Friday, August 3, 2012

HATIMAYE AMINI NA LINAH KURUDIANA..

                         
MSANII wa muziki wa kizazi kipya bongo, Amini Mwinyimkuu ‘Amini’, amedai kuwa anatarajia kutoa ngoma mpya ambayo atamshirikisha mpenzi wake wa zamani Linah, ingawa bado ngoma hajaipa jina.

Amini na Linah walikuwa wapenzi walioshibana lakini walikuja kuachana kwa amani na upendo, na sababu kubwa za kutengana kwao hakuna anayejua zaidi ya wao wenyewe.

Akizungumza na Bongo Mixx, Amini ambaye kwa sasa yuko bize na ngoma hiyo ili iwe ya kimataifa zaidi, alidai kuwa kutoka na mawazo ya watu kuwa yenye ana chuki na Linah, sasa ameamua kumshirikisha katika ngoma yake ili kuweka wazi na kufuta kauli za watu wenye nia mbaya.

Wakati huo huo Bongo Mixx ilimvutia Linah waya, nakudai kuwa naye alidai kuwa ameamua kufanya ngoma moja na Amini, kwani wao ni wasanii na wanahaki ya kushirikiana ingawa anaamini kuwa kuna watu baadhi ambao wanaamini wao bado ni wapenzi wakati ishu hiyo yamesha isha zamani.
                                     

Labels: , , ,

WEMA SEPETU “NAYAFANANISHA MAPENZI YANGU NA DIAMOND KAMA YA RIHANNA NA CHRIS BROWN…!!”


Jokate (kushoto), Diamond (katikati,) Wema(kulia)
                                                                   
                                                              
MSANII anayeongoza kwa ku-make headlines kwenye vyombo vya habari kila kukicha Wema Sepetu, amedai kuwa mahusiano yake yeye na mpenzi wake Nasseb Abdul ‘Diamond’, ni kama ya nyota wa marekani Rihanna na Chris Brown, huku akiamini kuwa kila kitu wanachokifanya kinakuwa kinafanana.

Wiki iliyopita Rihanna na Chris Brown, walioneka kwa nyakati tofauti huko St. Tropez, France wakila bata na kujiachia, ambapo hiyo pia imetokea kwa Wema na Diamond ambapo nao walionekana pamoja pande za Kigoma, Diamond alipoenda kwenye ziara ya Kigoma all stars inayoshirikisha wasanii wanaotokea mkoa wa kigoma.


Wema akiongea na Bongomixx alidai kuwa hakuna mtu anayeweza kumfanya ashindwe kula bata na mpenzi wake huo kwani anaamini kwa kufanya hivyo ndiyo njia moja wapo ya kuwakata vilimi wale wanaozungumza mabaya juu ya mapenzi yao.


Hata hivyo mwandishi wa habari hizi, alitaka kujua mipango yao ya baadaye juu ya mapenzi yao ambapo alidai kuwa juu ya hilo hawezi kuzungumzia kwani ni miezi kadhaa walikuwa katika matatizo hivyo bado wanakula bata na watakapofikia maamuzi ya kuvishana tena pete watafanya hivyo.


“Mapenzi yetu hayana matatizo kwani wanadamu kutofautiana hiyo ni hali ya kawaida, hivyo sioni kama kuna haja ya kuongea sana, na kitendo cha sisi kuonekana pamoja sehemu za bata kuna watu inawauma na sisi hatujali kwani kila mtu ana maisha yake,” alisema Wema.


Mbali na ishu hiyo pia, mwandishi alitaka kujua tena itakuwaje kwa upande wa Jokate, alijibu kwa upande wake hamuoni kama ni mtu wa maana kwani mapenzi yake hakuna wa kukatisha ingawa anaamini Jokate ni mtoto mdogo sana kwake.
Wana BongoMixx habari ndio hiyo, kumbe hata Bongo kama mamtoni..?

Labels: , ,

Monday, July 30, 2012

HEMED ATAMBA KUTEMBEA NA WANAWAKE 32..

Source: Bongo flava tz
Kwanza kwa kuanza ningependa kumshukuru Hemed Suleiman kwa kuwa mmoja kati ya wavaaji wazuri wa Single buttons ninazozitengeza... picha zote unaziona ni amevalishwa na Martin Kadinda..... turudi katika swala zima ambalo limenifanya kuandika Post hii.... Nilitaka kujua ni vijana wangapi watumiaji wazuri wa condoms hasa kwa vijana maarufu. Mtu wangu wa kwanza amekuwa Hemed Suleiman aliniambia: "we jamaa maswali gani hayo bana? mimi kondomu za nini? muda wote mimi nakwenda dry... akaongezea kuwa alikuwa katika mahusiano na msichana mmoja ambaye hajataka kumtaja na anasema kwa sasa wameachana imepita miezi 3... anasema aliwa kupima nae virusi vya ukimwi na walipojikuta wako safi wakaamua kujilipua kavu kavu....
Alinichosha na majibu yake ikanibidi nihamie katika swali la pili: ambapo nilimuuliza kama amewahi kuwa katika mahusiano na wasichana wa Kitanzania maarufu? 

                                           


SINA LA KUONGEZA HAPO.



HEMED: Marti Martin...... unauliza kengele kanisani??? unadhani kwanini naitwa Hemed PHD? nina taaluma ya kucheza na mioyo ya mabinti hawa wakibongo.... ila tatizo hawanivutii huwa napita tu kwakuwa nina hamu na wakati huo au ninakuwa sipo katika mahusiano na mtu yoyote....

MIMI: Duuh kwahiyo ushampitia nani hii..........?? na nanihiiii........??
HEMED: hilo sio swali... mpaka sasa nishawapitia 32... kwahiyo kuhusu majina katafute mwenyewe huko mtaani mbona stori zipo??

                                                         
                                                           

Labels: , ,

Tuesday, July 24, 2012

HIVI NDIVYO MH: ZITO ZUBERI KABWE ANAVYODAIWA KUREJESHA PENZI LA DIAMOND NA WEMA SEPETU

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ametajwa kuwa kichocheo cha kurejea kwa penzi la vijana wenye umaarufu mkubwa nchini kwa sasa, Nasibu Abdu Juma ‘Diamond’ na Wema Isaac Sepetu.

Uwazi, lina mkanda wa video, unaowaonesha Diamond na Wema pamoja kwa mara ya kwanza, baada ya muda mrefu wa kutupiana maneno mengi ya kashfa, huku kila upande ukimshusha hadhi mwenzake.
Diamond na Wema, walinaswa kwenye Tamasha la Kigoma All Stars, lililoandaliwa na Zitto kisha kufanyika Julai 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
Shukurani kwa Zitto, kwani kupitia tamasha hilo, Diamond na Wema, waliweza kudhihirisha kwa kila mtu kwamba uhusiano wao sasa umerejea upya kwa kuambatana kimahaba ndani ya Mkoa wa Kigoma.

SAFARI ILIVYOKUWA TAMU
Watu wengi wakijua kwamba kuna uhasama mkubwa kati ya Wema na Diamond, Julai 17, mwaka huu, ilikuwa ni mshangao wa aina yake kwa waliokuwepo Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma, baada ya vijana hao kushuka wakiwa wameongozana.

Diamond akiwa amevaa shati jekundu na tai nyeusi, chini akiondokea suruali ya jeans rangi ya bluu iliyopaushwa kimodo, huku Wema akitokelezea kwa koti la rangi ya maziwa, ndani blauzi nyeusi, halafu wote wameyaficha macho yao kwa miwani nyeusi, waliwaka vilivyo ndani ya Ujiji, Kigoma.
Baada ya kuwasili Kigoma, Wema na Diamond walielekea Hoteli ya Tanganyika Beach (ipo ufukweni mwa Ziwa Tanganyika) ambako walipata pumziko walilohitaji kabla ya nyota huyo wa wimbo wa Mbagala, hajaelekea Uwanja wa Lake Tanganyika kwenye Tamasha la Kigoma All Stars a.k.a Leka Dutigite.

WEMA ALIFUATA NINI KIGOMA?
Minong’ono ilitawala kila kona ya Mkoa wa Kigoma kwamba Wema amekwenda kuwakilisha Leka Dutigite, hivyo wakataraji kumuona Uwanja wa Lake Tanganyika, akitoa sapoti yake kwenye tamasha hilo.
Wapo ambao waliacha shughuli zao kwa ajili ya kwenda kumuona Wema tu uwanjani lakini waliambulia patupu, kwani mrembo huyo hakuonekana kabisa.
Kutokana na hali hiyo, wale waliovumisha stori kwamba Wema amekwenda Kigoma a.k.a Lwama, walionekana wazushi wasiofaa kusikilizwa, bila kujua kwamba mtoto alijificha ndani ya Hoteli ya Lake Tanganyika Beach.

HAKIKA WANAPENDANA
Kama ukaribu wao ulisababishwa na tamasha lililoandaliwa na Zitto peke yake, basi wangekuwa na muonekano ‘feki’ sehemu chache wanazopita lakini kinyume chake wao walithibitisha wanapendana haswaa!

Diamond, alishindwa kujichanganya na wasanii wenzake aliokuwa nao kwenye shoo ya Kigoma kama akina Said Juma ‘Chegge’, Peter Msechu, Banana Zorro, Mwasiti Almasi na wengineo, badala yake muda mwingi aliutumia kuwa umbali wa mita sifuri kutoka alipo Wema.
‘Mtundu’ wa nyimbo mbili mpaka sasa, Nai Nai na Baadaye, Omar Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, ndiye pekee aliyekuwa jirani na vijana hao maarufu, walioamua kurejesha penzi lao kupitia mwavuli wa shoo hiyo.

Kwa upande mwingine, ni kama vile waliamua kwenda kufanya tambiko nyumbani asili kwa mume mtarajiwa, yaani Diamond kwa sababu chimbuko la Wema ni Mkoa wa Tabora, japo baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu, amejichimbia Zanzibar kwa miaka mingi.
Mtu mmoja, mwenye hulka ya kutopitwa na mambo, akamueleza ripota wetu kuwa Julai 18, wasanii hao walikwenda Hifadhi za Gombe na Mahale, mkoani humo lakini jioni yake, Diamond aliongozana na Wema mpaka kwa babu yake, eneo la Ujiji Posta, mkoani humo ambako walisomewa dua na Babu Nasibu.

RAHA NDANI YA TILAPIA HOTEL
Safari ya furaha kwa Wema na Diamond, ilihamia ndani ya Jiji la Miamba ya Mawe, Mwanza ‘Rocky City’ kwenye Hoteli ya Tilapia, iliyopo ufukweni mwa Ziwa Victoria, eneo la Capri Point, hiyo ikiwa Julai 19, 2012.

Habari zinapasha kuwa wawili hao, walipumzika kwenye hoteli hiyo kwa muda mfupi, wakati wanasubiri saa ya ndege yao ya kuwatoa Mwanza hadi Dar es Salaam ifike.

Ndege waliyopanda Diamond na Wema kutoka Kigoma, ilitua Mwanza saa 9:30 alasiri, hivyo kuanzia muda huo, waliutumia Tilapia Hotel mpaka saa 2:30 usiku, wakaripoti Uwanja wa Ndege wa Jiji la Miamba ya Mawe, kabla ya saa 3:50 usiku, usafiri huo wa anga, uliitupa mkono ardhi ya Mwanza mpaka Dar es Salaam.

AIR PORT DAR ES SALAAM
Mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra Sammi’, alionekana Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, kuanzia saa 4:45 usiku (Julai 19), hivyo kwa jicho la ripota wetu, ikawa wazi kwamba amekwenda hapo kumpokea mwanaye kipenzi, Diamond ‘Sukari ya Warembo’.

Kutokana na safari hiyo kuwa mguu wa Diamond uliambatana na wa Wema, kwenda kwenye shoo ya kutoa shukurani nyumbani kwao Kigoma, ni wazi Mama Nasibu (Mama Diamond) alikuwa pale pia kwa minajili ya kumlaki mkwe a.k.a Mka Mwana.

PW 415 YAWASILI DAR
Diamond na Wema, walipanda ndege ya Kampuni ya Precision Air, PW415 na ilipotimia saa 5:30 usiku, ilitangazwa kuwa ndiyo inawasili kwenye uwanja huo wa ndege wenye jina la muasisi wa taifa huru la Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ‘Baba wa Taifa’.
Milango ya saa 5:52, Diamond na Wema, walipita kwenye mlango wa wanaowasili (arrivals gate), wakiwa sambamba na Ommy Dimpoz, walipokelewa na Mama Nasibu hadi sehemu ya maegesho ya magari uwanjani hapo.

Timu nzima, ilijipakia kwenye gari la Diamond aina Toyota Land Cruiser Prado, rangi ya fedha, wakatoweka eneo la uwanja huo.

DIAMOND KWA WASIWASI
Saa 6:14 usiku (Julai 20), Diamond alimpigia simu ripota wetu, eti akahoji kilichompeleka uwanja wa ndege. Mahojiano yalikuwa hivi;

DIAMOND: Kiongozi nilikuona Air Port, pale ulikuwa unafanya nini?

RIPOTA: Aah, kumbe uliniona? Mlivyojikausha nikadhani hamkuniona. Kuna mzigo
wangu nilikuwa naufuatilia pale.

DIAMOND: Mzigo wapi? Naomba uniambie ukweli.

RIPOTA: Acha hizo dogo, unafikiri mimi nilikufuata wewe? Tena ningejua unafika leo, halafu ujio wenyewe ni huo, ningetega kamera zangu na tuwapige picha za kutosha.

DIAMOND: Aah, usifanye hivyo kiongozi.
Baada ya mazungumzo hayo, Diamond kila alipopigiwa simu hakupokea mpaka gazeti hili linanyanyuka kwenda kiwandani.

UFAFANUZI WA WEMA
Wema alipopigiwa simu na ripota wetu, alijibu kuwa yeye na Diamond hawajarudisha mapenzi, isipokuwa hivi sasa wako karibu kama marafiki wazuri kwa ajili ya kusaidiana mambo mbalimbali.
“Kusema ukweli kwa sasa sijafikiria kurejesha mapenzi na Diamond ila tupo karibu kama marafiki,” alisema Wema.

ZITTO NAYE
Jitihada za kumpata Zitto aweze kuzungumzia kurejea kwa penzi la Wema na Diamond kwenye tamasha aliloliandaa, hazikuzaa matunda. Muda wote naibu huyo wa Kambi ya Upinzania Bungeni, simu yake ilikuwa imezimwa.

WANANCHI WAMPONGEZA
Fununu kuwa Wema na Diamond wamerudiana zilivuma kwa kasi ndani ya mitandao ya kijamii na maoni ya wengi yakaelekeza pongezi kwa Zitto, kwani kabla ya hapo, mastaa hao walikuwa na uhasama mkubwa.

UNAKUMBUKA?
Malumbano yao kwenye vyombo vya habari? Diamond alipomfedhehesha Wema baada ya kukataa kupokea fedha zake alizomtuza kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam Machi mwaka huu? Je, kauli nzito za Mama Wema, Mariam Sepetu kwamba Diamond ni kijana mbaya na hafai?

JIULIZE SASA
Mpaka hapo bado unabisha kwamba mapenzi ni upofu? Unaendelea kukataa kwamba mapenzi hayaulizwi kwa nini? Diamond alipoachana Wema, alitua kwa Miss Tanzania namba mbili 2006-07, Jokate Mwegelo, je, penzi lao limeyeyuka au bado lipo kwa sura gani?


Labels: , , ,

Tuesday, July 10, 2012

Diva Loveness Asema “Atakae Taka Kunioa Mahari Si chini Ya Mil 500

Mwana dadiva anaeendisha kipindi cha ala za roho ndani ya the people’s station Diva loveness love jana amefunguka alipokuwa akifanya kipindi cha xxl na mtu mzima Adam Mchomvu kuwa kwa yeyote atakae jitokeza kumuoa basi lazima awe na si chini ya shilingi millioni 500.
Diva Loveness love akiwa studio..

Labels: , ,

Sunday, July 8, 2012

MB DOG AJA NA 'ONLY YOU'

Ni miaka kama minne imepita tangu mwanamuziki na mkali wa miondoko ya bongo flava nchini Mb Dog kuachia ngoma zake. Sasa Mb Dog ameachia ngoma kali na mpya inayokwenda kwa jina la 'Only you'. Kwa mujibu wa Mb Dog amefunguka nakusema kuwa ngoma hii ni zawadi kwa mashabiki wake ambao walikuwa wakimsubiri kwa muda mrefu bila kutoa nyimbo yeyote."sasa nimekuja kuwashika tena, najua mtafurahi na track yangu hii.."
alionge Mb Dog alipokuwa akifanyiwa interview na moja ya radio hapa bongo.

Labels: