Tuesday, July 10, 2012

Diva Loveness Asema “Atakae Taka Kunioa Mahari Si chini Ya Mil 500

Mwana dadiva anaeendisha kipindi cha ala za roho ndani ya the people’s station Diva loveness love jana amefunguka alipokuwa akifanya kipindi cha xxl na mtu mzima Adam Mchomvu kuwa kwa yeyote atakae jitokeza kumuoa basi lazima awe na si chini ya shilingi millioni 500.
Diva Loveness love akiwa studio..

Labels: , ,

BIBI WA MIAKA 92 ABEBA UJAUZITO..

Bibi wa miaka 92 alibeba ujauzito kwa zaidi ya Miaka 60 na bibi huyo aliyejulikana kwa jina la Huang Yijun alifanikiwa kujifungua mtoto wa kike bada ya kubeba mimba kwa zaidi ya nusu ya century.
Bibi Huang Yijuu akiwa katika pozi na mimba yake
 

Labels: , ,

ADELE APEWA UJAUZITO..

Mwanamziki wa kimataifa kutoka uingereza ambaye mwaka huu alivunja rekodi kwa kujikombea tuzo za grammy's sita na anatamba vilivyo na album yake ya kwanza na pekee inayokwenda kwa jina la 21,Adele..anategemea kujifungua ndani ya mwaka huu..
Adele akiwa katika pozi.

Labels: ,

Monday, July 9, 2012

THE GLORY OF RAMADHAN KWENYE MAANDALIZI..

Ile filamu kali ya kibongo inayosubiriwa kwa hamu kubwa katika kipindi hiki kijacho cha mwezi mtukufu wa ramadhani 'GROLY OF RAMADHANI'  iliyowakutanisha mtangazaji maarufu wa East african radio 'Abdallah Hamis Ambua' ama Dullah wa planet bongo na  Vincent Kigosi ama Ray sasa ipo katika maandalizi ya mwisho kabisa. Filamu hiyo ambayo imelenga kabisa maadili ya kiislamu haswa katika mfungo wa ramadhani.
Dullah na Ray katika pozi kabla hawajaingia kuigiza hiyo movie.
Wala usishangae ukajua Ray kabadili dini? wala! hapa nikatika hiyo movie mpya ambapo iliwachukuwa mpaka ndani ya msikiti.
Chuchu Hans akiwa katika pozi na Dullah ndani ya hiyo movie..
Ray akifuatilia kwa karibu maandalizi ya movie..
Dullah akijiandaa kuigiza katika hiyo movie.
Ray akiwa na Chuchu Hans ndani ya hiyo movie..
Ray akiwa na Nesh wakiigiza.

Labels: ,

MAJAMBAZI WAVAMIA MGODINI NAKUUA..

Kundi kubwa la majambazi limevamia mgodi wa Buhemba, Musoma na kukata kata watu mapanga nakisha kuchukua mali pia na kuwachapa wengine risasi usiku wakuamkia ijumaa tarehe sita. kama unavyoona Mungu wape nguvu na afya nzuri.

Labels:

Sunday, July 8, 2012

Mawasiliano katika Mahusiano...



Leo katika tasfiri zetu nitaanza na tafsiri ya Umuhimu wa Mawasiliano katika mahusiano ambao ni msingi mkuu katika misingi mitano ya mahusiano ama ndoa bora.
Mawasiliano mazuri katika mahusiano ni moja ya suala muhimu sana linaloweza kusaidia mahusiano yenu yawe na mafanikio.

Siyo kila mtu anajua namna bora na makini ya kuwasiliana kwa kuzaliwa nayo, hata hivyo tunaweza kujifunza. Basi kama una matatizo ya mawasiliano mazuri katika mahusiano yako unaweza kujifunza kwa kusoma makala hii.
Ukijifunza mbinu za kuwasiliana kila inapobidi na kwa namna inayotakiwa utaweza kusaidia mahusiano yako kuwa bora na yenye furaha na kuepuka kubaki katika mashaka ya ndoa yako kuingia katika orodha ya ndoa zilizovunjika.
Mawasiliano hayana maana ya kuongea tu. Kipengele muhimu sana katika mawasiliano ni uwezo wa kuwa msikivu. Wakati mwingine ni hilo tu linahitajika, kusikiliza tu!
Mwenzako anaweza akawa anahitaji kusikilizwa tu ili kuweza kutatua tatizo ama kuondoa mashaka yaliyokuwapo. Kama utahitajika kujibu ama kuelezea kuhusu jambo fulani basi baada ya kumsikiliza mwenzako kwa umakini mkubwa wote wawili kwa pamoja mnapaswa kujaribu kujadiliana na kufikia muafaka wa tatizo husika.
Mawasiliano ni suala pana kwa ujumla, ni pamoja na maneno ya kutamkwa na mambo ambayo si ya kutamkwa-matendo ama ishara. Mbinu za mawasiliano makini katika mahusiano zinajumuisha namna zote mbili za kuwasiliana na kuziainisha kwa uhakika.

Tuchukue mfano, kama mpenzi ana hasira, anaweza akakaa amefumbata mikono kimya akikutizama tu bila kusema neno. Hali kama hiyo ni jambo ambalo linahitaji umakini wako wa haraka. Kama utanyamaza na kumwacha bila ya kufanya chochote utasababisha ajisikie kususwa, kutohitajika na kupelekea mambo kuwa mabaya zaidi. Kusoma sura na matendo ya mwenzako ni kipaji ambacho unapaswa kufanyia kazi vyema. Kinakuwezesha kuelewa mambo mengi sana kuhusu mwenzako anavyojisikia kwa wakati fulani na kugundua hata kama anadanganya.

Kama wewe ni mtu makini na mwerevu basi unaweza kugundua mbinu mbalimbali za mawasiliano makini kwa kutilia maanani tu mambo yanayoendelea katika mazingira uliyopo. Ni vyema kama unahitaji msaada zaidi ili kuelewa mbinu mbalimbali za mawasiliano mazuri ukahudhuria mafunzo maalumu au kusoma vitabu mbalimbali kuhusu jambo hilo. Hii inaweza ikakugharimu kidogo lakini thamani yake itakuwa kama dhahabu pale ambapo itaweza kukusaidia kuokoa ndoa ama mahusiano yako.

Mawasiliano mazuri ni pamoja na kutoa kipaumbele hata kwa mambo madogo madogo na kumwonyesha mwenzako kwamba anathaminiwa. Kumwambia asante mpenzi wako isiwe ni jambo gumu. Kuonyesha kuridhishwa na jambo fulani ni ukarimu wa kawaida katika maisha.

Usichoke ama kukata tamaa kutamka, “NAKUPENDA”, ama “ASANTE” au “POLE” ama muhimu zaidi "SAMAHANI". Maneno haya ni vyema yakawa sehemu muhimu sana ya mahusiano yenu. Kila mtu anahitaji kujisikia anathaminiwa.

Uelewa ama maelewano ni sehemu nyingine muhimu katika mawasiliano ambayo imeachwa bila kufanyiwa kazi. Tukisema bila kufanyiwa kazi ina maanaisha kwamba mara nyingi katika mazingira mbalimbali ya mahusiano, hayaulizwi maswali ya kutosha kuweza kuweka mambo bayana. Tunadhania kwamba tunajua kile ambacho wenzetu wanakiongelea bila kutaka kueleweshwa vizuri zaidi. Kudhania mara nyingi kutakupeleka katika matatizo. Hivyo hakikisha unaelewa kwa uhakika ni nini kinaongelewa. Kama huelewi, uliza maswali hadi pale kila kitu kitakapokuwa wazi na kueleweka.

Ushauri bora kwa suala hili ni kujifunza, kujaribu, kujaribu na kujaribu. Jifunze mbinu za mawasiliano bora na makini katika mahusiano na kufanyia majaribio kila siku. Baada ya muda yatakuwa kama asili yako na hutapata tabu tena ya kufikiria namna ya kuwasiliana.

Kumbuka, bila juhudi na kujitolea kuwa na mawasiliano makini na bora katika mahusiano, mahusiano hayo ni sawa na mahusiano-mfu!

Anza sasa kuwasiliana ipasavyo… na jenga mahusiano/ndoa bora!

Labels: ,

Maelewano katika Mahusiano..



Mahusiano ni kama mchanga uliowekwa katika kiganja cha mkono wako, utakapoushika vizuri na wazi, mchanga huo utabakia kuwa katika kiganja. Pale utakapojaribu kufunga mkono, kuminya na kubana kwa nguvu mkono wako ili kuuzuia mchanga huo, basi bila shaka utaanza kupenya katikati ya vidole vyako na kumwagika chini. Utaweza kuuzuia kiasi utakapoanza kumwagika, lakini mwingi utaishia chini. Mahusiano ndivyo yalivyo.
Yakupasa kumkubali mwenzako kwa nia njema na malengo yaliyo wazi ili kuweka maelewano ya pamoja kati yenu, na kwa namna hiyo mahusiano yenu yatashamiri. Mahusiano yakiachwa kuwa wazi lakini kwa kuheshimiana na uhuru baina ya wawili ni rahisi kuendelea kuwa imara. Lakini yanapobanwa ama mmoja wapo kumtawala mwenzie na kuwa na mamlaka zaidi, mahusiano hayo yataponyoka, kuyayuka na hatimae kupotea.

Mahusiano mengi ambayo yanashindikana na hatimaye kuelekea kuvunjika, talaka na kuachana hutokana na sababu kubwa ni : baada ya muda fulani katika mahusiano, mawasiliano yanapungua baina ya wawili hao, kutokuelewana kunajitokeza na maelewano katika mambo ya msingi yanatoweka!
Sababu nyingine kubwa ambayo inapelekea kuvunjika kwa mahusiano ni kutopeana muda wa kutosha kuwa pamoja kama wapenzi, katika dunia ya leo yenye changamoto nyingi kujitolea muda kuwa pamoja na mwenzako, familia ama ndugu imekuwa ni tatizo kubwa.
Tatizo kubwa zaidi katika mahusiano linakuja hasa kutokana na sababu watu wengi wanajiingiza katika mahusiano ili kupata kitu fulani: wanajaribu kupata mtu ambaye atawafanya wajisikie vizuri.
Ukweli ni kwamba , namna pekee ambayo unaweza kupangilia mahusiano yako yaweze kudumu na kushamiri ni kuwa tayari kujitolea zaidi kuliko kutegemea kuwa mpokeaji tu katika mahusiano yenu!
Talaka na kutengana katika mahusiano huacha madhara makubwa sana kwa wahusika hasa kwa upande wa afya zao; usumbufu wa akili hutokea, na matatizo kama midhaiko na ukosefu wa amani. Kumukumbu za mahusiano yaliyopita hukuandama na kusababisha kujishushia heshima, kutokujiamini na mambo mengine kama hayo.
Ni vigumu sana kupita katika matatizo kama hayo na kuweza kuhimili hali kama hizi baada ya kutokea. Hutokea hali ya kutojiamini tena na kuogopa kuingia katika mahusiano mengine ama kukurupuka na kujiingiza katika mahusiano mbalimbali bila kutafakari. Mara nyingi uwezo wa kufikiri na hata wa kufanya kazi wa watu waliokumbwa na matatizo kama haya hupungua, na hubadilika toka kuwa yenye kujenga zaidi na kuwa ya kubomoa zaidi kwa maisha binafsi ya wahusika. Madhara haya hutokea katika mazingira amabayo muhusika anapambana kujiweka katika hali ambayo atajisikia kila kitu kiko sawa kwa upande wake, wakati inakuwa sivyo.

Jambo ambalo linasababisha UELEWA/ MAELEWANO kuwa jambo gumu zaidi ni kuwa yatupasa zaidi kusikiliza na kuelewa nafasi ya upande wa pili wa wenzetu ambao tuna mitazamo tofauti. Hatupaswi kukubaliana nao, lakini hatuna budi kuwasikiliza. Labda, kutokana na ustaarabu yanaweza kutokea maelewano ya pamoja namna gani kila mmoja ameelewa namna mwenzake anavyochukulia na kuamini katika jambo husika… hata kama mwisho wa siku mtakuwa hamkubaliani kati yenu bado.
Hivyo, kabla hujakumbwa na bahati mbaya ya kujiingiza katika mahusiano yatakayoishia kuvunjika ama talaka, chukua tahadhari kumwelewa na kuelewana na mpenzi wako vizuri zaidi, ni vyema kila mmoja akajua uwezo na udhaifu wa mwenzi wake na namna gani anaweza kukabiliana na mapungufu yatakayojitokeza.
Jumapili njema...

Labels:

Uaminifu katika Mahusiano...

Wasalaam wapendwa wote,

Happy Sunday kwenu nyote na kila la kheri katika kuijenga nchi yetu na maisha binafsi kwa kila mmoja wetu.

Tukianza wiki mpya na mwezi mpya, nawapa pole ndugu zetu wa Kenya kwa mashambulio yanayoendelea dhidi yao, Mungu awalinde.
Wapendwa wataalam wetu wa tiba na hasa madaktari, kauli ya mkuu mtakuwa mmeisikia, chonde chonde tuweke utaifa mbele kwa maslahi ya maskini na wale wanaoteseka zaidi na walio wengi.

Wiki hii basi nitaendele na tafsiri zetu za misingi bora kwa mahusiano na ndoa bora!

UAMINIFU KATIKA MAHUSIANO..
Uaminifu ni msingi wa mahusiano yenye ukaribu, salama na ya mafanikio. Uaminifu ni lazima upatikane kwa stahili, uenziwe na kulindwa na uwe wa kudumu!

Kujenga uaminifu na kuamini kwamba mpenzi wako ni mwaminifu kwako siyo mambo rahisi hasa kwa wale ambao wamewahi kusalitiwa uaminifu wao.Hili ni tatizo kubwa katika jamii zetu kwani kusalitiana limekuwa jambo la kawaida!
Pale imani yako inapo vunjwa inakuwa vigumu kuweza kuwepo tena katika mahusiano yako. Makala hii itakusaidia kuelewa njia ambazo zitakusaidia kurudisha imani hiyo.
Uaminifu lazima uwe jambo la kila wakati na siku zote ili mahusiano yaweze kudumu.

Uaminifu ni muhimu katika mahusiano ya aina zote uwe wamapenzi, kifamilia na hata katika urafiki wa kawaida.

Faida gani mtu anapata anapokuwa mwaminifu katika mahusiano?

· Kwa kuanzia, kuwa katika mahusiano ya kimapenzi kuna faida nyingi kwa mwili, watu walio katika mahusiano bora ya mapenzi huishimaisha marefu na kufurahia afya njema kuliko wale wasiokuwa katika mahusiano ya aina hiyo. Faida hii haina pingamizi kwa sababu ya ukweli kwamba watu wanaokuwa katika mahusiano ya karibu wanajijengea hisia na nguvu fulani ambayo huwasaidia kusaidiana na kujaliana wakati wa shida. Siyo tu kwamba watu walioko katika mahusiano ya aina hii wanaishi muda mrefu lakini pia ni kweli kwamba wanakuwa na furaha na wanaridhika na maisha kuliko wale wanaoshindwa kukaa katika mahusiano.

· Pili, kuwa katika mahusiano mazuri ya mapenzi kunasaidia katika mambo mbalimbali ya kimahitaji. Kusaidiana katika mahitaji mbalimbali baina ya wapenzi ni njia nzuri ya kuwa na maendeleo. Watu wawili wanaoshirikiana pamoja mara nyingi watakuwa na maisha mazuri zaidi ya yule anayefanya peke yake. Unapokuwa na mtu karibu wa kusaidiana naye katika mahitaji ni rahisi kupata mafanikio.

· Tatu, Watu walio katika mahusiano mazuri wanapata msaada wa kijamii; kwa maana ya kuwa na mtu karibu ambaye anajali mahitaji yako ya msingi na hisia zako. Kuwa na msaada wa aina hii kuna faida nyingi, mojawapo muhimu ni kuweza kufanya maamuzi ya busara bila kuwa na mtindio wa mawazo na hofu ama mashaka.

· Nne, kuwa na mwenza katika maisha hufanya maisha kuwa ya faraja zaidi. Kuwa na mtu ambaye mnaweza kushirikiana mambo madogo madogo ya maisha kama kuangalia Tv, kutembea, kula pamoja ni muhimu; inaboresha mahusiano na mara nyingi watu walio katika mahusiano ya aina hii wamekuwa na maisha bora zaidi.

· Tano, Mahusiano ni muhimu kwa sababu wapenzi wana kawaida ya kuangaliana tabia zao hasa zile ambazo ni haribifu, na wamekuwa na kawaida ya kuonyana ama kushauriana kuacha kufanya mambo mabaya na tabia mbaya. Kwa mfano watu walio katika mahusiano ya karibu wamekuwa na tabia ya kujaribu kuwashauri wapenzi wao kuacha kuvuta sigara, kupunguza pombe, kuacha kutumia madawa ya kulevya nk.

· Mwisho, Watu walio katika mahusiano bora ya kimapenzi wanafanya mapenzi mara nyingi zaidi kuliko wale walio pekee. Kufanya mapenzi mara kwa mara, kimpangilio ni muhimu kwa afya bora ya mwili na akili. *Ni muhimu kuzingatia kwamba kufanya huko mapenzi ambako ni bora kwa afya ya mwili siyo kubadilisha wanaume ama wanawake, ila ni kwa mwenza wako ama mke au mume na katika hali ya maelewano, uhuru na amani lakini pia kwa utaratibu unaostahili ndiyo upelekea kuleta faida hiyo.
Baada ya kusema yote hayo, ni ukweli kwamba mahusiano mazuri baina ya wapenzi huwa na faida nyingi kwa watu wenye bahati ya kupata mtu wa kumpenda na hatimaye nao kupendwa pia.

Hatua muhimu katika kujenga uaminifu zitafuata…



 

Labels:

Jamaa nomaa

Mfalme mmoja aliwaita watu kijijini akasema shujaa atakayeogelea kwenye hili bwawa la mamba nampa binti yangu mara akasikia PWAAA!jamaa kajitosa kaogelea mpaka upande wa pili mfalme akasema nitakupa binti yangu na mali jamaa akasema"SITAKI BINTI YAKO WALA MALI NAMTAKA MTU ALIYENISUKUMA KWENYE BWAWA ATANITAMBUA LEO!"

Labels:

MB DOG AJA NA 'ONLY YOU'

Ni miaka kama minne imepita tangu mwanamuziki na mkali wa miondoko ya bongo flava nchini Mb Dog kuachia ngoma zake. Sasa Mb Dog ameachia ngoma kali na mpya inayokwenda kwa jina la 'Only you'. Kwa mujibu wa Mb Dog amefunguka nakusema kuwa ngoma hii ni zawadi kwa mashabiki wake ambao walikuwa wakimsubiri kwa muda mrefu bila kutoa nyimbo yeyote."sasa nimekuja kuwashika tena, najua mtafurahi na track yangu hii.."
alionge Mb Dog alipokuwa akifanyiwa interview na moja ya radio hapa bongo.

Labels:

KASEBA APEWA USHINDI, CHEKA AGOMA KUPIGANA..

Lile pambano la kukata na shoka kati ya bondia maarufu na mkali hapa bongo Japhet Kaseba na mkali mwingine kutoka Morogoro Francis Cheka jana halikufanyika baada ya Francis Cheka kukataa kuingia ndani ya uwanja kupigana na kumwamulu refarii ampe ushindi Kaseba.




Bondia Francis Cheka akitoka nje ya ulingo baada ya kugoma kupigana jana.


Labels:

WEMA SEPETU NA JACKLINE WOLPER NGOMA DROO..


Lile pambano lililokuwa linasubiliwa kwa hamu kubwa ndani ya tamasha la matumaini ndani ya uwanja wa taifa hatimaye lilifanyika jana na liliwakutanisha adui wawili wa bongo movie kati ya Wema Sepetu na Jackline Wolper. Mpambano huo mkali ambao ulianza kwa mbwembwe nyingi kabla na baada ya mpambano ambapo kila mmoja alikuwa na matambo kuwa atamgalagaza mwenzake vya kutosha. Kama kawaida ya mashabiki wao kazi ilikuwa ni macho kutazama na midomo kupiga makelele kwa shangwe na msisimko mkubwa ndani ya uwanja wa taifa. Mpambano huo ulichukuwa raundi mbili tu tofauti na ilivyotazamiwa ambapo maadui wote wawili walitoka ngoma droo huku kila mmoja akimpiga mwenzake vya kutosha.

Jackline wolper akijiandaa kuingia ndani ya uwanja kupambana na Wema Sepetu jana..



Kocha wa Wema Sepetu, Rashidi Matumla akimpa mbinu Wema sepetu jinsi ya kumpiga Jackline Wolper



Muamuzi akiwaachanisha Wema na Wolper baada ya kutupiana makonde..



Wema Sepetu akila tizi muda mfupi kabla hajaingia kwenye mpambano kati yake na Jackline Wolper

Labels: