Friday, August 31, 2012

Mambo 10 yanayozuia mafaniko ya kimasomo



UMASIKINI

Umasikini ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya wanafunzi kimasomo, lakini tunashauri kwamba kila mwanafunzi anayetoka katika familia masikini ajitambue na awe tayari kuishi sawa na kipato cha familia yake wakati akitafuta elimu.

Ni muhimu kwake kubana matumizi na asiwe mtu wa kujihukumu kwa kukosa hili na lile, awe mvumilivu na mwenye kuomba msaada kila sehemu anayoona hawezi kuivuka kwa nguvu zake. Uaminifu, bidii na utii unaweza kumsaidia kuvuka kikwazo hiki.

Kuhusu suala ya kufukuzwa shule kwa kukosa ada ni vema kwa mwanafunzi mwenye kipato kidogo akawasiliana na mwalimu wake au viongozi wa serikali ili wamsaidie kutatua tatizo. Haifai kujifungia chumbani na kuanza kulia au kuamua kuacha shule kwa kukosa mahitaji. Mambo yote yanawezekana kinachotakiwa ni nia, mipango na uvumilivu.


MAPENZI

Kama kuna mtu hafahamu nini maana ya mapenzi basi kuanzia leo ajue kuwa mapenzi ni ulevi kama vilevi vingine. Mtu anayependa hulewa na kujikuta anaharibu ufahamu wake kama mtu aliyelewa pombe.

Walevi wa mapenzi huweza kufanya mapenzi hata barabarani sehemu ya wazi, huku akili zao zikiwapa taarifa kwamba watu hawawaoni, mambo ya aina hii hufanywa pia na walevi wa pombe.

Lakini ulevi wa mapenzi una nguvu kubwa ya kuiteka akili na kumtia mtu mshawasho kiasi cha kuacha kazi muhimu na kukimbilia kufanya ngono.

Hivyo, mwanafunzi ambaye anataka mafanikio ya kimasomo lazima aweke kando masuala ya mapenzi kwa lengo la kutoitwika akili mzigo ambao kwa umri wa wanafunzi wengi hasa wa kike ambao ni waitikiaji wa kauli za wavulana ni vigumu kwao kuhimili.

Licha ya baadhi ya watalaamu wa masuala ya afya kubainisha faida za kufanya mapenzi kwa afya ya mwili, bado uchunguzi unaonyesha kuwa wanafunzi wengi ambao wengi wao huwa katika umri mdogo hushindwa kuzuia hisia za mapenzi na kujikuta wanakuwa watumwa wa ngono.

Mapenzi kwa mwanafunzi yana hasara za aina mbili. Kwanza, mapenzi yanapokuwa moto huteka hisia na kumfanya msomi atumie muda mwingi kuwaza juu ya mahaba na hivyo kuufanya ubongo uone kuwa mapenzi ni kitu muhimu na hivyo kujituma kuhifadhi mambo ya mapenzi kuliko masomo.

Jambo la pili ni machungu ya mapenzi hasa yanapokuwepo mafarakano, mfano kuachwa, kusalitiwa, kuudhiwa, kugombana na migogoro yote ya kimapenzi huleta msongo wa mawazo na kumfanya mwanafunzi asiweze kusoma kwa kiwango stahili. Hivyo, inashauriwa kuwa mwanafunzi asijihusishe kabisa na mapenzi.

MIGOGORO YA KIFAMILIA

Kizuizi kingine cha kufanikiwa kimasomo kwa mwanafunzi ni kuwepo katika familia zenye migogoro. Baba na mama hawaelewani, ndugu wanagombania mali na kadhalika. Lakini inashauriwa kuwa mwanafunzi anayetoka katika familia za aina hii hatakiwi kujiingiza katika misuguano ya kifamilia.

Anachotakiwa yeye ni kuwaza juu ya masomo na kutupilia mbali mawazo yote yanayochipuka kuisumbua akili kuhusu mambo makubwa ya kiukoo. Kimsingi ufahamu wa mtoto hasa wa madarasa ya chini ni mdogo, hivyo hawezi kutatua mambo ya wazazi na akijaribu atakuwa anajisumbua na kujiweka katika matatizo makubwa zaidi.

Jambo muhimu kwake katika ngazi ya maisha yake ya shule ni kusoma na kama atakuwa na kitu cha kulilia ni mahitaji ya shule tu, na akiona migogoro hiyo inaathiri masomo yake, labda ada hazilipwi anachotakiwa kufanya ni kuwaeleza wazazi na ndugu wamsaidie kuhusu haki yake ya kupewa elimu na akishindwa katika ngazi hiyo awasiliane na viongozi wa serikali kwa ngazi yake ili wamsaidie.

KUFIWA NA WAZAZI/WALEZI

Uchunguzi unaonesha kuwa watoto wengi hushuka kimasomo baada ya wazazi au walezi wao kufariki. Hapa kuna mambo mawili, kwanza ni huzuni na pili kukosa upendo toka kwa walezi wao wapya.

Kuhusu huzuni mwanafunzi aliyefiwa na wazazi anashauriwa kuacha kabisa kuishi na wazazi wake waliokufa kwenye akili, haitakiwi muda wote kuwaza jinsi wazazi walivyokuwa wakimfanyia mema katika maisha. Wanasaikolojia wanasema hakuna jambo baya la asili isipokuwa mawazo ya mtu mwenyewe.

Ieleweke kuwa jinsi mtu anavyowaza ndivyo anavyojiumiza, huku ukweli ukibaki kuwa hawezi kuwarudisha wazazi wake duniani. Hivyo basi kila wakati mwanafunzi ambaye ni yatima anapoingiwa na mawazo ya kuwakumbuka wazazi anatakiwa kuyaacha kwa kuzungumza na wenzake, kucheza au kutazama sinema za kufurahisha. Si busara kutazama picha za wazazi enzi za uhai wao na kupendelea kuwazungumzia kila mara.

MALEZI YA BUGHUDHA

Baadhi ya watoto ambao wanalelewa na ndugu au walezi ambao si wazazi hukumbwa na kadhia ya kubughudhiwa kwa matusi na maneno ya masimango, kupangiwa kazi ngumu na kunyimwa muda wa kujisomea. Usumbufu huu wa kimalenzi upo hata kwa baadhi ya wazazi ambao wanakasumba za kubagua watoto.

Lakini ushauri unaotolewa hapa ni kwamba maisha siku zote hayana njia ya mkato na watafiti wa masuala ya maisha wanasema misukosuko ya kimaisha ina faida kwa watu wenye uelewa. Wakomonisti wanasema huwezi kutambua uwezo wa nahodha kwenye bahari iliyotulia bali kwenye dhoruba kali.

Ni wazi kuwa mwanafunzi anayesumbuliwa kwa bughudha ana nafasi kubwa ya kushinda masomo kama atazichukua kadhia hizo kama changamoto za kumfanya asilale na kujitambua kuwa yuko kwenye bahari chafu isiyo salama.

Ukiwa kwenye familia za aina hii, soma kwa bidii, usijihukumu sana, jishushe na uwe tayari kutumia unachopewa bila kunung’unika, usijibu mapigo kwa ugomvi au kufokeana na wakubwa wanao kulea. Uwe tayari kutumika kama mtumwa ili baadaye uishi kama mfalme. Ila kama mambo yatazidi pendelea kushauriana na wazee wa ukoo au majirani ili wakutanue mawazo.

STAREHE

Maisha ya shule yanakata nidhamu ya matumizi ya pesa, muda na sheria za shule. Mwanafunzi hawezi kufanikiwa kimasomo kama ataendekeza mambo ta starehe, mfano kwenda disko, kukesha baa na kushiriki mapenzi na wanawake/wanaume kwenye majumba ya anasa.

Haishauriwi mwanafunzi kuwa mtu wa starehe kwani ni rahisi sana kwake kupata matatizo ambayo yanaweza kumharibia masomo yake, mfano kupigwa na kuumizwa, kukamatwa na polisi na kuhusishwa na matukio ya uhalifu na hata kukosa muda wa kuupumzisha mwili na akili.

UFUNDISHAJI DUNI

Walimu wasiokuwa na sifa za kufundisha ni tatizo kwa mafanikio ya mwanafunzi kimasomo, lakini wakati huo huo uhaba wa walimu nao huchangia kushusha kiwango cha kufaulu. Inashauriwa kuwa wanafunzi ambao hawafundishwi vizuri wamuone mwalimu wao wa taaluma na kumueleza tatizo lao ili ufumbuzi upatikane.

Lakini wakati huo huo ni sahihi kuwasiliana na wazazi/walezi na kuwataarifu uhaba wa walimu kwenye shule yako na kuwataka wakusaidie. Inaposhindikana kwa ngazi ya familia ni vema viongozi wa kitaifa wakajulishwa na hatua za kuhama shule zinaweza kufikiwa endapo kikwazo hiki kitakosa ufumbuzi.

UKOSEFU WA VIFAA

Shule nyingi zimekuwa hazina vifaa vya kutosha, hili nalo ni tatizo kubwa na dawa yake ni kwa wazazi wanaojiweza kuhakikisha kuwa wanawanunulia watoto wao vifaa binafsi vya kujisomea. Wakati huo huo ni wajibu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali kuwa na utamaduni wa kubadilisha vitendea kazi ili kupata unafuu wa tatizo hili.


KUHAMISHWA SHULE

Mwanafunzi anapohamishwa shule anaweza kuathirika kisaikolojia, lakini kama imebidi ni vema akatumia vidokezo nilivyoeleza huko nyuma katika kupata uenyeji na kuzoea mazingira mapya.

Haipaswi kuhuzunikia marafiki na walimu alioachana nao na kusahau kuwa yeye anajukumu la kusoma kwa bidii na kupata matokeo mazuri.

UDHALILI

Kuna wanafunzi ambao wanashindwa kufanikiwa kimasomo kwa sababu wanajiona wao ni duni mbele ya wenzao katika mavazi, uwezo wa kifedha na kadhalika. Kwao linakuwa ni jambo ngumu kujieleza mbele ya wenzao na muda wote hujawa na aibu na hali ya kutojiamini.

Kasoro hii ni kubwa na huwakwamisha wengi katika kupata uelewa wa mambo. Ni wajibu wa mwanafunzi kujiamini na kutupilia mbali aibu na kueleza hisia na kile anachofahamu mbele ya mwalimu na wanafunzi wenzake bila kujali kama atakosea au atachekwa. Mwanafunzi anatakiwa kuwa na mazoea ya kubadilishana mawazo na wengine na kuacha kujitenga.

Tabia hii si nzuri, mwanafunzi ambaye anataka kuwa na kumbukumbu juu ya yale aliyojifunza lazima awe tayari kushirikiana na wenzake katika kusoma, kujadiliana na kusaidia.

Labels: ,

MAGAZETI YA LEO..

Friday, August 31, 2012

Magazeti Leo Ijumaa













Labels:

Wednesday, August 29, 2012

Magazeti Leo Jumatano Tarehe 29.08.2012















Labels: ,

Tuesday, August 28, 2012

MAGAZETI YA LEO TAREHE 28.08.2012

Magazeti Leo Jumanne
















Labels:

Monday, August 27, 2012

VITU VINAVYOWAHARIBIA WANAWAKE KIMAPENZI


vKUNA msemo kuwa: “Wanawake, mwalimu wao ni kipofu.” Mimi siuamini kwa maana umekaa kiukandamizaji zaidi. Haujengi heshima kwa mtu wa jinsi ya kike tangu analizaliwa mpaka anapoingia kaburini. Binafsi naamini wapo wenye uelewa mkubwa lakini wanashambuliwa na mapokeo ya samaki mmoja akioza.

Ni msemo ambao ukiingia kwenye vichwa vya watu unaweza kuwafanya wanaume wawadharau hata mama zao. Mama anatoa mafundisho lakini kijana anasikiliza, linaingilia sikio la kwanza na kutokea la pili. Kichwani anajiongeza: “Aah, hawa si mwalimu wao kipofu?”

Msemo huo unamaanisha kuwa wanawake huwa hawajui waendako. Kwamba njia ya kupita walifundishwa na mwalimu mwenye ulemavu wa macho. Siupendi kwa sababu siyo tu hauna ladha nzuri kwa mwanamke bali pia kwa mtu mwenye ulemavu husika. Unadhalilisha kupita kiasi.

Tangu nikiwa na umri mdogo, nilipenda sana kusikiliza busara za watu walionizidi umri. Niliamini wananijenga na kweli walifanya hivyo. Mtazamo huo, ulinifanya nijue mengi nikiwa na umri mdogo. Hata haya ninayoandika na kushauri, yanatokana na elimu niliyopata kwenye kada tofauti.

Wakati huo sijui ndani ya mwanamke kuna nini, mtu mmoja aliniambia: “Mdogo wangu Luqman, napenda unavyopenda kukaa na sisi wakubwa. Unaweza kuwa na busara katika maisha yako lakini usipokuwa mwangalifu, mwanamke anaweza kukufanya uonekane mwendawazimu mtaani.

“Siku ukiwa na mwanamke, jaribu sana kuwa mwangalifu. Unaweza kumpa kila atakacho lakini mwisho akakuuguza uendawazimu. Ukatembea barabarani unazungumza peke yako kama kichaa au ukiwa nyumbani ukashinda unabwabwaja maneno yasiyoeleweka mpaka majirani wakakuona mwendawazimu.

“Mkeo anaweza kutoka nyumbani anakwenda kumtembelea shangazi yake, kwa kumthamini na kwa sababu huna gari, ukampa fedha ya kukodi teksi. Akitoka njiani, anakutana na dereva teksi anampa lifti. Huwezi kuamini, huyo aliyempa lifti ndiye atamuona bora, mwenye roho nzuri kuliko wewe uliyempa fedha ya kuchukua teksi.

“Matokeo yake ni kwamba akishamuona ni mkarimu sana, anakuwa mnyenyekevu hata kwenye maeneo mengine. Mwisho wanakuwa wapenzi. Hiyo ndiyo tabia ya mwanamke, atasahau mema yako, hatajali watoto mnaolea.” Huyo mtu aliyeniambia maneno hayo anaitwa Jaffari, ni mtu mzima hivi sasa. Enzi hizo nilikuwa nasoma sekondari Mwanza.

Ukweli upo wapi? Ninachoweza kueleza ni kwamba wapo wanawake waungwana mno hapa duniani. Wanadumisha mapenzi ya dhati bila kusaliti licha ya kukumbana na vishawishi kemkem. Wanajua thamani ya wapenzi wao pamoja na changamoto zinazoweza kuwakabili katika maisha.

Hata hivyo, kuna aina ya wanawake ambao Jaffari alikutana nao ndiyo maana akasema hivyo. Isingekuwa rahisi kutoa maneno hayo pasipo kuona kitu. Inawezekana alitendwa na mkewe au alishuhudia kitu kwa rafiki yake, hivyo kumpa tafsiri aliyojijengea kuhusu wanawake.

Tukishika moja kuwa kuna kitu alijionea, basi ni vema kuwazungumzia wanawake ambao walimfanya akawa na mtazamo huo. Hao ndiyo wanaowaharibia wengine mpaka wanakosa thamani. Mtu anatendwa na mkewe lakini lawama anazielekeza kwa wanawake wote kwamba eti ndivyo walivyo!
Jambo ambalo mtu hapendi afanyiwe, basi asianze kumfanyia mwenzake.
Heshima, woga na ‘breki’ katika kauli, vinapaswa kuzingatiwa. Kusaliti maana yake umekosa woga, heshima na busara ya kimapenzi na maisha kwa jumla.
Hekima ni ipi? Kuendelea kuwa na mwenzi ambaye hana heshima juu yako, hakuhofii kwa chochote, wala busara ya maisha haimuongozi kutenda yaliyo mema kwa ajili ya ustawi wa familia yenu. Bila shaka, hekima inafaa kukuongoza kuchukua uamuzi kwa ajili ya furaha na amani ya kudumu baadaye.
Nitoe hoja kuwa hata wanaume wapo wenye matatizo mtindo mmoja, kwa hiyo na wanawake wapo wenye hulka tofauti.
Kama huyo wako ni pasua kichwa, basi wapo waliojaliwa utulivu, heshima, hekima na maarifa ya kudumisha uhusiano. Ikiwa huyo anakunyima furaha, angalia kama unaweza kujivua gamba, kwani wapo wanawake wema.
Mungu hajaumba mtu akamfanya kuwa mbaya kwa asilimia 100, Shetani ndiye anayeharibu vichwa vya watu na kuwafanya wawe na akili zisizofaa. Hata katika jamii ya Wasamaria, alipatikana mmoja aliye mwema ndiyo maana akaitwa Msamaria mwema.
Hivyo basi, wasisemwe vibaya wanawake wote kwa ajili ya makosa ya wachache.
Hata hivyo, hao wachache wanapaswa kubadilika ili wawape heshima wenzao.
Tamaa haifai kwa namna yoyote.
Binafsi nawaheshimu wanawake kwa maana ndiyo waliotufanya tustarehe kwenye matumbo yao kwa miezi tisa, wanawezesha tuitwe akina baba na kadhalika.
Mambo hayo makuu, hayapingiki ndani ya kila mwanaume isipokuwa Adam.
Pamoja na hivyo, zipo dhana nyingine nyingi ambazo zinafanya wanawake wasemwe vibaya. Twende kwa mifano.
Hivi karibuni, niliitwa nimshauri kijana mmoja ambaye kwa hakika alikuwa amechanganyikiwa kabisa.
Alichanganywa na mapenzi.
Mwanamke ambaye aliamini ndiye wa maisha yake, alimuacha katika mazingira ambayo hakuyategemea.
Alikuwa anamhudumia kwa kila kitu lakini akapigwa kibuti kwa SMS.
Kijana huyo anaitwa Mully, akiwa kazini kwake, akaona SMS iliyotoka kwa mtu ‘aliyemsevu’ kwa jina la My Dream.
Kama ujuavyo tena mapenzi, kijana akafungua haraka, akitegemea atapata maneno matamu kutoka kwa mwenzi wake lakini alichokutana nacho ni hiki: “Kuanzia leo, mimi na wewe basi.
Nimepata mchumba nataka kuolewa.”
Mully aliposoma maneno hayo akapagawa, akaamua kupiga simu ya mpenzi wake lakini hakupokea.
Akaamua kumuuliza kwa SMS: “Baby upo serious au unatania?” Haikupita hata dakika moja, majibu yakarudi: “Nipo serious kabisa, tena kuanzia leo usiniite baby na usinijue kwa lolote.”
Meseji hiyo ikamchanganya akili kijana, akaondoka kazini kwake bila hata kuwaaga wenzake.
Yule mpenzi wake anaitwa Janette, ni mtumishi wa ndani kwenye nyumba ya ofisa wa benki Masaki, Dar. Kijana akaondoka kazini kwake Mwenge hadi kazini kwa mkewe. Akili siyo zake.
Itaendelea wiki ijayo

Tunaendelea kuchambua kuhusu dhana ambazo zinawaharibia wanawake kimapenzi. Katika kuhakikisha somo linaeleweka sawia, mwishoni mwa makala ya wiki iliyopita, nilieleza mfano huu:
Hivi karibuni, niliitwa nimshauri kijana mmoja ambaye kwa hakika alikuwa amechanganyikiwa kabisa.
Alichanganywa na mapenzi. Mwanamke ambaye aliamini ndiye wa maisha yake, alimuacha katika mazingira ambayo hakuyategemea. Alikuwa anamhudumia kwa kila kitu lakini akapigwa kibuti kwa SMS.
Kijana huyo anaitwa Mully, akiwa kazini kwake, akaona SMS iliyotoka kwa mtu ‘aliyemsevu’ kwa jina la My Dream. Kama ujuavyo tena mapenzi, kijana akafungua haraka, akitegemea atapata maneno matamu kutoka kwa mwenzi wake lakini alichokutana nacho ni hiki: “Kuanzia leo, mimi na wewe basi. Nimepata mchumba nataka kuolewa.”
Mully aliposoma maneno hayo akapagawa, akaamua kupiga simu ya mpenzi wake lakini hakupokea. Akaamua kumuuliza kwa SMS: “Baby upo serious au unatania?” Haikupita hata dakika moja, majibu yakarudi: “Nipo serious kabisa, tena kuanzia leo usiniite baby na usinijue kwa lolote.”
Meseji hiyo ikamchanganya akili kijana, akaondoka kazini kwake bila hata kuwaaga wenzake. Yule mpenzi wake anaitwa Janette, ni mtumishi wa ndani kwenye nyumba ya ofisa wa benki Masaki, Dar. Kijana akaondoka kazini kwake Mwenge hadi kazini kwa mkewe. Akili siyo zake.
Alipofika, akagonga geti halikufunguliwa, kwa hiyo akapanga matofali getini akakaa. Baadaye Janette akatoka, alikuwa anakwenda dukani, akakutana uso kwa uso na Mully. Yakaanza maneno, baby nimekukosea nini? … sikutaki… baby niambie kosa langu… nimesema sikutaki...
Mtoto wa kike akaona ubishi unampotezea muda, akaingia ndani, akatoka nje na beseni la maji machafu, akamwagia Mully. Kijana wa watu akaloa chapachapa. Janette akarudi ndani, akapiga simu kwa bosi wake, punde polisi wakafika na kumzoa, eti ni mwizi.
Kaka yake Mully akaenda kumuwekea dhamana Oysterbay Polisi. Kuanzia hapo kijana akawa chini, akawa anazungumza hovyo, kazi akawa hafanyi. Kijana akasema: “Mbona mimi ningemuoa tu, sina shida.” Kijana akawa hali, haogi, kazi hafanyi. Akili zikamruka.
Nilijitahidi kumpa ushauri unaofaa kwa vipindi vitatu ndani ya siku tatu mfululizo, baada ya kuona anapata nafuu, nilishauri apelekwe eneo ambalo atabadili mazingira. Alipelekwa nyumbani kwao Singida. Wiki iliyopita, alirudi Dar akiwa mpya kabisa. Anatazama mbele na hamfikirii tena yule mwanamke.
Hata kazi anaendelea vizuri. Machungu ya kuachwa na Janette yamebaki historia. Vema amekaa sawa lakini kitu ambacho kipo wazi ni kuwa Mully alimpenda sana mpenzi wake na aliamini ndiye mwanamke wa maisha. Hali hiyo ndiyo ilimfanya ashindwe kupokea matokeo ya kuachwa.
Alishawekeza mambo mengi kwa Janette hususan rasilimali. Mully aliniambia kuwa kwa siku alikuwa anampa Janette kuanzia shilingi 15,000 mpaka 20,000. Alikuwa anamnunulia mavazi ya kisasa, kiasi kwamba ukimuona, usingeweza kudhani ni mfanyakazi wa ndani.
Baadaye ikaja kubainika kuwa kumbe Janette alipata kiburi cha kuachana na Mully kwa sababu ya bosi wake. Kwamba yule ofisa wa benki baada ya kumuona mfanyakazi wake anameremeta, akaamua kujiweka, binti naye badala ya kufikiria kuwa ni mume wa mtu akakubali.
Wameendelea kuwa na uhusiano lakini za mwizi ni 40, mke akashtukia kuwa anaibiwa mumewe ndani ya nyumba yake. Akamtimua kazi Janette na kipigo juu. Yule jamaa wala hakumtetea ndiyo kwanza akashiriki kusaidia kumtimua. Binti aende wapi? Kazini ameshaharibu, kwa Mully nako alishalikoroga.

Labels: ,

***Play gal - 60 (Revenge)



Ilipoishia…

Chumba kilikuwa nikikubwa sana ambapo ndani yake kulikuwa na kila kitu. Kuanzia choo na bafu. Kitanda kikubwa. Nilimvua mwanangu Adrian nguo zake nakumpeleka bafuni ambapo nilimuogesha nakisha nikambadilisha pampasi, baada ya hapo nikaoga na nilipotoka kuoga tu Aisha tayari alikuwa chumbani kwangu kitandani na Adrian ananisubiri nitoke kuoga.
“..Tina nimekuletea nguo hizi hapa, mie huwa zinanibana sana si unajua kunenepa kwangu ovyo tena..!!”
“..Ooh..!!, ahsante Aisha..”
“..ila kuna kitu nahitaji ujue…

Endelea….

Mwili wote ukanisisimka kwa haraka na ghafla kuanzia kichwani mpaka miguuni. Kutokana na kule kutetemeka nilijikuta kuishiwa nguvu mwilini nakuhisi kama kojo linaanza kunidondoka mtu mzima huku akilini nikiwa na shauku kubwa ya kujua ni kitu gani hicho anachotaka kuniambia Aisha.
“…Eennhee shosti..!!  kitu gani tena hicho mbona waniacha roho juu na njia panda mwenzako....??”
“..njoo kwanza mpaka hapa kitandani.., halafu ukiwa katika kujifuta vizuri na kubadilisha nguo mimi nitakuwa nikikusimulia, sawa shosti wangu Tina..?”
“..ni sawa tu hamna neno, au mtoko nini jamani..?”
“..mbona una haraka kiasi hicho jamani hata sijakwambia ni kitu gani..?, siyo mtoko wala nini..??”
“..Sasa ni kitu gani hicho cha kunitia roho juu mwenzangu, wangwi wangwi hadi umeninyima raha na kunipa karaha kwa muda..?”
Muda wote Aisha ailionekana kama mtu wa masihara masihara kwani ni kweli alionesha kuna kitu anataka kuniambia, lakini hakuwa siriazi kwani alikuwa akicheka cheka huku akinipa mkono kwa kugonga.
“..hivi yule mchumba wako wa zamani ‘Jerry’ ushawahi kumuona..?”
Mapigo yangu ya moyo yalibadilisha uelekeo pale aliponitajia jina la ‘jerry’. Sikutaka kabisa kumsikikia Jerry  masikioni mwangu Tina mimi na hata sura yake kwani yeye ndio chanzo cha mimi kuishi maisha haya ya shida nakutangatanga mpaka hivi sasa.
“..kiukweli shosti wangu Aisha. Huyo ‘Jerry’ ndio kwanza nakusikia unamtaja wewe leo hii, kwani toka enzi hizo sikumtia machoni na si unakumbuka alichonifanyiaga kipindi cha nyuma mpaka tukamfanyizia nakumkata kata nanihii yake kwa kutumia viwembe si unakumbuka..?”
“”..hehe heee..!!, halooo!!! Nakumbuka shosti..!!, lakini nadhani yale yalishapita siku nyingi sana, ila kuna jipya nataka nikujuze shosti wangu Tina ambalo hulijui..?”
Sasa nikatuliza pumzi zangu huku nikimtolea macho Aisha aniambie ni kitu gani hicho..
“..haya niambie shosti kwani amekuwaje huyo Jerry..?”
“ni stori ndefu sana Tina lakini maadam upo nitakusimulia kila kitu na utajua nakuelewa tu huyo Jerry. Kwanza kabisa unajua kipindi kile tumemfanyizia  kwanza hakututambua kama ni sisi ndio tulimfanyia ule unyama wa kumkatakata nanii yake kwa viwembe hadi kumpelekea kuharibika njia ya kutolea mbegu za uzazi. Tina..?”
“nakusikia endelea tu..?”
“..najua hutaweza kuamini lakini inakubidi tu uanzae kuamini kwani Jerry kwa sasa amekuwa ni mtu wa karibu sana na mimi..?”
“..bado sijakuelewa elewa Aisha , unamaanisha nini haswa..?”
“..nimekuwa msaada mkubwa sana kwa Jerry katika maisha yake.. Kuna siku moja nilikuwa naelekea kufanya ‘shopping’ zangu pale Mlimani city na kwa bahati nikakutana nae uso kwa uso. Kwa kuwa nilikuwa katika kipindi kigumu sana cha chuo si unajua tena bumu likiisha tunavyotaabika sisi..?”
“..ni kweli..?”
“..basi nikajikomba Aisha mimi kwa Jerry nakujifanya namjua kuliko. Kwa kuwa siku hiyo alikuwa peke yake ikawa ni rahisi sana kumshawishi. Jerry alionesha yuko tofauti sana kwani alikuwa ni mtu mwenye msimamo haswaa. Lakini akaniambia yuko tayari kunigharamia kiasi chochote cha pesa endapo tu nitamtekelezea mambo mawili makubwa kwake..?”
“..hee makubwa..!!, mambo gani tena..??”
Akili yangu sasa ikawa kama imenivurugika huku nikibaki njia panda na nisielewe ni kitu gani hicho ambacho aisha ameambiwa na Jerry. Mawazo yangu yote yakanirudisha mpaka siku niliyoota kuwa nachukuliwa mwanangu na Aisha wakisaidiana na Jerry na kisha nikabakwa na vijana nisioweza kuwatambua..
“..inawezekana ile ndoto ikawa kweli na leo hii ikanitokea ‘live’..?”
Nilijisemea kimoyo moyo huku sura ikinibadilika nakumuangalia mwanangu Adrian pembeni. Hasira kali iliyoamsha misuli pembezoni mwa uso wangu huku ikihamasisha dukuduku kali moyoni. Japo alikuwa hajamalizia kuongea lakini akili yangu ikawa imeshabadilika kwa kiasi kikubwa nakuona huenda nitatekwa tu. kuwa hapa hapanifai hata kidogo tena.
“..ennhee Aisha ikawaje sasa ni mambo gani hayo mawili aliokuwa amekuomba huyo Jerry”..
“..aliniweka wazi kuwa yeye hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba, amesumbuka sana kwa madaktari na mpaka kwa waganga wa kienyeji  lakini imeshindikana. Hivyo akaamua aoe na kuishi na mwanamke ambaye yuko sawa nayeye ambaye hana uwezo wa kuzaa ‘mgumba’. Basi akaoa lakini mtafaruku umekuja kwa wazazi wa pande zote mbili wanataka wajukuu.. kilichofanyika Jerry akaniomba kwanza nimtunzie siri na aibu hii kubwa ambayo amehangaika nayo kwa muda mrefu sana bila ya kuwa na mtoto. Pili akaniomba apandikize mbegu zake kwangu kutokea hospitalini ili nishike mimba nakumzalia.
“..hee.., halafu..?”
“..kama nitashika mimba atakuwa bega kwa bega na mimi mpaka nitakapojifungua. Atahakikisha amenijengea jumba kubwa nakuniwekewa kila kitu ndani nitakachokihitaji. Pia mkewe atamsafirisha nje ya nchi kwa siri siri bila ya ndugu kujua chochote na atakaporudi atakuta nimeshajifungua hivyo atamchukuwa mtoto nakumlea. Tulijaribu mbegu zake karibu mara tano lakini ikashindikana mimi kushika mimba kwa kutumia mbegu za Jerry. Kwa kuwa tayari nilishaingia tamaa ya hela na makazi kama alivyoniahidi Jerry. Nikapanga dili na dokta kisha nikasafiri mpaka Morogoro kwa mpenzi wangu Almeida akanipa ujauzito hivyo nikamsakizia Jerry kuwa tumeshafanikiwa kushika mimba. Jerry alifurahi sana kwa kuwa nilikuwa katika kipindi kigumu. Ilinibidi nisimamishe kwanza mambo yangu ya chuo kwa muda wa miezi tisa huku na ujauzito. Nikatafutiwa mfanyakazi wa ndani ambapo hata hivyo haikuwa ikipita siku bila Jerry kunipigia simu au kuniletea vitu mbalimbali vya kuniliwaza..”
“..kwa hiyo sasa huyo mtoto ukajifungua au ikawaje sasa..?”
“tina..? yani mtoto nilijifungua salama bonge la toto  mzuri kama huyo wa kwako. Hii nyumba na gari unavyoviona ameninunulia Jerry. Na mkewe ni rafiki yangu wa karibu sana na haipiti siku bila kunitembelea ama kunipigia simu na hivi nimeshamaliza chuo kabisa utamuona hapa kila siku..”
Mapigo yangu ya moyo yakaishiwa nguvu na kwa sasa yakawa kama yamepigwa ganzi ama kumwagiwa maji tena yale ya barafu ambayo hutoa kama moshi. Kichwa kilianza kunigonga huku nisielewe nianzie wapi. Sikuwa na hamu tena ya kukaa hapa japo ndio kwanza ilikuwa siku ya kwanza. Tukiwa bado kwenye maongezi na Aisha mara tukasikia sauti ya gari ikipiga honi huko nje. Hatujakaa sawa mara tena Simu ya Aisha ikaita, akapokea..
“..yeahh honey mambooo..!!! Ni wewe karibu namimi ndio kwanza nimemaliza chuo leo vipi upo peke yako ama..?”
“..sikuweza kutambua vizuri kuwa Aisha anaongea na nani zaidi yakuniaga kwa ishara huku akiniacha chumbani nakuelekea sebuleni..”
Mawazo mengi bado yaliendelea kunitawala ndani ya halmashauri ya ubongo wangu. Sikuweza kujitambua Tina mimi. Nilihisi kama ndoto. Nilivaa nguo kwa kutetemeka mithili ya mtu mwenye ukoma au yule anayeumwa malaria kali sana. Midomo yangu ilikuwa ikitetemeka kwa haraka haraka mithili ya maji yanapochemka katika sufuria. Nilibaki nimeduwaa peke yangu huku nikiwa sipati jibu wala ufafanuzi wa hili jambo. Nilichokifanya niliiinuka taaratibu kisha nikamweka mwanangu Adriani vizuri kitandani nakuanza kunyatanyata kuelekea sebuleni huku mwanangu Adrian nikimuacha akiwa amelala fofofo.  Niliendelea kunyata kimya kimya. Sauti za taratibu na za kimahaba kuashiria sebuleni kuna mtu na mume wake ndizo zilikuwa zikinivuta zaidi. Nilipokaribia nilifunua pazia la kuingilia sebuleni kwa utaratibu huku nikifumba jicho langu la upande wa kulia nakuliachia jicho la upande wa kushoto likifanya kazi yake ya kuangaza nakushuhudia tukio zima huku masikio yangu yakiwa sambamba na hilo tukio.
“..Jerry..?? Jerry..? oohh…!! Nooo…!!! Aisha noo..??”
Maskini Tina mie alikuwa ni Jerry katika himaya hii. Na kwasasa alionesha sura ya ukali huku akimuhadithia Aisha tukio zima nililomfanyia pale stendi miezi michache iliyopita. Alikuwa akimuomba sana Aisha msaada wa kunitafuta popote pale nilipo ili ampate mtoto wake. Jerry alikuwa akitoa machozi kama mtoto mdogo vile huku akimbembeleza Aisha wawe kitu kimoja kuhakikisha huyo mtoto anapatikana. Nikiwa bado nashuhudia Jerry akimbembeleza Aisha mara Aisha akainuka pale nakutoka huku akielekea sehemu ambapo nipo..
“..Jerry haiwezekani mwanagu wa damu yangu kabisa eti amchukue Tina anajua tulivyompata..?, embu subiri nakuja sasa hivi..?”
Aisha alionekana kuwa na hasira zaidi kwani aliinuka kwa hasira na kwa shari. Nilichomoka kwa haraka huku nikielekea chumbani kwangu kumuwahi mwanangu Adrian lakini kabla sijafika chumbani Aisha akawa tayari ameshaniona kwa mbali kidogo akaniita kwa sauti ya kupaza na ya ukali..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaa….??????????????”






*** Najua bado unatamani sana kujua kitakachompata Tina, hii sio ndoto ni ukweli kabisa, je unavyodhani ndio utakuwa mwisho wa **Play gal..? nini hatma ya Tina..?


*** kwanini mikosi haimuishi Tina kila kukicha..?


*** utamu ndio kwanza unazidi kunoga, chonde chonde usikubali kusimuliwa **Play gal ittakayofuata kwani ni nzuri zaidi ya hapa.  Jiandae kwa kumshuhudia tena Tina kilichompata ndani ya   ***Play gal – 61



***itaendelea>>>>>>>>>

Labels: