Friday, August 10, 2012

MASTAA BONGO MOVIE WADAIWA KUJIUZA BBM



                                                                                                

BAADHI ya mastaa Bongo wanadaiwa kuwa na tabia ya kutumia mtandao wa simu wa BlackBerry Messenger ‘BBM’ vibaya ikiwa ni pamoja na kujiuza kwa wanaume, Ijumaa limebaini.
Utafiti uliofanywa na mapaparazi wetu umeonesha kuwa, wapo ambao wawapo vyumbani kwao hujipiga picha za utupu na kuzitupia kwenye mtandao huo kisha baada ya muda huzitoa.
Wakizungumzia tabia hiyo, baadhi ya wanaume wanaotumia BBM walikiri kukumbana na picha hizo za ajabu za mastaa huku zikiambatana na maneno ya kujitongozesha kwao.
“Huyu …(anataja jina la staa maarufu Bongo), juzi usiku mishale ya saa nane alianza kunitumia ‘sms’ kuniuliza kama niko macho. Nilipomjibu akaniambia kuna zawadi anataka kunipa, nilivyomkubalia akatupia picha yake akiwa kitandani mtupu.
“Hazikupita hata sekunde nyingi, kabla ‘sijai-download’ akaitoa kisha akaniuliza nimejisikiaje kumuona alivyo. Nilishangaa lakini nikamjibu kwa kifupi kuwa ana mvuto, basi kuanzia siku hiyo akawa ameniganda,” anasema kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Sule ambaye ni mfanyabiashara jijini Dar.
Msanii mwingine wa kiume aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema:
“Mbona huo ndiyo mchezo wao, yaani ukishamkubalia kuwa rafiki yao basi subiri vituko, kwa kifupi sasa hivi wengi wanajiuza kupitia BBM.”
Katika kupata ukweli juu ya habari hiyo, waandishi wetu walizungumza na baadhi ya mastaa wa Kibongo wanaotumia mtandao huo ambapo walikuwa na haya ya kusema:

JACQUELINE PATRICK
Modo huyo mwenye jina kubwa Bongo alifunguka: “Kwa upande wangu siwezi kukataa kuwa sijawahi kuweka picha kama hizo, mimi ni mpenzi sana wa picha na ninaupenda sana mwili wangu hivyo nikipiga picha ya aina yoyote lazima niitupie kwani ‘fansi’ wangu ndiyo wanaoweza kuniambia kama nimenenepa au nimekonda au kunisifia
“Suala la kutongoza wanaume naweza nikasema kuwa mimi siweki kwa sababu hiyo kwani marafiki zangu wote kwenye BBM wana wapenzi wao.”

ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
Mwigizaji huyo ambaye pia ni mwanamuziki alisema: “Mimi sijawahi kumtongoza mwanaume na siwezi kwa sababu mila za kwetu zinasema mwanaume ndiye anatakiwa kumtongoza mwanamke hivyo mwanamke anayemtongoza mwanaume anakosea kwani ataonekana wa bei rahisi sana.
Labda wenzangu wanaweza kufanya hivyo kupitia njia hiyo.”

MIRIAM JOLWA ‘JINI KABULA’
Mwigizaji huyo alifunguka: “Mimi nina mume wangu, nampenda sana na mara nyingi siingii BBM ila ninauzisha tu picha zangu kule lakini kuchati na watu siyo kivile na siwezi kumtongoza mwanaume kwa sababu wanaume wanaopatikana kwa njia hiyo siyo kabisa labda mastaa wenzangu, lakini mimi sijawahi kumtongoza mwanaume.”

RACHEL HAULE ‘RECHO’
Staa huyo wa filamu alisema: “Sijawahi kumtongoza mwanaume ila suala la kutongozwa na wanaume kwenye BBM ni la kawaida, inategemea na msimamo wa mtu. Najua BBM tumejiunga kwa ajili ya kujua matukio yanayotokea kwa haraka zaidi na siyo kwa ajili ya kujiuza.”

ISABELA MPANDA
Mwigizaji huyo alitiririka: “Katika orodha ya hao wanaojiuza kupitia mtandano huo, mimi simo. Nipo BBM ila sijawahi kumtongoza mtu wala kutupia za utupu.”
RUTH SUKA ‘MAINDA’
Mwigizaji huyo mkongwe alisema: “Ni kweli nimejiunga BBM lakini kwa sasa nipo ‘shouting’ nicheki baadaye.
Mastaa wengine waliotajwa kuwepo BBM nja na waigizaji Aunt Ezekiel, Irene Uwoya, Agnes Gerard ‘Masogange’ na wengineo.

Source: Global publishers

Labels: ,

TAFF YATOA TAMKO JUU YA MAHARAMIA WA FILAMU


                                                                                       


                                                                                
SHIRIKISHO la Filamu nchini(TAFF) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) pamoja Kampuni za usambazaji wa filamu na kazi za wasanii ‘wameapa’ kupambana na maharamia wote wa kazi hizo ili kulinda maslahi ya wasanii. Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam jana, umoja huo kwa pamoja ulisema umefika wakati tatizo la wizi wa kazi za wasanii lishughulikiwe kikamilifu ili kuzima mianya yote ambayo ni kero kwa muda mrefu. Rais wa Shirikisho hilo Simon Mwakifwamba, mbali na mikakati hiyo pia aliiomba Serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwasaidia wasanii kwa kupambana na maharamia hao aliodai kuwa wapo kila pembe ya nchi hii huku wakijiamini kwa kuendelea na kazi hiyo. “Umefika wakati kwa Serikali kusikia kilio hiki cha wasanii na kuweka mbinu kali zitakazosaidia kuokoa maisha ya wasanii wanaoendelea kuwa masikini kila kukicha kutokana na uwepo wa watu wachache wanaoiba kazi zao” “Tuna imani kuwa kama kazi za wasanii zitasimamiwa vizuri, tutaweza kuongeza pato la Taifa kwa kiwango kikubwa ikizingatiwa kuwa sanaa hii kwa sasa hapa nchini imeonyesha mafanikio isipokuwa kuna watu wachache ndiyo wananufaika nayo” alisema Mwakifwamba. Naye Mwenyekiti wa Bongomuvi Jacobo Steven ‘JB’ alisema sanaa inaweza kuwa na nafasi ya tatu kwa kuchangia pato la Taifa ukiacha pato linalochangiwa na sekta za madini maliasili pamoja na utalii. Alisema Serikali inapswa kuonyesha makali yake kwa kuwakamata wahusika wote wa wizi wa kazi hizo ili kuendeleza nguvu za wasanii wa hapa nchini walioamua kujitoa mughanga kufanya kazi zao.
Kwa upande wake Meneja usimamizi kutoka TRA Msafiri Ndimbo alisema Mamlaka hiyo imejipanga kudhibiti wizi wa kazi hizo kuanzia Januari Mwakani hasa baada ya Serikali kupitia Bunge lake kukubaliana kuweka mikakati ya kupamba na suala hilo.
Ambapo wasanii na wasambazaji wa kazi zao wameungana pamoja kwa ajili ya kuhakikisha kazi zao zinakwenda kwa haki ili wasanii na kazi zao

Labels: ,

Wednesday, August 8, 2012

KAMPUNI YA STEPS, WASANII, WAKAMATA WEZI WA KAZI ZAO DAR ES SALAAM



Baadhi ya wasanii pamoja na askari polis wakiwa wamerizingira duka lililokuwa linauza kazi za wasanii feki 
BAADHI YA MIZIGO YA DVD MPYA KABISA ZILIZO FEKI ZIKIWA ZIMEKAMATWA LEO JANA JIJINI DAR ES SALAAM
Msanii wa filamu nchini Mohamed Nice 'Mtunisi' kushoto na Jacob Stevin 'JB' wakiwa katika duka ambalo lilikuwa linauza kazi zao ambazo ni feki ambapo walikamatwa kwa kushilikiana na Kampuni ya usambazaji ya Steps Entantainment ya jijini Dar es salaam
MSANII WA MUZIKI WA TAARABU, MZEE YUSUFU KUSHOTO, AKIANGALIA MOJA YA KAZI YAKE ILIYOKUWA FEKI ZILIZOKAMATWA NA WASANII WENYEWE KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA STEPS ENTANTAINMENT YA JIJINI DAR ES SALAAM JANA
MSANII MOHAMED NICE 'MTUNISI' AKIZUNGUMZA JINSI WALIVYOKAMATA MZIGO FEKI WA KAZI ZA WASANII MBALIMBALI KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA STEPS ENTATAINMET YA JIJINI DAR ES SALAAM INAYOSAMBAZA KAZI ZA WASANII NCHINI
Moja ya gari lililokuwa limejaa kazi feki za wasanii mbalimbali nchini zinazouzwa baada ya kurudufiwa kinyume cha sheria na kukosesha wasanii mapato mazuri.
MSANII KAPTEN RADO AKIKAGUA KAZI ZAKE MPYA AMBAPO KAZI YAKE IJULIKANAYO KAMA 'HATIANI' ILIYOINGIA MTAANI JANA ILIKUWA IMESHACHAKACHULIWA NA KUINGIZWA SOKONI
MSANII MOHAMED 'NICE' AKILIA KWA UCHUNGU BAADA YA KUKUTA KAZI ZAO ZILIZOKUWA ZIKIUZWA KATIKA MOJA YA DUKA MTAA WA MAGILA NA LIKOMA JANA

Labels: ,

Tuesday, August 7, 2012

Wema na Diamond wanaumwa ugonjwa mmoja?


Wema Sepetu akichukua vipimo
Diamond alipokuwa hospitali baada ya kuugua ghafla
Pengine huu si muda wa kuendelea kuspeculate tena iwapo Wema Sepetu na Diamond wamerudiana. Kuna mambo mengi yanayoonesha dalili kuwa wapenzi hawa wa zamani wamerudiana. Hawajasema hadharani lakini picha za hivi karibuni zinaweka wazi. 

Kuanzia zile picha za Kigoma kwenye video ya Leka Dutigite na zingine. Lakini inaonekana kama vile Diamond na Wema Sepetu wanaumwa ugonjwa mmoja. 

Wiki iliyopita Diamond alionekana kwenye picha akiwa amelala kwenye kitanda cha wagonjwa na akichukuliwa vipimo na daktari. Na sasa kuna picha ya Wema akiwa kwenye kitanda hicho hicho na akichukuliwa vipimo vilevile kama Diamond. 

Daktari ni yule yule japo anaonekana akiwa na nguo tofauti. Swali ni je wapenzi hawa wanaumwa ugonjwa mmoja? Ama kuna kamchezo kaitwako 'Public Stunt' wanakacheza?

Labels: ,

BONGO MOVIE: Ney wa mitego naamin kabisa unatafuta jina lipande kupitia "Bongo Movie" tunaomba uwataje wahusika

Ney wa mitego akiwa katika pozi



            Msanii wa maarufu wa bongo movie nchini 'Divanesh aidan' kama anavyojulikana kwa jina la Nesh ambaye hivi sasa anatamba kwenye filamu mpya ya 'Glory of Ramadhan' aliyoshilikishwa na Ray. ameibuka juu nakumchana live' Mwanamuziki wa bongo flava nchini Ney wa mitego. Kitendo cha ney kuikashifu sanaa ya bongo movie nchini imechukizwa na wengi wana bongo movie akiwemo Nesh ambaye uvumilivu ulimshinda nakujikuta akimchana live' kupitia mtandao wa kijamii wa 'facebook alinukuliwa akisema.
         "Ney wa mitego naamin kabisa unatafuta jina lipande kupitia "Bongo Movie" tunaomba uwataje wahusika" Baada ya habari hizi kusikika Bongomixx iliamua kunyanyua waya nakumtafuta Ney mwenyewe aeleze lakini jitihada zilishindikana baada ya simu yake kuita muda mrefu bila kupokelewa.

Nesh 'kushoto akiwa na Ray
                                                             
                                            
                                                               
                                                                                                     

Labels: , ,

Mke: BABY MADAHA KANIPORA MUME WANGU..

                                    
Mke wa mwigizaji wa bongo movie 'Khadija kushoto. kulia ni Huyo mume akijirusha na Baby madaha
                                                            

MKE wa mwigizaji wa filamu Bongo, Slim Omar, Khadija Amir ‘Kay’  amemfungukia msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ kuwa amempora mume.

Akizungumza na mtandao huu  hivi karibuni nyumbani kwake, Mwananyamala jijini Dar, Khadija alidai kuwa alimwagwa na Slim huku akiwa mjamzito na kwenda kupiga kambi kwa Baby Madaha.


“Mimi nalia na Baby Madaha jamani. Amenipora mume wangu, Slim. Mbaya zaidi aliniacha nikiwa na ujauzito kama hivi mnavyonioa. Lakini sijali kwa sababu naamini kama sikupangiwa niishi na Slim hata nikifanya nini haitasaidia.


“Nashangaa sana kufanyiwa kitu kama hicho na mtu ambaye ni rafiki yangu wa siku nyingi, bora angefanya mwingine lakini si Baby Madaha,” alisema Khadija ambaye ni Miss Shinyanga 2009.


Baby Madaha anayelalamikiwa kwa ‘wizi’ wa mume, alipopatikana kwa njia ya simu alisema yeye hayupo tayari kuzungumzia mambo yasiyo na msingi zaidi ya kutafuta fedha.


“Slim kweli namjua, nafanya naye kazi. Juzi tu hapa nilikuwa nashuti naye wimbo wangu mpya, ghafla ndiyo huyo mwanamke (Khadija) akaanza kunitukana na kudai nimemuibia mumewe.


“Sasa kama anadai wameachana anachokitafuta tena ni nini? Si amuache Slim awe huru kutafuta mtu mwingine?” alisema Baby Madaha pasipo kuweka wazi kama wanatoka na mwanaume huyo au vipi.


Jitihada za kumpata Slim ili kufafanua juu ya msimamo wake kwa wanawake hao hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

Labels: , ,

Saturday, August 4, 2012

J.B ; BONGO MOVIE HAIWEZI KUFA KAMWE..


KUNA tetesi kuwa Klabu ya Bongo Movie inayoundwa na baadhi ya mastaa wa filamu Bongo, inaelekea kusambaratika huku mwenyekiti wao, Jacob Steven ‘JB’ akiibuka na kusema umoja huo hauwezi kufa ila unahitaji kuombewa.

Madai ya awali yalisema Bongo Movie inapumulia mashine ikiwa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi kutokana na kutokuwa na uongozi bora.

“Mimi naweza kusema kuwa Bongo Movie haiwezi kufa tena inahitaji kuombewa sana kwa sababu sasa hivi ukiwataka wasanii wa filamu unawapata kirahisi kuliko wale wa muziki, pia tunainua vipaji vya chipukizi, nadhani hao wanaosema tumesambaratika washindwe na walegee kabisa,” alisema Jb.



Mwenyekiti wa klabu ya Bongo Movie, Jacob Steven 'JB'
                                                                                 

Labels: ,

Monday, July 30, 2012

HEMED ATAMBA KUTEMBEA NA WANAWAKE 32..

Source: Bongo flava tz
Kwanza kwa kuanza ningependa kumshukuru Hemed Suleiman kwa kuwa mmoja kati ya wavaaji wazuri wa Single buttons ninazozitengeza... picha zote unaziona ni amevalishwa na Martin Kadinda..... turudi katika swala zima ambalo limenifanya kuandika Post hii.... Nilitaka kujua ni vijana wangapi watumiaji wazuri wa condoms hasa kwa vijana maarufu. Mtu wangu wa kwanza amekuwa Hemed Suleiman aliniambia: "we jamaa maswali gani hayo bana? mimi kondomu za nini? muda wote mimi nakwenda dry... akaongezea kuwa alikuwa katika mahusiano na msichana mmoja ambaye hajataka kumtaja na anasema kwa sasa wameachana imepita miezi 3... anasema aliwa kupima nae virusi vya ukimwi na walipojikuta wako safi wakaamua kujilipua kavu kavu....
Alinichosha na majibu yake ikanibidi nihamie katika swali la pili: ambapo nilimuuliza kama amewahi kuwa katika mahusiano na wasichana wa Kitanzania maarufu? 

                                           


SINA LA KUONGEZA HAPO.



HEMED: Marti Martin...... unauliza kengele kanisani??? unadhani kwanini naitwa Hemed PHD? nina taaluma ya kucheza na mioyo ya mabinti hawa wakibongo.... ila tatizo hawanivutii huwa napita tu kwakuwa nina hamu na wakati huo au ninakuwa sipo katika mahusiano na mtu yoyote....

MIMI: Duuh kwahiyo ushampitia nani hii..........?? na nanihiiii........??
HEMED: hilo sio swali... mpaka sasa nishawapitia 32... kwahiyo kuhusu majina katafute mwenyewe huko mtaani mbona stori zipo??

                                                         
                                                           

Labels: , ,

Tuesday, July 24, 2012

HIVI NDIVYO MH: ZITO ZUBERI KABWE ANAVYODAIWA KUREJESHA PENZI LA DIAMOND NA WEMA SEPETU

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ametajwa kuwa kichocheo cha kurejea kwa penzi la vijana wenye umaarufu mkubwa nchini kwa sasa, Nasibu Abdu Juma ‘Diamond’ na Wema Isaac Sepetu.

Uwazi, lina mkanda wa video, unaowaonesha Diamond na Wema pamoja kwa mara ya kwanza, baada ya muda mrefu wa kutupiana maneno mengi ya kashfa, huku kila upande ukimshusha hadhi mwenzake.
Diamond na Wema, walinaswa kwenye Tamasha la Kigoma All Stars, lililoandaliwa na Zitto kisha kufanyika Julai 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
Shukurani kwa Zitto, kwani kupitia tamasha hilo, Diamond na Wema, waliweza kudhihirisha kwa kila mtu kwamba uhusiano wao sasa umerejea upya kwa kuambatana kimahaba ndani ya Mkoa wa Kigoma.

SAFARI ILIVYOKUWA TAMU
Watu wengi wakijua kwamba kuna uhasama mkubwa kati ya Wema na Diamond, Julai 17, mwaka huu, ilikuwa ni mshangao wa aina yake kwa waliokuwepo Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma, baada ya vijana hao kushuka wakiwa wameongozana.

Diamond akiwa amevaa shati jekundu na tai nyeusi, chini akiondokea suruali ya jeans rangi ya bluu iliyopaushwa kimodo, huku Wema akitokelezea kwa koti la rangi ya maziwa, ndani blauzi nyeusi, halafu wote wameyaficha macho yao kwa miwani nyeusi, waliwaka vilivyo ndani ya Ujiji, Kigoma.
Baada ya kuwasili Kigoma, Wema na Diamond walielekea Hoteli ya Tanganyika Beach (ipo ufukweni mwa Ziwa Tanganyika) ambako walipata pumziko walilohitaji kabla ya nyota huyo wa wimbo wa Mbagala, hajaelekea Uwanja wa Lake Tanganyika kwenye Tamasha la Kigoma All Stars a.k.a Leka Dutigite.

WEMA ALIFUATA NINI KIGOMA?
Minong’ono ilitawala kila kona ya Mkoa wa Kigoma kwamba Wema amekwenda kuwakilisha Leka Dutigite, hivyo wakataraji kumuona Uwanja wa Lake Tanganyika, akitoa sapoti yake kwenye tamasha hilo.
Wapo ambao waliacha shughuli zao kwa ajili ya kwenda kumuona Wema tu uwanjani lakini waliambulia patupu, kwani mrembo huyo hakuonekana kabisa.
Kutokana na hali hiyo, wale waliovumisha stori kwamba Wema amekwenda Kigoma a.k.a Lwama, walionekana wazushi wasiofaa kusikilizwa, bila kujua kwamba mtoto alijificha ndani ya Hoteli ya Lake Tanganyika Beach.

HAKIKA WANAPENDANA
Kama ukaribu wao ulisababishwa na tamasha lililoandaliwa na Zitto peke yake, basi wangekuwa na muonekano ‘feki’ sehemu chache wanazopita lakini kinyume chake wao walithibitisha wanapendana haswaa!

Diamond, alishindwa kujichanganya na wasanii wenzake aliokuwa nao kwenye shoo ya Kigoma kama akina Said Juma ‘Chegge’, Peter Msechu, Banana Zorro, Mwasiti Almasi na wengineo, badala yake muda mwingi aliutumia kuwa umbali wa mita sifuri kutoka alipo Wema.
‘Mtundu’ wa nyimbo mbili mpaka sasa, Nai Nai na Baadaye, Omar Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, ndiye pekee aliyekuwa jirani na vijana hao maarufu, walioamua kurejesha penzi lao kupitia mwavuli wa shoo hiyo.

Kwa upande mwingine, ni kama vile waliamua kwenda kufanya tambiko nyumbani asili kwa mume mtarajiwa, yaani Diamond kwa sababu chimbuko la Wema ni Mkoa wa Tabora, japo baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu, amejichimbia Zanzibar kwa miaka mingi.
Mtu mmoja, mwenye hulka ya kutopitwa na mambo, akamueleza ripota wetu kuwa Julai 18, wasanii hao walikwenda Hifadhi za Gombe na Mahale, mkoani humo lakini jioni yake, Diamond aliongozana na Wema mpaka kwa babu yake, eneo la Ujiji Posta, mkoani humo ambako walisomewa dua na Babu Nasibu.

RAHA NDANI YA TILAPIA HOTEL
Safari ya furaha kwa Wema na Diamond, ilihamia ndani ya Jiji la Miamba ya Mawe, Mwanza ‘Rocky City’ kwenye Hoteli ya Tilapia, iliyopo ufukweni mwa Ziwa Victoria, eneo la Capri Point, hiyo ikiwa Julai 19, 2012.

Habari zinapasha kuwa wawili hao, walipumzika kwenye hoteli hiyo kwa muda mfupi, wakati wanasubiri saa ya ndege yao ya kuwatoa Mwanza hadi Dar es Salaam ifike.

Ndege waliyopanda Diamond na Wema kutoka Kigoma, ilitua Mwanza saa 9:30 alasiri, hivyo kuanzia muda huo, waliutumia Tilapia Hotel mpaka saa 2:30 usiku, wakaripoti Uwanja wa Ndege wa Jiji la Miamba ya Mawe, kabla ya saa 3:50 usiku, usafiri huo wa anga, uliitupa mkono ardhi ya Mwanza mpaka Dar es Salaam.

AIR PORT DAR ES SALAAM
Mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra Sammi’, alionekana Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, kuanzia saa 4:45 usiku (Julai 19), hivyo kwa jicho la ripota wetu, ikawa wazi kwamba amekwenda hapo kumpokea mwanaye kipenzi, Diamond ‘Sukari ya Warembo’.

Kutokana na safari hiyo kuwa mguu wa Diamond uliambatana na wa Wema, kwenda kwenye shoo ya kutoa shukurani nyumbani kwao Kigoma, ni wazi Mama Nasibu (Mama Diamond) alikuwa pale pia kwa minajili ya kumlaki mkwe a.k.a Mka Mwana.

PW 415 YAWASILI DAR
Diamond na Wema, walipanda ndege ya Kampuni ya Precision Air, PW415 na ilipotimia saa 5:30 usiku, ilitangazwa kuwa ndiyo inawasili kwenye uwanja huo wa ndege wenye jina la muasisi wa taifa huru la Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ‘Baba wa Taifa’.
Milango ya saa 5:52, Diamond na Wema, walipita kwenye mlango wa wanaowasili (arrivals gate), wakiwa sambamba na Ommy Dimpoz, walipokelewa na Mama Nasibu hadi sehemu ya maegesho ya magari uwanjani hapo.

Timu nzima, ilijipakia kwenye gari la Diamond aina Toyota Land Cruiser Prado, rangi ya fedha, wakatoweka eneo la uwanja huo.

DIAMOND KWA WASIWASI
Saa 6:14 usiku (Julai 20), Diamond alimpigia simu ripota wetu, eti akahoji kilichompeleka uwanja wa ndege. Mahojiano yalikuwa hivi;

DIAMOND: Kiongozi nilikuona Air Port, pale ulikuwa unafanya nini?

RIPOTA: Aah, kumbe uliniona? Mlivyojikausha nikadhani hamkuniona. Kuna mzigo
wangu nilikuwa naufuatilia pale.

DIAMOND: Mzigo wapi? Naomba uniambie ukweli.

RIPOTA: Acha hizo dogo, unafikiri mimi nilikufuata wewe? Tena ningejua unafika leo, halafu ujio wenyewe ni huo, ningetega kamera zangu na tuwapige picha za kutosha.

DIAMOND: Aah, usifanye hivyo kiongozi.
Baada ya mazungumzo hayo, Diamond kila alipopigiwa simu hakupokea mpaka gazeti hili linanyanyuka kwenda kiwandani.

UFAFANUZI WA WEMA
Wema alipopigiwa simu na ripota wetu, alijibu kuwa yeye na Diamond hawajarudisha mapenzi, isipokuwa hivi sasa wako karibu kama marafiki wazuri kwa ajili ya kusaidiana mambo mbalimbali.
“Kusema ukweli kwa sasa sijafikiria kurejesha mapenzi na Diamond ila tupo karibu kama marafiki,” alisema Wema.

ZITTO NAYE
Jitihada za kumpata Zitto aweze kuzungumzia kurejea kwa penzi la Wema na Diamond kwenye tamasha aliloliandaa, hazikuzaa matunda. Muda wote naibu huyo wa Kambi ya Upinzania Bungeni, simu yake ilikuwa imezimwa.

WANANCHI WAMPONGEZA
Fununu kuwa Wema na Diamond wamerudiana zilivuma kwa kasi ndani ya mitandao ya kijamii na maoni ya wengi yakaelekeza pongezi kwa Zitto, kwani kabla ya hapo, mastaa hao walikuwa na uhasama mkubwa.

UNAKUMBUKA?
Malumbano yao kwenye vyombo vya habari? Diamond alipomfedhehesha Wema baada ya kukataa kupokea fedha zake alizomtuza kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam Machi mwaka huu? Je, kauli nzito za Mama Wema, Mariam Sepetu kwamba Diamond ni kijana mbaya na hafai?

JIULIZE SASA
Mpaka hapo bado unabisha kwamba mapenzi ni upofu? Unaendelea kukataa kwamba mapenzi hayaulizwi kwa nini? Diamond alipoachana Wema, alitua kwa Miss Tanzania namba mbili 2006-07, Jokate Mwegelo, je, penzi lao limeyeyuka au bado lipo kwa sura gani?


Labels: , , ,

Thursday, July 19, 2012

SASA NI ZAMU YA JB NA MAJUTO NDANI YA MUVI MPYA YANAKWENDA KWA MWANANGU..

King majuto aliyekaa akiwa na Jb huyu aliyesimama..












Sikuzote wapenzi wa filamu za bongo walikuwa wanahamu sana kuona Jb akiigiza na Majuto kwenye movi moja. Kwa kulithibitisha hilo bila kuwaacha wapenzi na dukuduku. Wasanii maarufu na wanaoongoza katika soko la filamu hapa bongo Jacob Stephen ama JB na yule nguli namba moja wakuchekesha hapa bongo AMRI ATHUMANI ama king majuto hivi karibuni wameibuka na movi moja kali inayokwenda kwa jina la NAKWENDA KWA MWANANGU. akizungumzia juu ya muvi hiyo, Jb alisema kuwa ameamua kubadilika nakutengeneza seriously comedy. Mbali na muvi hiyo pia Jb na Majuto wanatarajia kuelekea Mwanza kwa ajili ya uzinduzi huo tarehe 30 ya mwezi huu wa 7.

Labels: ,