Saturday, August 11, 2012

Hatua 10 za Kuchagua Mchumba


                                                                                             

Kwanza niwasalimu wasomaji na wafuatiliaji wa blog hii yetu ya Bongomixx ambayo inaendelea kujitahidi katika kuelimisha na hata kukutabainisha mambo jinsi yalivyo sambamba na kukujuza ambavyo huyafahamu.
Kwa siku ya leo jumamosi nimependa niwaandalie jinsi yakumtambua mchumba mwema wa kuoa.
Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Suzzy aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.


Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.

Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.

Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.

Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.


Labels: ,

BLACK IS BEAUTIFUL

 
BRAZILIAN SUPERMODEL SAMIRA CARVALHO SPOTTED IN FUNKY GROOVES COLLECTION BY VILSCO ON THEIR AD CAMPAIGN
The Holland based fabric company Vlisco has just released its Funky Grooves collection. The ad campaign features super models Grace Bol and Samira Carvalho, but is it the sexy Brazilian model that steals the spotlight in the “Urban Allure” off shoot. Check out her fierce form, sophisticated angles and feminine grace as she glides through what Vlisco terms as “a collection of contrasts, with edgy street wear influences reinterpreted through a lens of pure glamour.”
For a 165 years, the Dutch company has been supplying the West and Central African market with “high-end and highly desired textiles, which have become part of the vibrant culture.” Currently Vlisco Group has four brands in its portfolio: Vlisco, Woodin, Uniwax and GTP. Design, Fashion, Creativity, Innovation and Quality are the overall brand values, values which are explicitly manifested by Caravlho in this shoot. Enjoy
 




























Labels:

Friday, August 10, 2012

BREAKING NEWS: AJALI TENA..

WATU zaidi ya 11 WAHOFIWA KUFA KATIKA AJALI iliotokea daraja la mto wami alfajili ya jana tarehe 10.
Watu zaidi ya 11 wanahofiwa kufa kufuatia ajali ya mabasi mawili ya abiria yaliyokuwa yakitokea Nairobi nchini Kenya kuja Dar es Salaam.Ajali hiyo inaelezwa kuwa imetokea maeneo ya Daraja la mto Wami alfajiri ya jana Mkoani Pwani. Wadau tunazidi kuzifuatilia taarifa hizi kwa ukaribu,tutazidi kutaarifiana kadiri ya taarifa zitakavyokuwa zinapatika,lakini pia si vibaya kwa mwenye taarifa kamili akatujuza hapa hapa bongomixx.

Labels:

MASTAA BONGO MOVIE WADAIWA KUJIUZA BBM



                                                                                                

BAADHI ya mastaa Bongo wanadaiwa kuwa na tabia ya kutumia mtandao wa simu wa BlackBerry Messenger ‘BBM’ vibaya ikiwa ni pamoja na kujiuza kwa wanaume, Ijumaa limebaini.
Utafiti uliofanywa na mapaparazi wetu umeonesha kuwa, wapo ambao wawapo vyumbani kwao hujipiga picha za utupu na kuzitupia kwenye mtandao huo kisha baada ya muda huzitoa.
Wakizungumzia tabia hiyo, baadhi ya wanaume wanaotumia BBM walikiri kukumbana na picha hizo za ajabu za mastaa huku zikiambatana na maneno ya kujitongozesha kwao.
“Huyu …(anataja jina la staa maarufu Bongo), juzi usiku mishale ya saa nane alianza kunitumia ‘sms’ kuniuliza kama niko macho. Nilipomjibu akaniambia kuna zawadi anataka kunipa, nilivyomkubalia akatupia picha yake akiwa kitandani mtupu.
“Hazikupita hata sekunde nyingi, kabla ‘sijai-download’ akaitoa kisha akaniuliza nimejisikiaje kumuona alivyo. Nilishangaa lakini nikamjibu kwa kifupi kuwa ana mvuto, basi kuanzia siku hiyo akawa ameniganda,” anasema kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Sule ambaye ni mfanyabiashara jijini Dar.
Msanii mwingine wa kiume aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema:
“Mbona huo ndiyo mchezo wao, yaani ukishamkubalia kuwa rafiki yao basi subiri vituko, kwa kifupi sasa hivi wengi wanajiuza kupitia BBM.”
Katika kupata ukweli juu ya habari hiyo, waandishi wetu walizungumza na baadhi ya mastaa wa Kibongo wanaotumia mtandao huo ambapo walikuwa na haya ya kusema:

JACQUELINE PATRICK
Modo huyo mwenye jina kubwa Bongo alifunguka: “Kwa upande wangu siwezi kukataa kuwa sijawahi kuweka picha kama hizo, mimi ni mpenzi sana wa picha na ninaupenda sana mwili wangu hivyo nikipiga picha ya aina yoyote lazima niitupie kwani ‘fansi’ wangu ndiyo wanaoweza kuniambia kama nimenenepa au nimekonda au kunisifia
“Suala la kutongoza wanaume naweza nikasema kuwa mimi siweki kwa sababu hiyo kwani marafiki zangu wote kwenye BBM wana wapenzi wao.”

ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
Mwigizaji huyo ambaye pia ni mwanamuziki alisema: “Mimi sijawahi kumtongoza mwanaume na siwezi kwa sababu mila za kwetu zinasema mwanaume ndiye anatakiwa kumtongoza mwanamke hivyo mwanamke anayemtongoza mwanaume anakosea kwani ataonekana wa bei rahisi sana.
Labda wenzangu wanaweza kufanya hivyo kupitia njia hiyo.”

MIRIAM JOLWA ‘JINI KABULA’
Mwigizaji huyo alifunguka: “Mimi nina mume wangu, nampenda sana na mara nyingi siingii BBM ila ninauzisha tu picha zangu kule lakini kuchati na watu siyo kivile na siwezi kumtongoza mwanaume kwa sababu wanaume wanaopatikana kwa njia hiyo siyo kabisa labda mastaa wenzangu, lakini mimi sijawahi kumtongoza mwanaume.”

RACHEL HAULE ‘RECHO’
Staa huyo wa filamu alisema: “Sijawahi kumtongoza mwanaume ila suala la kutongozwa na wanaume kwenye BBM ni la kawaida, inategemea na msimamo wa mtu. Najua BBM tumejiunga kwa ajili ya kujua matukio yanayotokea kwa haraka zaidi na siyo kwa ajili ya kujiuza.”

ISABELA MPANDA
Mwigizaji huyo alitiririka: “Katika orodha ya hao wanaojiuza kupitia mtandano huo, mimi simo. Nipo BBM ila sijawahi kumtongoza mtu wala kutupia za utupu.”
RUTH SUKA ‘MAINDA’
Mwigizaji huyo mkongwe alisema: “Ni kweli nimejiunga BBM lakini kwa sasa nipo ‘shouting’ nicheki baadaye.
Mastaa wengine waliotajwa kuwepo BBM nja na waigizaji Aunt Ezekiel, Irene Uwoya, Agnes Gerard ‘Masogange’ na wengineo.

Source: Global publishers

Labels: ,

TAFF YATOA TAMKO JUU YA MAHARAMIA WA FILAMU


                                                                                       


                                                                                
SHIRIKISHO la Filamu nchini(TAFF) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) pamoja Kampuni za usambazaji wa filamu na kazi za wasanii ‘wameapa’ kupambana na maharamia wote wa kazi hizo ili kulinda maslahi ya wasanii. Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam jana, umoja huo kwa pamoja ulisema umefika wakati tatizo la wizi wa kazi za wasanii lishughulikiwe kikamilifu ili kuzima mianya yote ambayo ni kero kwa muda mrefu. Rais wa Shirikisho hilo Simon Mwakifwamba, mbali na mikakati hiyo pia aliiomba Serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwasaidia wasanii kwa kupambana na maharamia hao aliodai kuwa wapo kila pembe ya nchi hii huku wakijiamini kwa kuendelea na kazi hiyo. “Umefika wakati kwa Serikali kusikia kilio hiki cha wasanii na kuweka mbinu kali zitakazosaidia kuokoa maisha ya wasanii wanaoendelea kuwa masikini kila kukicha kutokana na uwepo wa watu wachache wanaoiba kazi zao” “Tuna imani kuwa kama kazi za wasanii zitasimamiwa vizuri, tutaweza kuongeza pato la Taifa kwa kiwango kikubwa ikizingatiwa kuwa sanaa hii kwa sasa hapa nchini imeonyesha mafanikio isipokuwa kuna watu wachache ndiyo wananufaika nayo” alisema Mwakifwamba. Naye Mwenyekiti wa Bongomuvi Jacobo Steven ‘JB’ alisema sanaa inaweza kuwa na nafasi ya tatu kwa kuchangia pato la Taifa ukiacha pato linalochangiwa na sekta za madini maliasili pamoja na utalii. Alisema Serikali inapswa kuonyesha makali yake kwa kuwakamata wahusika wote wa wizi wa kazi hizo ili kuendeleza nguvu za wasanii wa hapa nchini walioamua kujitoa mughanga kufanya kazi zao.
Kwa upande wake Meneja usimamizi kutoka TRA Msafiri Ndimbo alisema Mamlaka hiyo imejipanga kudhibiti wizi wa kazi hizo kuanzia Januari Mwakani hasa baada ya Serikali kupitia Bunge lake kukubaliana kuweka mikakati ya kupamba na suala hilo.
Ambapo wasanii na wasambazaji wa kazi zao wameungana pamoja kwa ajili ya kuhakikisha kazi zao zinakwenda kwa haki ili wasanii na kazi zao

Labels: ,

NAMNA YA KUTAMBUA TABIA YA MTU..


Hakuna anayependa kusahihishwa, kugombana au kukemewa mbele za watu, hii ndiyo tabia ya watu wajeuri na walio na tabia za kitukutu. Mara nyingine hudhani wanapata sifa. Wako watu wa jinsi hii ambao hawawezi kukugombeza au (kukupa vidonge vyako) mkiwa wawili peke yenu, watangoja watu wengine wawepo ndiyo waanze kubwabwaja, chakufanya jiepushe nao.

Kwa kule kukimbiwa na marafiki, na kuwa pweke, huongeza tabia za kitukutu na kijeuri na hii huwafanya watu hawa kutambulika haraka na kiurahisi zaidi.

Zifuatazo ni alama zitakazokutambulisha mtu jeuri na mtukutu
a)Alama za kimaneno
Mara kwa mara hupendelea kusema maneno haya vinywani mwao.
Nakwambia bora unge…”
Wewe sichochote, silolote…”

Nakwambia, lazima u...”
Fanya vile ninavyokuambia mimi…”
Nataka u...”
Wewe endelea tu tutaona...”

Alama za kimwili
Hupendelea kusimama wima
Huwa wenye pozi kavu, ngumu (still and rigid pause)
Hupenda kukunja mikono

Hupenda kupayuka au kupigia wengine kelele
Hupenda kuwanyooshea wengine vidole.
Hupenda kuwazodoa wengine na vidole (hawezi kukuelekeza hadi kidole chake kikusukume)
Hupenda kupiga au kugonga meza na viti akizungumza

2. Watu wapole, waliotayari kukubali kushuka (Submissive)
Hawa ni watu wanaopenda kujitoa sadaka kwa ajili ya manufaa ya wengine. Kwa hali hii ni rahisi watu hawa kujikuta wanatumiwa vibaya na watu wengine hasa wale wajeuri na watukutu tulio waangalia awali.

Mara nyingi watu walio wapole na wanaokubali kushuka hupenda kuwatia moyo wengine wawe kama wao. Katika vizazi vilivyopita, wanawake walitegemewa zaidi kuwa watu wa kundi hili. Ni mabadiliko ya maisha na ya jamii ya leo ambayo yamemfanya hata mwanamke kuwa mjeuri na mshindani tofauti na jamii za awali.

Kwa upande mwingine mfumo wa maisha wa vizazi vya nyuma ulimweka chini mwanamke na kuzuia maendeleo yake hasa katika kujiendelezea vipawa alivyonavyo kwa vigezo tu kwamba yeye ni wakukubali chochote na wakati wowote sasa tunayaona mabadiliko kwa kiasi fulani.

Mara kwa mara watu wapole, na waliotayari kushuka wamekuwa wenye hisia za kinyonge na kutengwa, wakijihisi kutokuwa salama wakati mwingi. Kujijali, kujipenda na kujithamini kwa watu hawa siyo kwa kudumu, bali kunakuwa na nyakati za kuyumbayumba kutokana na mazingira. Hawa siyo watu wenye ujasiri ndani yao wenyewe na hata katika vile wavifanyavyo.

Mara mtu wa kundi hili anapokutana na mtu mjeuri na mtukutu, hofu na ujasiri wake hupungua sana, na anaweza kukubali kupingwa hata kama alikuwa ana haki. Kwa sababu mara nyingi watu wa jinsi hii wanajua kuwa kwa upole wao watu wengi wamekuwa wakiwatumia na kuwachezea, hii imewafanya wawe ni watu wenye vihasira vya mara kwa mara.

Kwa sababu wameunganishwa na hisia zao zaidi, ni rahisi wao kuzielezea hisia zao kwa mtu mwingine, hata kama hisia zao ni za kujutia kile walicho kifanya wenyewe.
Mara nyingi husikia amani kwa yale wanayofanya au kuyaamua.

Ingawa mara nyingine mambo huwaendela tofauti na walivyopanga, watu hawa hufahamu kuwa hawanabudi kukubali kosa au na kuwa tayari kujifunza kutokana na yale makosa.

Mambo yanapowaendea vema hupenda kujisifia na kujiona walio juu. Mara nyingine misimamo yao huwashawishi na kuwavutia wengine watazame kama wao, sio watu wanaopenda kuwatumia wengine vibaya (being manipulative) kama vile kuwasema au kuwasengenya wengine, hii huwafanya kuwa na wafuasi au washabiki wengi zaidi.

Kule kujiamini kwao na kuwa na ujasiri hupunguza sana msongo wa mawazo maishani mwao na hii huwasaidia kuelekeza nishati na nguvu zao zote katika kufikia malengo waliojiwekea.

Mara kwa mara sio watu wenye mabadiliko ya hisia (change of attitude) na hii hufanya mahusiano yao na wengine kuwa yasiyoyumba na mawasiliano baina yao na wengine huwa wazi, sio watu wakuficha wanachokiona, uwazi walionao kuwaweka huru.

Hujisikia vema hujipenda na kujithamini muda mwingi. Hujijengea hisia za usalama na imani kwa sababu ya mawasiliano bora walionayo na wale wanaowazunguka, hii pia husababishwa na wao kuelewa fika wajibu wao na wajibu wa wengine pia.

Ingawa wanaweza kuwa wabishi, lakini huheshimu misimamo ya wengine na kupenda ya kwao iheshimiwe pia na hii huwafanya kuwa na ushirika na wale wanaowazunguka. Mara nyingi ni wazuri katika kuwatia wengine moyo kujitahidi zaidi.

Alam za kuwatambua.
Alama za maneno
Nahisi……. Najisikia kuu……………”
Ningependa kuu…………”
Wewe unaonaje hapa/mawazo yako nini…………..”
Unadhani njia gani bora kulishuhulikia hili ………..”
Nafikiri………..”
Hembu tu……………..”

Alama za kimwili
Hupenda kuwa wima ila wenye pozi laini (relaxed stance)
Huangalia kijasiri na kuangalia usoni (kukodoa macho).
Huwa na hisia za upole, kujitawala na kujimiliki wenyewe
Kwa vyovyote vile, mara zote unapokutana na mtu mwenye tabia yeyote kati ya hizi tatu kumbuka una haki ya kufanya yafuatayo;

jifunze kuelezea hisia zako njema (usiogopoe au kuona aibu kwakuwa hutokuwa umejitendea haki)
Jifunze kuzielezea hisia zako mbaya au za hasira, kamwe usifunike. Mfano; “Sipendi kabisa unavyokula”
Jifunze kusema hapana, Mfano; “Hapana sitaweza kufika leo”

Toa wazo la kweli, usipake watu mafuta kwa mgongo wa chupa. Mfano; “Mimi siliafiki hilo jambo hata kidogo”
Kiri kuwa umekasirika, hasa pale ambapo haunabudi kukasirika.

Mf. “Kweli umeniudhi sana baada ya kusema hayo maneno”. Usitoe tabasamu la mamba tu, kutabasamu wakati ndani yako unahisi kuungua moto.

Labels: ,

HATIMAYE MALAWI YASALIMU AMRI KWA TANZANIA..

Siku chache baada ya Serikali ya Tanzania kupitia kwa waziri wake wa mambo ya nje Mh. Bernad Membe kuitaka Serikali ya Malawi kuondoa majeshi na kampuni zinazofanya utafiti wa gesi kwenye ziwa Nyasa ukanda wa Tanzania wakidai kuwa ziwa hilo ni la kwao lote wameanza kufanya hivyo na kuondoka taratibu ukanda huo. Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro alisema kuwa kwa sasa eneo hilo hali ni shwari kwani

makampuni, ndege na askari wa malawi waliokuwa wakiendesha shughuli zao kwenye eneo la Tanzania wametii amri na kuondoka kwenye eneo hilo hivyo wananchi wasiwe na shaka bali waendelee na kazi zao za kila siku kwenye ziwa hilo, Mbali na Waziri Membe, viongozi wengine waliozungumzia mgogoro huo na

kuitaka Malawi iache uchokozi ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika

Mashariki, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya

Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa.

Labels: ,

Thursday, August 9, 2012

Sifa 10 za Mpenzi wa Kweli




                                                                               
Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatizwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha mtoto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto zinazowakabili.
Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo ni hizi zifuatazo.

1.Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.

2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri

4.Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuwa mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa kikwazo cha maisha yako, atakulinda daima.

6. Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7. Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine, hafichi hisia zake mbele za watu, atakutetea na kukufanya wa kwanza.

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9.Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.

Labels:

SHOW MPYA ALIZOFANYA LINAH MAREKANI

Labels:

Wednesday, August 8, 2012

BIFU LA SINTAH NA AGNESS MASOGANGE LAINGIA PART II

 
 
Sintah akiwa katika pozi.
                                                                               
 
 
Mwigizaji  mwenye  mbwembwe nyingi  kutoka ndani ya  tasnia ya filamu Bongo Christina Manongi 'Sintah' amemtaka  video queen wa Bongo Agness Gerald Masogange   kufunga bakuli lake (kunyamza kimya) na kuacha  kumapakazia meneno machafu kwenye vyombo vya  habari.
Akizungumza na mwandishi wetu  mapema leo Sintah amesema kuwa amesikitishwa  sana na kitendo cha  Agness kumtaja yeye (Sintah) kuwa ndiye anahusika na kuisambaza kwenye mitandao video  inayomuonyesha Agness akiwa mtupu huku pia akionekana kufanaya  matendo kadhaa ya kingono.

"Nimemsikia na isitoshe kuna watu wengi wameniambia juu ya hilo la kunitukana na kunitaja redioni kuwa nahusika, mimi  sijui lolote awaulize marafiki zake  ambao mimi naamini ndiyo wanahusika kuzisambaza kwani hata kwenye BBM yangu ni wao ndiyo walinitumia namuomba afunge bakuli  lake la siivyo nitazitoa zaidi kwani ninazo pati wani mpaka 3 na zote nimetumiwa na marafiki zake ambao yeye anacheka nao lakini hajui kama ni ma-sn***ch" alisema Sintah

Akiendelea zaidi Sintah amefunguka kuwa  kamwe hajui lolote kuhusu kamera anayoisma Agnes, kwani binafasi hajawahi kukutana naye  na  alimjua  kupitia   nyimbo za wasanii wa Bongo Fleva kwa kuwa msichana huyo anapenda kuuza sura  na zaidi hajui hata  anapokaa.

Labels: ,

KAMPUNI YA STEPS, WASANII, WAKAMATA WEZI WA KAZI ZAO DAR ES SALAAM



Baadhi ya wasanii pamoja na askari polis wakiwa wamerizingira duka lililokuwa linauza kazi za wasanii feki 
BAADHI YA MIZIGO YA DVD MPYA KABISA ZILIZO FEKI ZIKIWA ZIMEKAMATWA LEO JANA JIJINI DAR ES SALAAM
Msanii wa filamu nchini Mohamed Nice 'Mtunisi' kushoto na Jacob Stevin 'JB' wakiwa katika duka ambalo lilikuwa linauza kazi zao ambazo ni feki ambapo walikamatwa kwa kushilikiana na Kampuni ya usambazaji ya Steps Entantainment ya jijini Dar es salaam
MSANII WA MUZIKI WA TAARABU, MZEE YUSUFU KUSHOTO, AKIANGALIA MOJA YA KAZI YAKE ILIYOKUWA FEKI ZILIZOKAMATWA NA WASANII WENYEWE KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA STEPS ENTANTAINMENT YA JIJINI DAR ES SALAAM JANA
MSANII MOHAMED NICE 'MTUNISI' AKIZUNGUMZA JINSI WALIVYOKAMATA MZIGO FEKI WA KAZI ZA WASANII MBALIMBALI KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA STEPS ENTATAINMET YA JIJINI DAR ES SALAAM INAYOSAMBAZA KAZI ZA WASANII NCHINI
Moja ya gari lililokuwa limejaa kazi feki za wasanii mbalimbali nchini zinazouzwa baada ya kurudufiwa kinyume cha sheria na kukosesha wasanii mapato mazuri.
MSANII KAPTEN RADO AKIKAGUA KAZI ZAKE MPYA AMBAPO KAZI YAKE IJULIKANAYO KAMA 'HATIANI' ILIYOINGIA MTAANI JANA ILIKUWA IMESHACHAKACHULIWA NA KUINGIZWA SOKONI
MSANII MOHAMED 'NICE' AKILIA KWA UCHUNGU BAADA YA KUKUTA KAZI ZAO ZILIZOKUWA ZIKIUZWA KATIKA MOJA YA DUKA MTAA WA MAGILA NA LIKOMA JANA

Labels: ,

NDOA YA WAKE WATATU YAIBUA MENGI..

Mwananume anayedaiwa kuwaoa wake watatu kwa mpiga.
                                                                             
Mwanamme mmoja huko jamhuri ya kidemokrasia ya kongo kafunga ndoa na wanawake watatu kwa mpigo siku moja kanisani. Tukio hilo limetokea wiki iliyopita ambapo pedeshee huyo aliamua kuwapeleka wake waote  watatu kwa mpigo kanisani na kuwafungisha ndoa kwa nia ya kuishi nao pamoja.

Labels:

NAIBU WAZIRI ABUDULLAH JUMA APATA AJALI MBAYA


Naibu Waziri wa Afrika Mashariki, Mhe. Abdullah J Abdallah, amenusuirika katika ajali ya gari leo jioni katika maeneo ya Tumbi – Kibaha wakati akitokea Bungeni Dodoma akielekea Dar.
Ndani ya gari alikuwa pamoja na mkewe na watoto wake ambao wote wamepata majeraha madogo, dereva wake ameumia zaidi na hivyo kulazimika kukimbizwa katika hospitali ya Tumbi.

Labels: ,

MESSAGE NZURI ZA MAPENZI

Kuna miezi 12 katika mwaka siku 30 katika mwezi�siku 7 katika wiki, masaa 24 katika siku dakika 60 katika saa 1 lakini wewe ni mmoja tu  maishani mwangu.
                                          ****
I asked God for a rose and He gave me a garden. I asked God for a drop of water and He gave me an ocean. I asked God for an angel and He gave me you!
                                         ****
Kuna vitu viwili zinavyoniamsha asubuhi na mapema: Alamu ya saa yangu na wewe
*****
I will walk with you side by side for only one condition: hide your wings every time we walk together because the whole world might know that you're my angel! 
****
Bongo zenye fikra kali huwa na mawazo, suluhu na sababu; ubongo wa kisayansi huwa na kanuni, nadharia na takwimu; wangu una wewe tu!
****
Do you take me to be your lawfully wedded text mate, in sickness or in health, through metering or not, till low bat do us part?
****
Penzi linaweza kuelezewa kwa namna nyingi. Namna moja niijuayo nikumtumia mapenzi hayo mtu asomaye meseji hii.
****
Each of us is an angel with one wing. The only way we could fly is to hold each other and share wings. So if you have trouble flying, I will always share mine with you.
****

Kama ningeweza kubadili herufi, ningeweka yangu na yako kuwa pamoja.
****
Minsan caring is better than loving. Minsan tea is better than coffee. Minsan smile is better than laughter. Pero nobody is better than you.
****
Umewekwa usiku ili tuweze tuukubali mchana, huzuni ili tuikubali furaha, ubaya ili tuukubali uzuri, wewe ili niyakunali mapenzi.

I don't want to say I miss you, though deep inside I do, coz I'm afraid you might see thru and know how much fear I have of losing someone like you.
****
Unaonekana kung�ara leo nilijuaje��.ni kwasababu unaonekana hivyo kila siku
****
You greeted me hi, I didn't reply. You gave me a sweet smile, I responded with a sigh. You showed me your love, you received a shrug. But when you bid goodbye I began to cry.
****
I have heard from the phone company, the water company, the electric company, but haven't heard from you. Too bad, it's your company I love the most.
****
Mapenzi ni nini? Wale wasiopenda huita majukumu, wale wanaoyachezea huita mchezo, wale wasiokuwa nayo huita ndoto, na wale wanaoelewa huyaita mwisho wa safari, na mimi, mwisho wangu ni wewe.
****
I've been wondering why you're not texting... Multiple choices: a. busy b. dilemma c. tired d. thrifty e. want me to miss you.
****
Love is something special, a treasure I want to find... To others, love is blind but for me, its not true, coz when I fell in love...I saw you.
****
Ni mapenzi gani yanayofanya simu yako ilie kila nitumapo meseji?
****
True love is hard to find, special one, one of a kind. I know because it appeared to me on a strange day I met you.
****
Kama mapenzi huweza kukimbiwa kwa kufumba macho yetu tu, basi nisingefunika macho kabisa. Sitaki sekunde ipite bila kukupenda wewe.
****
While you gave her flowers, you gave me thorns. While all she did was smile, all I did is mourn. While she was so happy, I felt so blue. Because while you loved her, I was loving you.
****
Nilikuwa nikifiria kwamba ndoto haziwezi kuwa kweli, lakini nilibadili mawazo yangu pale tu nilipokuona wewe.
****
Baadhi ya watu huzaliwa na vipaji. Huweza kufanya mambo mazuri kwa ujuzi wao, lakini hamna anayekufikia wewe, kwani ukinisogelea tu kila kitu huwa kizuri.
****
Can I say I love you today? If not, can I ask you again tomorrow? And the day after tomorrow? And the day after that? Coz I'll be loving you every single day of my life.
****

Labels:

EDWARD LOWASSA: TUPO TAYARI KUINGIA VITANI NA MALAWI NA TUMEJIPANGA VIZURI


KAMATI ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imesema Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo.

Akizungumza mjini Dodoma jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Edward Lowassa alisema kamati yake imeridhishwa na maandalizi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

“Tumepewa maelezo na jeshi letu na tumeridhika kuwa ikibidi kuingia vitani jeshi letu liko vizuri sana na limejipanga vizuri sana kwa uhakika, kiakili na kivifaa,” alisema Lowassa.

Kabla ya Lowassa kuzungumza na waandishi wa habari, alifanya kikao cha faragha kilichohusisha pia wajumbe wa kamati hiyo na makamanda wa JWTZ walipofika bungeni kutoa taarifa kwa kamati hiyo.

 
Hata hivyo, katika tamko hilo Lowassa alisema Tanzania inatarajia mgogoro huo utamalizika kwa njia za kidiplomasia kwa sababu Watanzania na Wamalawi ni ndugu wa muda mrefu.

“Ikibidi kuingia vitani jeshi letu liko vizuri sana na kama ilivyo ahadi yao (JWTZ), wako tayari kulinda mipaka ya nchi yetu hadi tone la mwisho. Tunasali sana tusifike hapo,” alisema Lowassa na kuongeza: “Tunategemea hatutafika huko, lakini kwa heshima ya nchi yetu kama ikibidi kufika huko (vitani) tutafika kulinda mipaka yetu”.

Mwenyekiti huyo ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu, alisema kama Tanzania itafikishwa mahali itabidi damu ya Watanzania imwagike, nchi iko tayari kulinda mipaka yake kwa nguvu.


Alisema kama itabidi kuingia vitani, itatumia umoja na mshikamano wa Watanzania wa mwaka 1978 wakati wa Vita na Uganda kulinda mipaka ili kulinda heshima ya nchi.

Alisema mwaka 1978 wakati Rais wa Uganda, Idd Amin na majeshi yake walipochukua sehemu ya Tanzania na kujitangazia ni mali yake, ilichukua hatua kumfukuza Amin.

“Alijitangazia sehemu ile ni mali ya Uganda hutegemei nchi ikae kimya, hutegemei Watanzania wanyamaze wakati nchi yao imetekwa, tulichukua hatua tukamfukuza hadi nchini kwake.”

 
Lowassa alisema Kamati ya Bunge inajua madhara ya kiuchumi yaliyotokana na Vita ya Idd Amin na kwamba vita yoyote ikipiganwa lazima kunakuwa na madhara ya kiuchumi.

Hata hivyo, alisema anaamini mgogoro huo hautafika huko na kusisitiza kuwa, lakini ikibidi JWTZ ni moja kati ya majeshi bora duniani na ni jeshi lililojiandaa vizuri kwa lolote.

 
“Wako tayari sisi ni moja kati ya jeshi lililojiandaa vizuri na jeshi bora duniani na la kujivunia. Tuko imara kiakili na kivifaa tena vya kisasa,” alisema Lowassa.

Alisema kamati yake inaunga mkono msimamo ulitolewa bungeni juzi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuhusu mgogoro huo na kwamba ndiyo kauli rasmi ya Serikali.

 
Juzi, Waziri Membe alizionya kampuni za kigeni za Malawi zilizoingia katika ardhi ya Tanzania eneo la Ziwa Nyasa kutafiti mafuta na gesi kusitisha mara moja.

Akiwasilisha makadirio ya wizara yake, Membe alisema upo ushahidi kuwa ndege tano za utafiti za Malawi ziliruka anga la Tanzania na kutua katika Ziwa Nyasa upande wa Tanzania.Membe alisema pamoja JWTZ kutoruhusu ndege hizo za Malawi kuingia na kutua eneo hilo la Ziwa Nyasa, bado ziliingia na kutua kinyume kabisa cha sheria za kimataifa.

“Wenzetu wa Malawi wanadai Ziwa Nyasa lote lipo Malawi na msingi wa madai yao ni mkataba wa Heligoland wa mwaka 1890 na sisi tunasema mpaka uko katikati ya Ziwa.”

Membe alisema hata mgogoro wa mpaka kati ya Cameroon na Nigeria ulitatuliwa na Mahakama Kuu ya Dunia kuwa mpaka baina ya nchi hizo mbili upite katikati ya Ziwa Chad.

Juzi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Patrick Kabambe alikaririwa na Redio Sauti ya Ujerumani akisema wataendelea na utafutaji mafuta licha ya onyo hilo la Tanzania.

Waziri huyo alisema ziwa hilo linaitwa Malawi na siyo Ziwa Nyasa na kwamba utafutaji wa mafuta na gesi utaendelea na hakuna wa kuwasimamisha. Alihoji, iweje Tanzania ishtuke sasa

Labels: ,

Tuesday, August 7, 2012

UNAJUA JINSI YA KUTENGENEZA BURGER


WATOTO WENGI SANA WANAPENDA KULA BURGER HATA WATUWAZIMA PIA HUPENDA KULA SIKU MOJA KATIKA CHAKULA CHA MCHANA WATENGENEZEE
FAMILIA WAFURAHI

Kwaujumla napenda sana burger ya kutengeneza nyumbani, na ninapenda kutengeneza mwenyewe au mke wangu lengo ni kuhakikisha viungo na mchanganyikowote unakua sawa. Kwakutmia recipe hii unaweza kutengeneza 8 -10 hamburgers Inategemea utaweka upana gani wa nyama yako.Baada ya kuandaa unaweza kuhifadhi mchanganyiko huo wa nyama kwenye freezer kwa matumizi ya baadae.
MAHITAJI

 1 kg nyama ya kusaga safi 
 240 gram kitunguu kilichokatwa katwa vipande vidogo 
 60 gram bread crumbs ( Unga wa mikate)
 1 kijiko cha chakula Worcestershire sauce
 2 cloves of garlic, peeled and minced
50 gram kitunguu swaumu
 5 gram chumvi
 5 gram pili pili manga
1 lettuce
1 kitunguu
2 nyanya fresh

Katika bakuli kubwa changanya nyama pamoja na kitunguu, bread crumbs, Worcestershire sauce na kitunguu swaumu kisha weka . Kisha changanya safi na gawa katika mafungu 8 au 10 kulingana na ukubwa unaopenda wewe.
JINSI YA KUPIKA

Unaweza ukakaanga kwenye kikaango au ukapika kwa moto wa 160 degrees katika oven. Chukua mkate wa burger kisha kata katika pande mbili kisha paka mayonnaise na tonato  ketchup kwenye mkate upande wa chini, ongezea lettuce, slice kitunguu na nyanya fresh na slice ya tango la kopo. Nyunyizia chumvi kidogo mpatie mlaji ikiwa yamoto


Labels:

JINSI YA KUPIKA BIRIYANI KWA KUTUMIA WALI WA BASMATI NA NYAMA YA KUKU, MBUZI AU NG'OMBE

                                                       MAHITAJI


1 kilo mchele wa basmati mrefu

1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.
1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)
1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana
240 gram ya Mafuta ya kupikia
240 gram ya samli au mafuta yeyote ya kupikia
2 maggi chicken soup cubes
3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari (turmeric powder)
3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (coriander powder)
2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa (ginger-garlic paste )
50 gram korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima
50 gram majani ya girigilani (fresh coriander leaves, washed and chopped)
8-12 mbegu za nzima ya hiriki (green cardamoms)
4 bay leaves ( sifahamu kiswahili chake)
15 mbegu nzima ya pili pili manga (whole black peppercorns)
30 gram majani mabichi ya minti ( mint leaves )
salt kulingana na ladha yako binafsi
Jinsi ya kuanda

Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)

Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, bay leaves, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.
Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.
Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.
Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, majani ya mint na korosho funika kwa dakika 10 picha inaonyesha hapo chini, kisha weka wali wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto,


Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva


muonekano wa majani ya girigirani wakati wa kukaangwa


 Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva ukakaangwa na vitungu na korosho


Nyama ya kuku iliokaangwa vizuri na viungo na nyanya ukapata mchanganyiko mzuri mzito




Muonekano halisi wa biriyani yako baada ya kuiva ikiwa imechanganyikana na nyama pia kumbuka kunamchuzi mzito na nyma ilibaki pembeni mlaji ataweza kujongezea kiasi apendacho.
Furahia chakula hiki pamoja na familia yako.

Labels: