali tena hela zenyewe zile nilizokuwa nimeziiba baada ya kufanya mauaji ya mchungaji James. Nikatoa shilingi elfu arobaini na kumpatia yule mkata tiketi.
“.. nipe tiketi moja..”
“..ya lini..? maana za leo mpaka kesho zote zimejaa…”
“..zimejaa..?”
“..ndio dada. Zimejaa na hapa unavyoona wanafunzi wengi wa vyuoni haswa wale wa chuo cha Mtakatifu Agustino na chuo cha biashara ndio wamefunga hivyo tangu juzi mabasi yanawabeba wao wanafunzi tu..”
“..Ooooh Mungu wangu..!! sasa nitafanyaje jamani na nahitajika Dar es salaamu leo leo hata niingie saa ngapi..?”
“..labda usubiri basi letu jingine linatokea Kigoma litapita hapa hivyo kaa pale usubiri..”
Kidogo akili yangu ikakaa sawa nakusogea mpaka eneo la kupumzikia abiria nakuanza kusubiri. Ilinichukuwa kama masaa mawili kusubiri huo usafiri wa kutokea Kigoma. Bado hakukuwa na dalili zozote wala hata taarifa zinazotia nguvu juu ya hilo basi litokalo huko kigoma. Jua kali lililochora kivuli kikubwa chini ilimaanisha dhahiri kuwa itakuwa tayari imetimu mchana tena ule mchana wakuanzia saa sita nakuendelea maana jua lilikuwa kali sana. Nilikiwa bado nimezubaa mwenyewe mara ghafla nikahisi kama kuna mtu ananigusa mgongoni taratibu. Sikutaka hata kugeuka kwani niliamini kwa asilimia zote huenda atakuwa ni mdudu ama kweli kuna mtu. Nilichukua mkono wangu wa kulia nakuanza kupapasa papasa kwa nia yakukitoa kitu kinachonigusa kwa begani. Kadri nilivyozidi kukitoa ndipo kilizidi kunibonyeza kwa nguvu na kwa sasa nikaanza kuisikia na muambatano wa sauti ya kike kwa mbali.
”..Samahani dada naomba kukuuliza kitu..?”
Alikuwa Mmama mwingine na ni  mgeni machoni mwangu kwani hata sikuwahi kumuona maishani mwangu. Sura yake pana iliyokuwa imeng’arishwa na manukato ya zile losheni zinazopendwa na baadhi ya kina dada wa uswahilini na waliokuwa na kipato kidogo. Zile  zinazojulikana sana kwa kubadilisha sura yako ya kutoka weusi nakuwa weupe. Wengi wanapenda kuiita ‘carolite’. Na kwa sasa harufu ile ya carolite ilikuwa inapambana na pua zangu zilizokuwa zimenasa harufu hiyo kali na inayochukiwa na baadhi ya wanaume wenye pesa zao. Niliendelea kumtolea macho huku nikijipa maswali mara mbili mbili ndani ya ubongo wangu nakuona sasa huyu huenda ndio akawa Mke wa mchungaji James kweli. Nilimkazia macho nakumjibu.
“..uliza tu mama yangu..?”
“..haya..! Ujue  nakufahamu sana binti japo wewe huwezi kunikumbuka mpaka nikukumbushe..?”
“..ni kweli unayosema mama..!”
Woga tayari ulishaninyemelea Tina mimi nakuona sasa haya ni majaribu haswa ya dunia. Nilikuwa mpole ghafla nakujidai mtakatifu tena Yule wa kanisani kabisa. Nilijinyenyekeza huku nikimtolea macho na kutega maskio yangu kwa kumsiliziza kwa umakini mkubwa.
“..nimekufuatilia muda mrefu.., kwanza kabisa pole na matatizo yaliokukuta kule tuliposafiri wote ikiwa ni pamoja na ajali tuliokuwa tumeipata..”
“..pole ya nini tena Mama. Mbona mimi sijasafiri nina muda mrefu nahii leo ndio kwanza nasafiri kuelekea Dar..?”
“..wala usitie shaka na mie. Mie nilikuwa mmoja wapo katika lile basi tulikuwa tumesafiri nalo jana kutoka Dar, na nakumbuka kabisa ulipandia kijiji fulani hivi japo kwa jina sikikumbuki na hapo ukapata siti tena kwa bahati nzuri ukakakaa na mchungaji mmoja hivi anaitwa mchungaji James..”
Akili yangu ikawa haitaki kabisa kukubaliaana na ukweli aliokuwa anaendelea kuongea huyu Mama. Sura yake kila nikiivutia kumbukumbu bado ilikuwa ni kazi kuikumbuka. Nilichokifanya niliendelea kumkana kama vile Yuda alivyomkana Yesu mara tatu..
“..wewe Mama utakuwa umenifananisha mie..?, embu niondokee hapa..!! Kwanza unavyoendelea kukaa na mimi, hiyo mikarolite yako inazidi kuharibu pua zangu..?”
Nilijifanya nimekasirika nakumgeuzia kibao yule Mama. Umati wa watu ukaanza kujaa katika eneo nililokuwa nimekaa na huyu Mama ukinizunguka. Yule Mama aligeuza macho yake huku na huku kana kwamba kafumaniwa ama ameona kitu cha ajabu sana kwangu.
“..nakupa dakika moja tu na wala siendelei.. Jibu ndio au hapana..?”
kwa muda huu yule mama alikuwa amebadilika sura na sauti nakuwa mbogo kwa muda. Kigugumizi cha ajabu kilichoambatana na kwikwi kali kikaanza kunishika Tina mimi huku nikiwa sina ujanja tena. Nikiwa bado najiandaa kumjibu yule Mama akanishika kwa nguvu ile blauzi yangu nakuanza kuropoka.
“..sasa utaeleza vizuri kwanini umemuua mchungaji wetu tena mchungaji James tuliokuwa tukimpenda sana kwa mahubiri yake..?”
Maskini Tina mimi nilijikuta nimeshaingia matatani tena, nilijitahidi japo kuzirudisha kumbukumbu kumtambua huyu Mama. Ndipo nikakumbuka kuwa jana wakati nipo safarini siti moja na marehemu mchungaji James aliniambia kuwa nilizimia mara mbili wakati ananiombea na tena wakisaidiana kuniombea na Mmama ambaye alikuwa mtu wa Mungu. Nilihuzunika sana nakuanza kuilaumu nafsi yangu kwa kutokufikiria. Nikiwa bado kwenye mawazo huku watu wakinishangaa mimi na huyu Mama. Mara huyu Mama akatoa sauti ya kuamuru kitu.
“.. jamani mapolisi binti mwenyewe ndio huyu hapa..!!, mchukuweni tumpeleke kituoni..”
Kumbe na mapolisi walikuwa wamenizunguka eneo lote nililokuwa nimezungukwa na watu ambapo walikuwa wamevalia nguo za kiraia. Walinichukuwa nakunipiga pingu huku umati wa watu ukinisikitikia kwa kitendo nilichokifanya cha kumuua mchungaji wao mchungaji James..





*** Inamaana ndio utakuwa mwisho wa safari ya Tina..?


*** Huyo Mama umeshamkumbuka..? na nini hatma ya Tina huko kituoni..?


*** Utamu wa story hii ndio kwanza unaanza kunoga. Endelea kufuatilia ujue ** Play gal – 55 itakuwaje..?



*****Itaendelea..*****
 

Labels:

Thursday, July 26, 2012

JIFUNZE KUPIKA KEKI HII YA MAZIWA AINA TATU

KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KEKI HII YA MAZIWA AINA TATU


MAHITAJI

240 gram unga wa ngano
1-½ kijiko kidogo cha chai Baking Powder
¼ kijiko kidogo cha chai Salt
5 yai zima, kisha tenganisha ute wa njano na mweupe
240gram Sukari, gawa nusu pembeni
1 kijiko kidogo cha chai Vanilla
30 gram maziwa ya maji
1 kopo la Evaporated Milk
1 kopo la Sweetened au Condensed Milk
60gram za cream nzito kabisa ( Heavy Cream)


KWAJILI YA ICING:


1 kijiko kikubwa cah chakula Heavy Cream, kwajili ya kupambia
3 kijiko kikubwa cha chakula sukari nyeupe ya unga
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEKEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi : 1 mpaka masaa 2

Muda wa mapishi : 30 dakika mpaka saa 1
Ukubwa na Idadi : utapata cake 2 


Washa kwanza oven kwa moto wa 350 degrees. Kisha chukua tray yenye size hii 9 x 13 inch unaweza paka siagi au ukaspray. Kisha chukua unga changanaya na baking powder pamoja na chumvi katika bakuli kubwa.

Kisha chukua bakuli safi na kavu weka ute wa yai wa njano pamoja na sukari 180 gram piga kwa kutumia mchapo kwa nguvu sana au kama unatumia mashine basi weka spidi kali.

 

Hakikisha inakua muonekano huu baada ya kupiga na mshine unapata rangi ya cream.



Kisha chukua yale maziwa ya maji pamoja na vanilla kisha chukua mwiko huo na changanya pole pole mpaka vyote vichanganyike vizuri.


Kisha chukua ute mweupe wa yai (egg whites) piga tena kwa kutumia mashine kwa spidi kali mpaka uone imetoa mapovu kabisa na kuongezeka. 



Baada ya kutoa povu basi chukua sukari 60 gram na mimina katika mchanganyiko huo wa ute mweupe wa yai.


Endelea kupiga tena kwa kutumia mashine kwa spidi kali hakikisha imekua laini kabisa kama mapovu lakini isikwe kavu.



Unaona muonekano baada ya kua katika kiwango safi na imetengeneza kama milima miwili?



Chukua ule mchanganyiko mweupe wa yai changanya pamoja na mchanganyiko ule wa unga.



Hakikisha unachanganya pole pole

 


Mpaka ichanganyike vizuri kabisa.


Kisha mimina mchanganyiko wako kwenye tray ulioandaa kwajili ya kuokea hakikisha unasambaza vizuri.

 

Choma kwa dakika 35 mpaka 45 au mpaka toothpic ukitoa inabaki kavu. Mara yangu ya kwanza kuipika keki hii nilifungua oven zaidi ya mara 100 ambayo ni kosa sababu ya harufu nzuri ilioenea jikoni kila muda nahisi labda imeshaiva! Nadhani ndio maana keki yangu ilinywea hahahahaaaa! usifanye kosa hili ingawa taste yake ilikua YUMMO!



Keki yako tayari inarangi safi sana ya kahawia kisha chukua condensed milk, evaporated milk pamoja na heavy cream changanya.


Hakikisha unachanganya pole pole mpaka ichanganyike vizuri.

 

Baada ya keki yako kuiva weka pembeni ili ipoe na ikishapoa, Chukua uma na uitoboe pole pole . 


KIsha chukua mchanganyiko huo wa nmaziwa na cream mwagia juu ya keki na uruhusu ipoe kwa dakika 30. Weka kwenye friji ili ipate ubaridi kabisa isisumbue unapoipamba na icing. Chukua  heavy cream na vijiko 3 vyasukari kisha piga pamoja. 

 

Hakikisha unapiga mpaka inalainika kabisa.


Hakikisha unapakaza vizuri icing yako juu ya keki yote ili kuongeza ladha, ingawa mimi huwa nagawa nusu napaka na nusu sipaki maana sio watu wote wanapenda cream. Umeona muonekano baada kukata kipande? Unaona muonekano wa maziwa sehemu tuliokata kipande cha keki? maziwa unayoweka katika hii keki hayatabadiklisha sana keki yako iwe tepe tepe bado itakua na hali ya sponji.



Keki hii asili yake ni nchi ya spain wao wanapenda sana kupambia kwa juu matunda aina ya peaches na cherries. Kwakua ilikua ni msimu wa maembe mi nikaona kwanini nisipambie maembe ?!


Baada ya kupaka cream kwa juu kisha pamba na maembe na kata vipande kama muonekano katika picha.



Ukitafuna utaona sponji safi kabisa na ladha safi
 


Pia hata hotelini unaweza kuuza keki hii kama chakula kitamu baada ya mlo kamili
 



Waandalie nyumbani waweze kufurahia keki hii kwa chai ya jioni au baada ya chakula.

Labels: